Kwanini mamlaka husika haitoi tamko juu ya kuzuiwa kwa baadhi ya mitandao?

blackhawk

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2020
Posts
262
Reaction score
587
Habarini wakuu ,

Ni zaidi ya siku kadhaa baada ya kuwepo kwa zuio la baadhi ya mitandao hasa ya kijamii nchini

Sites kama AppStore , PlayStore , YouTube, Instagram, WhatsApp, Telegram , JamiiForums na baadhi ya sites zenye resources za applications, programs na habari

Watu wengi kwa asilimia kubwa wanaweza sema zuio ni kwa ajili ya kupunguza habari zisizo rasmi kusambaa hasa kipindi cha uchaguzi mkuu

Ndio ni sababu muhimu kwa upande wa hasara lakini si wote wanaitumia kwa sababu hizo ni kwa asilimia fulani

Kumekua na mazui ya mitandao kwa nchi nyingi tu ila huwa linakuepo tamko rasmi na sababu ya kuzui mtandao huo na mamlaka husika huwa zinatoa njia mbadala baada ya zuio hilo kwa wale walio kua wanautumia

Mfano China wamefungia Mitandao ya ki marekani mfano google na apps zote za Mark Zuckerberg (WhatsApp, Instagram etc..) kwa sababu za kiusalama dhidi ya marekani na wali tengeneza apps zao mbadala mfano WeChat na App Stores zao

Sasa kwa nini kwetu baadhi ya mitandao imefungwa na hakuna mbadala hata store hazifunguki kutafuta mbadala

Wafanya biashara wengi sasa hv wanatengemea mitandao hiyo kama njia ya kutangaza na kuuza bidhaa zao,

Wanafunzi pia kkwa asilimia kubwa kutengeneza makundi yao kurahisisha mawasiliani ya kimasomo lakini pia Kufanya mawasiliano ya njia ya video kwa watu walio nje ya nchi kibiashara , ki elimu hata ki mahusiano pia

YouTube ni sehemu huria ya kujifunza vitu vipya kupitia Tutorials mfano mimi ndio huwa najifunzia vitu hasa (how to solve different tasks ) career yangu inahitaji sana tutorials

Apps stores tunashindwa hata kupakua productive apps mfano juzi nataka ku install app ya CRDB SimBanking ikashidikana hadi nilipapata njia mbadala ya mtandao wa ki binafsi (VPN)

Mtando wa ki binafsi (VPN ) una faida zake na hasara zake tofauti na mtandao wa umma (public network)

Hasara kubwa ni kukosa kasi kama ilivyo kwa mtandao huru maana inatumia njia ndefu kufika kwa mlengwa ili tu kujiweka kibinafsi (private) na kugushi eneo la mtumaji (sender) inabidi itumie server zinazipatikana eneo husika kwa hivyo route inakua ndefu ndio maana inakua slow

Ni nzuri kuficha mawasiliano lakini sio nzuri kwa kasi kiufanisi

Ombi langu ni vyemba mamlaka husika itoe tamko rasmi watu wajue na itoe njia mbadala kwa watakao athirika na tamko hilo

UH-60Blackhawk
 
Umewezaje kupost hapa kama umezuiwa?
 
Umepost kwa kutumia nn
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…