Kwanini mtoto mchanga anachomwa sindano kwenye paja na sio matakoni?

Kwa watoto chini ya miaka mitatu misuli ya tako "gluteus" inakua bado haijadevelop vya kutosha hivyo sehemu nzuri kuchoma sindano ni msuli flani wa paja unaitwa "vastus lateralis" ambao ndo unakua na unene wa kutosha na fat hivyo kuzuia sindano isipitilize na kufikia mifupa , pia baada ya miezi sita hivi sehemu nyingine inayoweza kutumika ni sehemu ya juu ya mkono "deltoid muscle" na hapo ndipo ambapo chanjo nyingi huchomwa mf.tetanus. hivyo tako si salama kwa mtoto kwa kua linakua halina unene wa kutosha hivyo sindano inaweza kupitiliza mpaka kwenye mifupa.

karibuni Ze Heby, HERNANDEZ kwa nyongeza
 
asante dr trigeminal
 
naongezea kwa mkuu trigeminal hapo, ukiachilia mbali swala kukomaa kwa musles, pia uptake ya dawa kutoka kwenye paja iko haraka kuliko kwenye tako, lakini pia kuna complication za hizi sindano ambazo ni nafuu zikitokea kwenye sehemu ya paja kuliko ziliko gluteals, mfano swellings, ulcers na hata abscess
 
Pia Sindano Kuchomwa Matakoni Yaweza Kumuongezea Maumivu Kwakuwa Mtoto Mchanga Mara Nyingi Hulala Chali.
 
Nahisi paja lina minofu ya kutosha kuliko kalio
 

Dr. Trigeminal nisaidie. Nikimeza kitu koo inauma sana. Hasa nikila maharage ninapata shida sana kooni kumeza. Ni masahibu gani haya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…