Kwanini ni vigumu sana kupata "A" katika vyuo vyetu? Tunawahujumu wanafunzi wetu?

Kwanini ni vigumu sana kupata "A" katika vyuo vyetu? Tunawahujumu wanafunzi wetu?

Yo Yo

JF-Expert Member
Joined
May 31, 2008
Posts
11,210
Reaction score
1,720


Matokeo ya Mwaka wa nne Mlimani
1. Kwa shahada ya kwanza pale Mlimani gredi zenyewe zimekaa hivi (kama hazijabadilika) A: 75-100, B+: 70-74, B: 60-69, C: 50-59, D: 45-49 na E: 0-44 2. Gredi za hapa Marekani (kutoka katika silabasi yangu katika darasa la Language and African Society) zimekaa hivi: A: 93-100, A-: 90-92, B+: 87-89, B: 83-86, B-: 80-82, C+: 77-79, C: 73-76, C-: 70-72, D+: 67-69, D: 63-66, D-: 60-62, E: 0– 59. Japo profesa unaweza kujipendekezea gredi zako mwenyewe, mfumo huu wa alama ndio umependekezwa na chuo kwa wanafunzi wa shahada ya kwanza. 3. Hali ilivyo kule nyumbani (kama bado haijabadilika)

  • Utakuta darasa lina wanafunzi 100, na kati ya wanafunzi hawa pengine wawili, watatu na hata mmoja tu ndiyo atapata "A". Hata madarasa makubwa yenye wanafunzi 300, eti wanafunzi wanne au watano tu ndiyo wanapata "A". Kwa nini? Ni kwa sababu masomo ni magumu sana? Wanafunzi hawajisomei sawasawa (Na kama hawajisomei ni kwa nini?), maprofesa hawafundishi vizuri kiasi kwamba wanafunzi hawawaelewi? Au maprofesa wanatunga mitihani migumu kupindukia? Au pengine wanafunzi wa vyuo vikuu vyetu ni mbumbumbu na hawana uwezo wa kupata A?

  • Ninacholalamikia hapa siyo kila mwanafunzi kupata A bali ule ugumu uliopo wa kupata alama hizi kwani siamini kama kweli eti katika darasa la wanafunzi 300, ni wanafunzi watatu au wanne tu ndiyo wana uwezo wa kufaulu vizuri. Kama hivi ni kweli basi ni wazi kuna tatizo kubwa katika mfumo wetu wa elimu.
4. Hali ilivyo hapa Marekani

  • Hapa kupata A ni jambo la kawaida na maprofesa na wanafunzi wanalijua hili. Mahusiano kati ya wanafunzi na maprofesa ni ya wazi na wanafunzi wanaweza kuuliza maswali na kujadili masuala ya gredi watakazozipata na maprofesa wao kwa uwazi. Hali hii inasababisha matatizo fulani na haya nitayaongelea siku nyingine.

  • Kwa wanafunzi wanaotegemea kuendelea na shahada za uzamili na uzamivu ni lazima wahakikishe kwamba wanapata A kwa sababu ushindani wa kupata ufadhili ni mkubwa sana na vyuo vingi vinataka wanafunzi ambao ni bora kabisa. Kwa ujumla alama za B, na hata B+ na pengine A- hazimsaidii sana mwanafunzi kuweza kujiunga na vyuo vikuu vyenye hadhi kama Harvard, Yale, Columbia, UCLA, Stanford, Berkeley na vinginevyo
5. Uzoefu Wangu

