Kwanini nchi ya "Mozambique" tuliamua kuuita "Msumbiji" tofauti na nchi zingine za jirani zinazopakana na Tanzania zilizobaki na majina ya Kiingereza?

Egypt kuitwa Misri
 
Funny thing Italia ni exactly Sawa na wanavyojiita wao..
 
Wait... hizo nchi zingine ambao ni majirani zetu ni kwamba zina majirani ya Kiingereza au labda majina yametolewa na Wakoloni au yalistawi zama za ukoloni baada ya jamii mbalimbali kuwekwa kwenye pande moja la ardhi lililoitwa nchi, na kisha majina husika yakaanza kutumika?!

Anyway, jibu fupi ni kwamba nchi ZOTE ambazo ni majirani zetu, kama nchi husika ina jina la Kizungu basi ama tulibadilisha na kuleta jina la Kibantu au tulitohoa kutoka kwenye uzungu hadi kwenye Uswahili!

Kwa haraka haraka, naona majina yote ya hizo nchi ulizosema "nyingine" zenyewe zina majina ya Kibantu au yenye origini ya Kibantu na kwahiyo hatukuwa na sababu ya kubadilisha!

Kenya kwa mfano.., the word sounds like a Bantu Word! Uganda bila shaka linatokana na Buganda, Baganda or anything like that! Na yenyewe ni ya Kibantu! The same to Burundi, Rwanda, Zambia, Zimbabwe!!!

Tusisahau, Zambia ilikuwa ni Northen Rhodesia (kama sikosei coz' am not an historian guy) lakini baadae wakabadilisha na kuwa Zambia! Hiyo inaonesha wazi wenyewe waliachana na jina la Kizungu na kutumia la Kibantu ambalo hatukuwa na sababu ya kubadilisha manake hata mzee asiye na meno anaweza kutamka Zambia!

Kinyume chake, hata kama sifahamu KIreno bado nasikia harufu harufu za Ureno kwenye neno Mozambique! Iistoshe, HATUNA herufi Q kwenye Kiswahili! Na kwa maana hiyo, tulikuwa na kila sababu ya kuachana na neno la Kizungu na kuja na la kwetu wenyewe lenye taste ya Kibantu!!

Lakini pale tuliposhindwa kupata jina linaloendana na lugha yetu kama tulivyofanya kutoka Mozambique to Msumbiji, basi tulitohoa!! Kwa mfano, hautuiti Comoro bali Ngazija au Komoro!

Hatuiti Democratic Republic of Congo bali Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo! Enzi za Mobout, hatukulazimika kutohoa wala kutafuta jina la Kiswahili/Kibantu kwa sababu Zaire lenyewe tayari lilishakuwa jina la Kibantu!!
 
Okay...
 
Hata wao hawaiiti msumbiji wala mozambique, nchi yao inaitwa Moçambica (inatamkwa mosanbiki).

Kwahiyi hata hilo jina la kiingereza sio lao, point yangu ni kwamba hiyo ni kawaida kabisa. Baadhi ya lugha hamua kubadili majina ya nchi / watu na kuvipa majina ya lugha zao.

Mifano mingine ni Deutschland (Germany), España (Spain), Italia (Italy), La France (France), Misr (Egypt) n.k

Mifano ya majina ya watu, Job (Ayubu), Noah (Nuhu), Yeshua (Jesus / Yesu) n.k
 
Hata wao hawaiiti msumbiji wala mozambique, nchi yao inaitwa Moçambica (inatamkwa mosanbiki).

Kwahiyi hata hilo jina la kiingereza sio lao, point yangu ni kwamba hiyo ni kawaida kabisa.
Tanzania ni nchi inayotumia kiingereza kama moja kati ya lugha mbili rasmi ndio maana nikafanya reference katika hilo...
 
Tanzania ni nchi inayotumia kiingereza kama moja kati ya lugha mbili rasmi ndio maana nikafanya reference katika hilo...
Ni kweli, lakini hatujatafsiri jina la msumbiji peke yake. Italia, uingereza, marekani, urusi, afrika ya kusini n.k yote ni majina ya kiswahili.

Kwakua watanzania wengi wa kawaida lugha yao ya kwanza ni ama kiswahili au lugha ya kabila lake, inaleta maana zaidi kwa majina hayo ya kiswahili kuwa maarufu zaidi.

Lakini ukienda kwenye nyaraka zilizoandikwa kwa kiingereza haotokuta hayo majina ya kiswahili.

Kwahiyo kila jina linatumika kwenye mazingira sahihi kwa lugha sahihi.
 
Sawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…