hayaland
JF-Expert Member
- May 4, 2012
- 712
- 399
Nimekuwa nikijiuliza sana kwa nini makampuni makubwa kama ya magari mfano NİSSANİ,VOLVO,SCANIA na mengine ikiwa ni pamoja na mashirika makubwa ya ndege kama vile BRITISH AIRWAYS,AMERICAN AIRLINES,EMIRATES,ITALIAN AIRWAYS,KLM,na mashirika mengine ya ndege yana safari zake nchini Kenya,
Vyombo vya habari vikubwa navyo haviko nyuma katika kuwekeza nchini Kenya,CNN,SKY,BBC,AL JAZEERA na vingine vingi wanazo ofisi zao Nairobi,ndo maana hata habari ndogo ndogo za Kenya zinarushwa na vyombo hivyo.
Tanzania tunao mkakati gani kuwashawishi wenye makampuni makubwa kama haya japo sio yote kuja na kuwekeza nchini mwetu? Nimeona hata kama takwimu zinadai uchumi wetu unakua kuliko wa Kenya bado hatutaweza kushindana na wenzetu Kenya.
Hata mabarozi wanaoziwakilisha nchi zao,kama barozi anawakilisha nchi yake katikaTanzania na Kenya,barozi huyo atapenda zaidi kuishi Kenya na sio Tanzania,hapa nchini atakuja tu na kurudi Kenya .
Pamoja na história kutuhukumu kuwa Kenya wawekezaji walikuja miaka mingi enzi za ukoloni(colonialism) bado nchini yetu inalo la kufanya ili KUWEZA kuwa na wawekezaji wakubwa kutoka ulaya na Marekani.
Vyombo vya habari vikubwa navyo haviko nyuma katika kuwekeza nchini Kenya,CNN,SKY,BBC,AL JAZEERA na vingine vingi wanazo ofisi zao Nairobi,ndo maana hata habari ndogo ndogo za Kenya zinarushwa na vyombo hivyo.
Tanzania tunao mkakati gani kuwashawishi wenye makampuni makubwa kama haya japo sio yote kuja na kuwekeza nchini mwetu? Nimeona hata kama takwimu zinadai uchumi wetu unakua kuliko wa Kenya bado hatutaweza kushindana na wenzetu Kenya.
Hata mabarozi wanaoziwakilisha nchi zao,kama barozi anawakilisha nchi yake katikaTanzania na Kenya,barozi huyo atapenda zaidi kuishi Kenya na sio Tanzania,hapa nchini atakuja tu na kurudi Kenya .
Pamoja na história kutuhukumu kuwa Kenya wawekezaji walikuja miaka mingi enzi za ukoloni(colonialism) bado nchini yetu inalo la kufanya ili KUWEZA kuwa na wawekezaji wakubwa kutoka ulaya na Marekani.