  • Nina uzoefu na uteuzi wa wanafunzi wa shahada za uzamili na uzamivu hapa Marekani na huwa nashangaa sana kugundua kwamba kwa kawaida waombaji kutoka Afrika huwa na alama za chini sana hasa ikilinganishwa na waombaji kutoka sehemu zingine duniani kama China, Korea, Ulaya, Amerika ya Kusini na hata nchi za Uarabuni. Maprofesa hapa huwa wanajiuliza inawezekanaje mwanafunzi mwenye azma na ari ya kujisomea ashindwe kupata A (75) ambayo hapa ni C? Na kama hakuna profesa wa kuwafahamisha wanakamati wenzie wanaofanya uteuzi kuhusu mambo yalivyo, mara nyingi maombi ya wanafunzi kutoka Afrika huwa hafifu sana na huishia kutupiliwa mbali. Ndiyo maana nahoji hapa kwamba pengine tunawahujumu vijana wetu kwa kuwapa alama za chini na kuishia kuwakosesha ufadhili ambao ungewawezesha kusomeshwa bure. Na sijui mfumo huu unamsaidia nani.
6. Ilivyokuwa Kwangu

  • Mwaka 1997 nilipata nafasi ya ufadhili wa kusoma shahada za uzamili na uzamivu katika Idara ya Isimu pale UCLA ambapo pia nilitakiwa kufanya kazi kama mwalimu msaidizi wa Kiswahili. Barua ya mwanzo niliyopata ilikuwa na masharti mawili yaliyonichanganya na kuninyima usingizi. Sharti la kwanza lilisema kwamba ilikuwa ni lazima nipate "first class" katika shahada yangu ya kwanza na la pili ni kufanya mtihani korofi wa GRE.

  • Sharti la kwanza liliwashtua watu wengi sana na niliambiwa kwamba kwa muda mrefu kulikuwa hakujawa na mtu aliyepata hiyo "first class". Niliambiwa kwamba pengine hawa jamaa wa UCLA walikuwa hawataki niende na niliambiwa kuachana nao kwani walichokuwa wananiomba kufanya kilikuwa hakiwezekani. Kilichonishangaza ni kwamba kulingana na matokeo yangu ya miaka mitatu iliyopita, ningeweza kupata hiyo first class kama ningepata angalau A nne tu katika mitihani yangu ya mwisho ya mwaka wa nne. Na kupata A nne katika masomo 10 niliyokuwa nikisoma eti ilikuwa haiwezekani. Sikukubali!
7. Nilichokifanya na Matokeo Yake

  • Sijawahi kusoma kwa nguvu zaidi, ari zaidi na kasi zaidi kama katika kipindi kile katika maisha yangu yote mpaka nikapachikwa majina ya "Librarian", mkazi wa "Special Reserve", "Aliyetumwa na kijiji" na mengineyo. Sikujali!

  • Matokeo ya mwaka wa nne yalipotoka nilikuwa nimepata A tisa, B+ moja na B moja. Nilikuwa nimeipata hiyo "first class!" tena nzuri. Haraka haraka niliyatuma matokeo hayo UCLA na msimamizi wangu (ambaye anafahamu ugumu wa kupata first class) alifurahishwa sana kiasi kwamba aliiomba kamati ya ufadhili kufuta sharti la mimi kufanya mtihani wa GRE. Habari hizi kuhusu GRE hata hivyo zilikuwa zimechelewa kwani tayari nilikuwa nimeshaanza maandalizi na nilikuwa nimeshalipia ada (dola 120). Niliufanya mtihani huu ili kujipima nguvu tu lakini first class tayari ilikuwa imesharekebisha mambo. Na hivi ndivyo nilivyoweza kusomeshwa UCLA kwa miaka sita (mitatu shahada ya uzamili na mitatu shahada ya uzamivu) huku nikilipiwa karibu dola 30,000 kwa mwaka.
Risti ya malipo ya GRE

  • Ati, kwa nini ni vigumu sana kupata A na hatimaye "first class" katika vyuo vikuu vyetu? Tatizo hasa ni nini? Ni mfumo wa elimu tuliorithi kutoka kwa Waingereza? Pengine inabidi tulifikirie jambo hili kwani inawezekana tukawa tunawahujumu wanafunzi wetu kwa kuwapotezea nafasi za ufadhili katika mashirika mbalimbali vikiwemo vyuo vikuu, jambo ambalo si jema hasa katika kipindi hiki ambapo kusema kweli mambo yako wazi sana kuhusu masuala ya ufadhili wa kimataifa.
Source:MATONDO: KWA NINI NI VIGUMU SANA KUPATA "A" KATIKA VYUO VYETU? TUNAWAHUJUMU WANAFUNZI WETU ???
 
