Kwanini ni vizuri kujuana magroup yenu ya damu kabla ya kuoana?

Annointed

Member
Joined
Oct 13, 2011
Posts
46
Reaction score
8
Wanajamvi,Hivi kuna umuhim wa kujuana groups za damu kwamba zinaendana or not??Jee nini madhara ya groups kutokuendana??Na jee group O aoe mtu wa group gan?Group A,AB pia wafaa kuoana na watu wa groups zipi?
 
unaweza oa mtu wa group lolote. kila group lina rhesus factor(Rh) positive+ au negative- hicho ndio wanachoangalia.
Mf: mama akiwa rh- na baba rh+, mtoto atakuwa rh+. Hivyo antibodies za mama zitashambulia rb cells za mtoto na kusababisha matatizo hata kifo iwapo tu damu zao zitagusana.
 

Kwahiyo ni vyema kuoana wote mkiwa na rh zinazofanana?Kama ni positive wote muwe positive na kama negative wote muwe negative ili kuepuka matatizo hayo hasa kifo cha mtoto?
 
mkuu danny job tafadhali njoo maana nimeanza kuogopa njoo ujibu

Ww si strong umeanza kuogopa nini ha ha ha ha!Anyway nimekua nikishuhudia vifo vya watoto wa dada yangu na wanasema tatizo ni magroup ya dam ya wazazi,Yan mtoto akikaribia kutembea baaasi anafariki,imekua ikiniumiza sana nimeona ni heri nije humu tujuzane mapema
 
wakuu Hiyo kitu ni kwere, kuna jirani yangu imemtokea Mara mbili...tena Mara ya pili mtoto ameishi kwa week 2 tuu...

Hebu mdau anaeelewa Haya mambo vizuri aje hapa adadavue vizuri, na if kuna prevention methods... tupee tuu..😱
 
Kwa uelewa mdogo nilionao mimi ni kwamba watu wa rh- ni wachache sana sana duniani kiasi kwamba probability ya kukutana nae ni ndogo karibu na hakuna. Katika nchi ambazo zipo serious wanakuwa wanajulikana kabisa katika database za hospitali. Wajuzi wa mambo watatujuza zaidi
 
Kwahiyo ni vyema kuoana wote mkiwa na rh zinazofanana?Kama ni positive wote muwe positive na kama negative wote muwe negative ili kuepuka matatizo hayo hasa kifo cha mtoto?

mara nyingi mtoto wa kwanza anaweza akatoka salama, shida ni kwa wanaofuata wanaweza kupata matatizo kiafya au kifo.
Pia watu wenye Rh- ni wachache sana.(Rh- maana yake huyo mtu hana rhesus factor).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…