Kwanini Niyonzima hajawahi kuitwa nchi yeyote kufanya Trial?

demigod

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2015
Posts
8,292
Reaction score
15,250
Hili swali huwa najiuliza Mara nyingi sana, licha ya Jamaa kuwa na uwezo kwenye kusakata kabumbu ....Hivi kwanini hatujawahi kusikia jamaa akihitajika sehemu Fulani akafanye trials kama wenzake akina Ndemla, Ajibu, Msuva na Mkude au kama Mao?

Ina maana uwezo wa huyu Jamaa umepitwa na viungo hao wote? Licha ya kusifiwa sana kuuweza mpira.

Je hivi jamaa miaka yote amekuwa akiwa Overrated kwenye soka la Bongo?

Maana hili jambo huwa haliniingii kumkichwa kabisa.
Unaweza kusema labda hayuko exposed sana kwenye mazingira ya kuwa scouted, lakini mbona amezurura sana na wana Jangwani kwenye mechi za kimataifa? Kwann aonekane Msuva pekee.

Au kwanini aonekana Ndemla ambaye ni mara chache sana hupata namba kikosi cha kwanza?

Mnaonaje wana jamvi? Huyu jamaa anakuwa overrated au ni nini haswa?.
 
Kufanya majaribio wanaangalia na umri pia hao uliowataja wote wana umri mdogo kuliko Niyonzima pia Niyonzima ametoka Rwanda kuja kucheza soka la kulipwa Tanzania while hao uliowataja hawajawahi kucheza soka nje ya Tanzania
 
mkuu nio ameshakwenda mara nyinngi huko ulaya akiwa rwanda kabla hajajua dsm
 
Alishafanya trial Ufaransa wakiwa na yule kiungo wa zamani wa Azam Mugiraneza
 
Bado tu unaweweseka! Du! Ulimpenda kupita kiasi mkuu! Kubali matokeo!

Arage Jekundu.
 
Kufanya majaribio wanaangalia na umri pia hao uliowataja wote wana umri mdogo kuliko Niyonzima pia Niyonzima ametoka Rwanda kuja kucheza soka la kulipwa Tanzania while hao uliowataja hawajawahi kucheza soka nje ya Tanzania

Siyo sababu ya kutokuitwa nje zaidi ya Tanzania mbona Okwi, Mbuyu Twite wametokea hapa kwenda nchi zingine? Labda age ndiyo sababu.
 
Siyo sababu ya kutokuitwa nje zaidi ya Tanzania mbona Okwi, Mbuyu Twite wametokea hapa kwenda nchi zingine? Labda age ndiyo sababu.
Kule kwao Rwanda Niyonzima anaitwa mchezaji wa kimataifa sababu anacheza nje ya nchi yao,hawa wa kwetu ni domestic players

FYI
Kwa miaka aliyocheza bongo Niyonzima ni mchezaji wa kigeni ambaye amevuna fedha nyingi kuliko wote waliochezaTanzania
 
Bongo ni timu gani ambayo ni njiapanda ya kwenda ulaya ukipata jibu jiulize he nio yupo au alikua timu gani

nadhani umepata majibu mujarabu kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…