Kwanini Magomeni Mwembe Chai inafanana na Morogoro?

Kwanini Magomeni Mwembe Chai inafanana na Morogoro?

James Hadley Chase

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2020
Posts
1,984
Reaction score
3,695
Magomeni, Mikumi, Kimamba, Rudewa na Kidodi. Ni miongoni mwa Kata zilizopo Wilayani Kilosa, mkoa wa Morogoro.

Mji wa Turiani, Dakawa na Mziha, ni miongoni mwa Kata zilizopo Wilayani Mvomero, Mkoa wa Morogoro. Na Matombo (yaani matiti ya mwanamke), ni sehemu ya milima iliyopo Wailaya ya Gairo, Mkoani Morogoro.

Sasa najiuliza... Hivi ni kwanini baadhi ya majina haya 👉 kutoka mkoani Morogoro, yaje kutamba ktk mkoa wa Dar es Salaam, hususan Magomeni Mwembe-Chai?

Eneo la Magomeni Mwembe-Chai, jijini Dar es Salaam. Kuna Mitaa ya Kimamba, Rudewa, Kidodi, Dakawa, Mziha, Mikumi, Turiani na Matombo... Ambapo majina hayo yanapatikana ktk Kata na maeneo ya mkoa wa Morogoro... Hivi ni kwanini? Je, nani aliita majina hayo ktk Mitaa ya Magomeni Mwembe-Chai?

Inasemekana kwamba, asili ya jina MAGOMENI, ilitokana na miti iliyokuwa inapatikana maeneo hayo 👉Miti hiyo ilikuwa na Magome mengi na makubwa. Hivyo kupelekea eneo hilo kuitwa Magomeni.

Je, ni nani aliyeita eneo hilo Magomeni? Je, kabla ya kuitwa Magomeni kufuatia hiyo miti yenye 'magome' kwanza eneo hilo lilikuwa likiitwaje?
 
Moro na Dar na mkoa wa pwani ni milki za warugulu


Pia warugulu na wazaramo wanatumia lugha moja
 
Eneo la Magomeni Mwembe-Chai, jijini Dar es Salaam. Kuna Mitaa ya Kimamba, Rudewa, Kidodi, Dakawa, Mziha, Mikumi, Turiani na Matombo... Ambapo majina hayo yanapatikana ktk Kata na maeneo ya mkoa wa Morogoro... Hivi ni kwanini? Je, nani aliita majina hayo ktk Mitaa ya Magomeni Mwembe-Chai?
Huenda kuna watu wa huko waliishi mitaa hiyo
 
Back
Top Bottom