Omba kazi ya ufundishaji, halafu kifike kipindi cha usahihishaji, hapo ndipo utakapojua kuwa ni kwanini A hazipatikani kwa wingi. I bet wewe unaweza usitoe hata B+ kwa aina ya wanafunzi waliopo vyuoni leo.
 
Omba kazi ya ufundishaji, halafu kifike kipindi cha usahihishaji, hapo ndipo utakapojua kuwa ni kwanini A hazipatikani kwa wingi. I bet wewe unaweza usitoe hata B+ kwa aina ya wanafunzi waliopo vyuoni leo.
Tatizo nini? hawana akili au? inawezekana kuwa wanafunzi wa tz wasiwe na akili zaidi ya wa nchi nyingine?? na ni kwanini hawana akili kama ndio sababu.....
mfumo wetu wa elimu unajenga wanafunzi wasome na waelewe mwisho wa siku wapate A?
 
Wale walimu wamepata ile kazi kwa msuli kweli kweli...they like to see few reach where they reached...the GPA of above 3.8 in the past
 
Tatizo nini? hawana akili au? inawezekana kuwa wanafunzi wa tz wasiwe na akili zaidi ya wa nchi nyingine?? na ni kwanini hawana akili kama ndio sababu.....
mfumo wetu wa elimu unajenga wanafunzi wasome na waelewe mwisho wa siku wapate A?

Hebu fikiria mchapo huu, ni jana tu nilikuwa naongea na mwanafunzi mmoja wa Mwalimu Nyerere Memorial University, nikamuuliza vipi matokeo yako ya mwaka wa kwanza? Akasema ni mazuri ana GPA ya 4.1 ambayo kiukweli ni matokeo mazuri sana yenye A kibao, yeye anasema ni mwanafunzi wa Economics of Development, nikamwambia aniambie kwa kifupi tu course yake inahusu nini, chali hakujibu lolote, nikamwuuliza achague eneo lolote katika course yake (topic) ambayo yeye yuko mahiri zaidi, akachagua micro economics, nikamuuliza ni ma-author gani ambao ni nguli katika uwanda huo? Chali, hakuweza kumention hata mmoja, na cha kusikitisha zaidi I'm telling truth aliuliza ma-authors ndio kina nani? Sasa that's it, sio kwamba A hazipatikani, no zinapatikana katika vyuo flaniflani kirahisi tu pengine, lakini jee hao ni A students? Jibu utakuwa nalo mwenyewe.
 
Mfumo wa University/College kwa hapa bongo ni mbovu sana!! mwalimu wako wa darasani ndiye atakayesahisha mtihani wako wa semester na kukukabidhi GPA...this is very big prob by the way
 
Sithan kama hizo ndio grade ambazo tunazitumia hapa UD. Nadhani sasa hivi wamebadilisha. Ninakataa. Ila mbona kupata A inawezekana tu ukiamua? Ukiingia na coursewrk ya maana UE mbona unapata tu. Mbona mimi kuna masomo nimeipata?
 
Hebu fikiria mchapo huu, ni jana tu nilikuwa naongea na mwanafunzi mmoja wa Mwalimu Nyerere Memorial University, nikamuuliza vipi matokeo yako ya mwaka wa kwanza? Akasema ni mazuri ana GPA ya 4.1 ambayo kiukweli ni matokeo mazuri sana yenye A kibao, yeye anasema ni mwanafunzi wa Economics of Development, nikamwambia aniambie kwa kifupi tu course yake inahusu nini, chali hakujibu lolote, nikamwuuliza achague eneo lolote katika course yake (topic) ambayo yeye yuko mahiri zaidi, akachagua micro economics, nikamuuliza ni ma-author gani ambao ni nguli katika uwanda huo? Chali, hakuweza kumention hata mmoja, na cha kusikitisha zaidi I'm telling truth aliuliza ma-authors ndio kina nani? Sasa that's it, sio kwamba A hazipatikani, no zinapatikana katika vyuo flaniflani kirahisi tu pengine, lakini jee hao ni A students? Jibu utakuwa nalo mwenyewe.

