Kwanini mtoto akiamka analia?

Joined
Sep 27, 2015
Posts
83
Reaction score
15
Hi wanaJF
Kama kuna mwenye uelewa juu ya hili la mtoto akiamka analia basi naomba anijuze tafadhali
 
Anaashiria kitu fulani kati ya hivi
1. Anategemea kumuona mtu anayemjua pembeni yake akiamka...ikiwa tofauti lazima ahamaki hivyo kupelekea kulia
2. Amejisaidia na anahitaji msaada...watotot wengi waki~puu au kukojoa wanajisikia Hali tofauti hivyo hulia kuashiria anahitaji msaada wa kusafishwa
3. Homa za vipindi...mtoto akiwa na Homa Mara nyingi hupata ahueni akiwa usingizini hivyo usingizi ukiisha anaamka na anahisi Homa tena lazima atalia

Kwa ujumla mtoto hulia kuashiria jambo fulani ambalo ni tofauti na Hali ya kawaida kwake.
 
4. Ameamka na ana njaa.... fungua hotel
 
pia punguza kelele na epuka kuwa mkali sana kwa mtoto mdogo, jitahidi kumfurahisha muda mwingi ili kumpunguzia ndoto mbaya zitakazomfanya ashtuke kutoka usingizini.
 
Kawaida sana...labda njaa, kajisaidia, anahis joto au baridi, upweke na sio mara zote atalia chunguza utaona. Wengine wanaamka na kuanza kuchezacheza...hakuna mchawi wala shetan
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…