Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 9,189
- 16,128
Watanzania huwa tuna mambo ya ajabu sana. Tupo kinyumenyume sana. Kulima mazao kama mahindi mjini hakuna madhara yoyote, zaidi zaidi ni faida kwa mazingira ya mjini. Ni kama bustani mjini. Lakini utakuta miji mingi inasheria ya kutoruhusu mazao kama mahindi kupandwa mjini, wakitishia kuyakata.
Wanatoa sababu za wezi na kupendezesha mji. Sababu zisizo na mashiko yoyote. Maana mimea inafanya mji iwe mizuri na mjini hakuna mashamba ya kusema yatakuwa makazi ya wezi.
Lakini serikali hiyohiyo inaruhusu ufugaji wa kuku, ng'ombe, nguruwe, bata na mbuzi mjini. Hawa ni hatari sana kwa afya na mazingira. Wanasababisha harufu, wanaeneza magonjwa(hii ni hatari kubwa sana) na kuchafua mazingira.
Kwanini tunafikiri kinyume nyume? Kwanini hatupigi marufuku ufugaji mjini?
Wanatoa sababu za wezi na kupendezesha mji. Sababu zisizo na mashiko yoyote. Maana mimea inafanya mji iwe mizuri na mjini hakuna mashamba ya kusema yatakuwa makazi ya wezi.
Lakini serikali hiyohiyo inaruhusu ufugaji wa kuku, ng'ombe, nguruwe, bata na mbuzi mjini. Hawa ni hatari sana kwa afya na mazingira. Wanasababisha harufu, wanaeneza magonjwa(hii ni hatari kubwa sana) na kuchafua mazingira.
Kwanini tunafikiri kinyume nyume? Kwanini hatupigi marufuku ufugaji mjini?