Same way jana niliongea na dent wa mwaka wa kwanza Mwalimu Nyerere College....same nae anasomea Economics Development...na mada ambayo lecturer wake ana boa ni ile ya macro-economics..nilivyomuuliza kuhusu matokeo akasema anatarajia suppl 2 na results bado haijatoka!! Bt she is somehow empty kwa anavyojieleza!!
 
Mkuu nmefurahshwa xana na ufafanuz wko thabiti!Mi ni undergraduate ktk chuo kikuu kimoja hapa tz!Ukwel ni kwamba TATIZO NI MFUMO 2lorith toka kwa wakolon!Istoshe PYRAMID SYSTEM ndo kinachotuua African states as some lecturers feel hppy wen FEW reach ze top
 
Kutana na mwenye A then mwambie aitafsiri kwa vitendo utalia. Mara nyinigi nimekutana na wenye PASS field wapo fit kwa vitendo kuliko hayo ma A. Nadhani hata mwanafunzi anapotamani A ajiulize kama ataweza kuitetea kibaruani. A zimetuumbua wengi
 
Hebu fikiria mchapo huu, ni jana tu nilikuwa naongea na mwanafunzi mmoja wa Mwalimu Nyerere Memorial University, nikamuuliza vipi matokeo yako ya mwaka wa kwanza? Akasema ni mazuri ana GPA ya 4.1 ambayo kiukweli ni matokeo mazuri sana yenye A kibao, yeye anasema ni mwanafunzi wa Economics of Development, nikamwambia aniambie kwa kifupi tu course yake inahusu nini, chali hakujibu lolote, nikamwuuliza achague eneo lolote katika course yake (topic) ambayo yeye yuko mahiri zaidi, akachagua micro economics, nikamuuliza ni ma-author gani ambao ni nguli katika uwanda huo? Chali, hakuweza kumention hata mmoja, na cha kusikitisha zaidi I'm telling truth aliuliza ma-authors ndio kina nani? Sasa that's it, sio kwamba A hazipatikani, no zinapatikana katika vyuo flaniflani kirahisi tu pengine, lakini jee hao ni A students? Jibu utakuwa nalo mwenyewe.
Kwa hiyo kwa maelezo yako tatizo ni wanafunzi wenyewe? hivi kweli unataka kusema ni woote maana kuna baadhi ya fani hakuna first class kabisa miaka zaidi ya mi5....hiki kizazi ni vipi? na kama huyo kwa maelezo yako kapata GPA hiyo lakini ianonekana ni bonge la kilaza....je tatizo ni yeye mkuu?????? tafakari..

Mkuu nmefurahshwa xana na ufafanuz wko thabiti!Mi ni undergraduate ktk chuo kikuu kimoja hapa tz!Ukwel ni kwamba TATIZO NI MFUMO 2lorith toka kwa wakolon!Istoshe PYRAMID SYSTEM ndo kinachotuua African states as some lecturers feel hppy wen FEW reach ze top
wow.....unasomea kozi gani mkuu?
 
Kutana na mwenye A then mwambie aitafsiri kwa vitendo utalia. Mara nyinigi nimekutana na wenye PASS field wapo fit kwa vitendo kuliko hayo ma A. Nadhani hata mwanafunzi anapotamani A ajiulize kama ataweza kuitetea kibaruani. A zimetuumbua wengi
mkuu kwanini mtu upate A na ushindwe kuitetea kibaruani?? tatizo nani? mwanafunzi au mwalimu au nini? au CCM arifu?
 


