Kutwa
JF-Expert Member
- Aug 29, 2016
- 238
- 717
Habari wakuu,
Hivi hili neno Kilaza lilizoeleka kutumika vizuri tu kumuwakilisha mtu asiye na maarifa fulani huku akijifanya maarifa hayo anayo. Kinachonishangaza neno hili limekuwa likitumika kama tusi kubwa sana jukwaani kwa siku za hivi karibuni.
Najua kuna baadhi ya watu hutakiwi kulitumia kuwawakilisha wao ila hata humuhumu na id zetu unakuta mtu akitaka kulitumia anaweka dot(.) katikati mfano kila.za au kil.aza nk. wengine wanaweka ****** na ukishakutana na hizo nyota sita hapo unajua kabisa jamaa kaitwa Kilaza.
Je mods wanatoa ban ukitumia neno "Kilaza" kama lilivyo au.
Halafu kuna ndugu zetu wale wa Kilimanjaro ambao hili jina wengine unakuta ni la ukoo kabisa kama la yule ambaye chimbuko la hili jina lilipatikana tutakuwa tunawaita na Mr. ****** kweli.
Tuwape uhuru na wengine neno kilaza litumike tu vizuri panapostahili. Tuwapeni uhuru na wenye majina yao mbona matusi ya kuwekewa * yanajulikama wakuu.
Nawasilisha.
Hivi hili neno Kilaza lilizoeleka kutumika vizuri tu kumuwakilisha mtu asiye na maarifa fulani huku akijifanya maarifa hayo anayo. Kinachonishangaza neno hili limekuwa likitumika kama tusi kubwa sana jukwaani kwa siku za hivi karibuni.
Najua kuna baadhi ya watu hutakiwi kulitumia kuwawakilisha wao ila hata humuhumu na id zetu unakuta mtu akitaka kulitumia anaweka dot(.) katikati mfano kila.za au kil.aza nk. wengine wanaweka ****** na ukishakutana na hizo nyota sita hapo unajua kabisa jamaa kaitwa Kilaza.
Je mods wanatoa ban ukitumia neno "Kilaza" kama lilivyo au.
Halafu kuna ndugu zetu wale wa Kilimanjaro ambao hili jina wengine unakuta ni la ukoo kabisa kama la yule ambaye chimbuko la hili jina lilipatikana tutakuwa tunawaita na Mr. ****** kweli.
Tuwape uhuru na wengine neno kilaza litumike tu vizuri panapostahili. Tuwapeni uhuru na wenye majina yao mbona matusi ya kuwekewa * yanajulikama wakuu.
Nawasilisha.