Kwanini Masai hawarogani wala kuibiana wao kwa wao tofauti na makabila mengine?

Kwanini Masai hawarogani wala kuibiana wao kwa wao tofauti na makabila mengine?

YEHODAYA

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2015
Posts
36,902
Reaction score
52,001
Kuna kitu kinanishangaza kuhusu wamasai. Ni kawaida kwa makabila mengine kulogana, kutuhumiana uchawi, kuibiana na kutapeliana.

Masai hivyo vitu havipo kwenye kabila yao najiuliza ni kwanini?

Mwenye jibu atusaidie.
 
Kuna kitu kinanishangaza kuhusu wamasai.Ni kawaida kwa makabila mengine kulogana ,kutuhumiana uchawi ,kuibiana na kutapeliana.

Masai hivyo vitu havipo kwenye kabila yao najiuliza Ni kwa Nini?

Mwenye jibu atusaodie
Wao wanalogana kwenye mifugo tu kimaendeleo
 
hata kwenye kesi za ajabu ajabu huwezi wakuta, sana sana mifugo au baadhi zinazoendana na tamaduni zao,
 
Huwajui wamasai wewe, mimi niko nao kila siku kwenye shughuli zangu, wanaloga balaa ila sasa wao unakuta asilimia kubwa mganga wao ni mmoja.
 
Ukifika masaini ulizia kitu kinachoitwa macho(nimesahau neno la kimaasai) huo ni uchawi mmoja hatari sana,ulizia idadi ya wamasai waliofia kwenye karamu za nyama, hujaishi nao ukawajua vizuri.
 
Ndugu ukiwa waandika jambo fanyia uchunguzi kwanza. Sasa umeandika jambo ambalo hata hulijui

Uliza wanaoishi nao huko Arusha,Manyara,Pwani,Tanga na morogoro wakupe majibu.

Kifupi ni zaidi ya kulogana tena kama ni ndugu wako tayari kumuuwa hata mzee waje warithi mali
 
Ndio shida ya mtu wa Dar aliyezoea kuwaona wamasai wakiwa walinzi, wanasuka dada zetu na kuuza 'sendozi',ugoro etc hapo dar.

Njoo 'site' uwaone wamasai org ndio utajua wanalogana au wanafanyaje?
 
Wanatuita Orumekii
Kabisa mkuu,huyu mtoa mada hawajui hawa watu kabisa.[emoji1][emoji1][emoji1],akiwaona wanasuka nywele hapo Dar anajua ni jamaa wa ukweli kumbe sio binadamu kabisa. Anakuja shambani kwako analisha ng'ombe ukiongea wanakuja kibao na mafimbo na sime,shughuli yake hapo ni mpaka polisi waende.
 
Back
Top Bottom