Same way jana niliongea na dent wa mwaka wa kwanza Mwalimu Nyerere College....same nae anasomea Economics Development...na mada ambayo lecturer wake ana boa ni ile ya macro-economics..nilivyomuuliza kuhusu matokeo akasema anatarajia suppl 2 na results bado haijatoka!! Bt she is somehow empty kwa anavyojieleza!!

You see? Picha inakuja yenyewe
 
Kutana na mwenye A then mwambie aitafsiri kwa vitendo utalia. Mara nyinigi nimekutana na wenye PASS field wapo fit kwa vitendo kuliko hayo ma A. Nadhani hata mwanafunzi anapotamani A ajiulize kama ataweza kuitetea kibaruani. A zimetuumbua wengi

Good observation, na mimi binti yule nilimueleza awe tayari kuprove, kwa watu makazini ama kokote atakapo pata nafasi, kivitendo na kwa uelewa kwamba kweli ni wa alama hizo. Sababu ukiwa na Cheti chenye A kibao na watu watakua wanakuexpect kudeliver ki-A-A tu.
 
You see? Picha inakuja yenyewe
post zenu ni coincidence....
au ni sawa kama alivyosema Prof matondo..
kama katika kipindi kile katika maisha yangu yote mpaka nikapachikwa majina ya "Librarian", mkazi wa "Special Reserve", "Aliyetumwa na kijiji" na mengineyo. Sikujali!
 
Mi nasoma shahada ya biashara ktk menejiment ya utalii na ukarim!Ninachokiona ni kuwa wapo wachache wanaopata A's ambapo weng wao hawabahatish pa1 na kwamba few ktk hao wanababaisha!kwan elim ya chuo ka unajua unajua tu ukisubir kubahatisha inakula kwako!
 
Sithan kama hizo ndio grade ambazo tunazitumia hapa UD. Nadhani sasa hivi wamebadilisha. Ninakataa. Ila mbona kupata A inawezekana tu ukiamua? Ukiingia na coursewrk ya maana UE mbona unapata tu. Mbona mimi kuna masomo nimeipata?

Utakuwa umedesa sana vibuti na nondo nyingine kama si uongo tutajie somo ulilopata A kama sio la ngwini na tupe hesabu kama haujaegemea kuti kavu ndo nyie mmeambiwa mkiulizwa swali after exam mmeshasahau.
 
sijui kwakweli, labda nwdays hatuna akili,
lakini kule bcom kule kuna walimu wanajua kukomoa sijaona?? anatunga mtihani mgumu majibu yake mwenyewe hana hadi aende kudownload kitabu tena unalipia uko uko online!
ss maisha gan hayo, wengi wao pia wanakomoa watu wawaogope kwa idadi ya sup!
 
Hebu fikiria mchapo huu, ni jana tu nilikuwa naongea na mwanafunzi mmoja wa Mwalimu Nyerere Memorial University, nikamuuliza vipi matokeo yako ya mwaka wa kwanza? Akasema ni mazuri ana GPA ya 4.1 ambayo kiukweli ni matokeo mazuri sana yenye A kibao, yeye anasema ni mwanafunzi wa Economics of Development, nikamwambia aniambie kwa kifupi tu course yake inahusu nini, chali hakujibu lolote, nikamwuuliza achague eneo lolote katika course yake (topic) ambayo yeye yuko mahiri zaidi, akachagua micro economics, nikamuuliza ni ma-author gani ambao ni nguli katika uwanda huo? Chali, hakuweza kumention hata mmoja, na cha kusikitisha zaidi I'm telling truth aliuliza ma-authors ndio kina nani? Sasa that's it, sio kwamba A hazipatikani, no zinapatikana katika vyuo flaniflani kirahisi tu pengine, lakini jee hao ni A students? Jibu utakuwa nalo mwenyewe.

Mwalimu Nyerere Memorial Academy wako shallow sana, sasa we ulikuwa unategemea nini!?
 
Back
Top Bottom