Kwanini Serikali haitaki kubadilisha vifungu vya MOU ya DP world? Kama hakuna rushwa

Kwanini Serikali haitaki kubadilisha vifungu vya MOU ya DP world? Kama hakuna rushwa

Wamepokea ushauri wanatizama namna ya kutoka,inaitwa "nitoke vipi ya bwana misosi"
 
Milele ni tamu sana hawataki kuitema.
 
Wanabadilishaje wakati tayari washaweka saini zao?

Walitakiwa pale pale bungeni waombe mabadiliko yafanyike kisha uletwe mwezi wa 9 kupitiwa tena na kupitishwa kabla ya muda wake kuisha Mwezi wa 10
 


Hii ina uhusiano gani ya kurekebisha MOU
1688141119764.png
 
Walisha tafuta rushwa.. wengine wamesha nunua tofali, unataka wakazirudishe
 
Kama wamekula hela ya mwarabu wairudishe haraka sana. Hatutaki mkataba wa kimangungo!
Kuna tetesi kwamba mwarabu ametoka dollar millioni 500 kwa TPA,kama ni kweli Kuna uwezekano mkubwa sehemu ya fedha hizo imetembezwa mjengoni kwa akina msukukuma and co.
 
Tujiulize kama hakuna rushwa kwanini Serikali wanakuwa wagumu kukubali ushauri na kufanya marekebisho ya MOU kwa manufaa ya nchi. Mikataba ya baadae haitakuwa ya wazi! MOU ndiyo muhumu sana kufanyiwa marekebisho.
Watanzania hawapingi uwekezaji bali vifungu vya MOU!
MOU imetoka wapi tena ?

Huu uliopita bungeni mkataba
 
Msaada wa Dola za Marekani milioni 500 kupitia Mkataba wa Makubaliano uliosainiwa kati ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na kampuni ya usafirishaji ya DP World ya Dubai, utafadhili miradi mbalimbali inayolenga kuboresha ufanisi wa bandari za Tanzania. Kampuni hiyo ina utaalam wa usafirishaji wa mizigo, shughuli za bandari, huduma za baharini na maeneo ya biashara huria. Makubaliano ya msaada huo yalitiwa saini katika maonyesho ya Dubai Expo kati ya Mkurugenzi Mkuu wa TPA Eric Hamissi na Ofisa Mtendaji Mkuu wa DP World Sultan Ahmed Bin Sulayem na kushuhudiwa na Rais Samia Suluhu Hassan. Fedha za mkataba huo zitatumika katika kuendeleza bandari za Tanzania, zikilenga maeneo muhimu ya habari na mawasiliano, mifumo ya teknolojia (ICTs), mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi wa TPA na uboreshaji wa miundombinu ya bandari. Fedha hizo pia zinatarajiwa kuziwezesha bandari za nchi kuongeza uwezo wa kiushindani katika ngazi ya kikanda na kimataifa na kuboresha huduma.






Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tujiulize kama hakuna rushwa kwanini Serikali wanakuwa wagumu kukubali ushauri na kufanya marekebisho ya MOU kwa manufaa ya nchi. Mikataba ya baadae haitakuwa ya wazi! MOU ndiyo muhumu sana kufanyiwa marekebisho.
Watanzania hawapingi uwekezaji bali vifungu vya MOU!
CCM-CHUKUA CHAKO MAPEMA?
 
Msaada wa Dola za Marekani milioni 500 kupitia Mkataba wa Makubaliano uliosainiwa kati ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na kampuni ya usafirishaji ya DP World ya Dubai, utafadhili miradi mbalimbali inayolenga kuboresha ufanisi wa bandari za Tanzania. Kampuni hiyo ina utaalam wa usafirishaji wa mizigo, shughuli za bandari, huduma za baharini na maeneo ya biashara huria. Makubaliano ya msaada huo yalitiwa saini katika maonyesho ya Dubai Expo kati ya Mkurugenzi Mkuu wa TPA Eric Hamissi na Ofisa Mtendaji Mkuu wa DP World Sultan Ahmed Bin Sulayem na kushuhudiwa na Rais Samia Suluhu Hassan. Fedha za mkataba huo zitatumika katika kuendeleza bandari za Tanzania, zikilenga maeneo muhimu ya habari na mawasiliano, mifumo ya teknolojia (ICTs), mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi wa TPA na uboreshaji wa miundombinu ya bandari. Fedha hizo pia zinatarajiwa kuziwezesha bandari za nchi kuongeza uwezo wa kiushindani katika ngazi ya kikanda na kimataifa na kuboresha huduma.






Sent using Jamii Forums mobile app
Hahaha, kucheka nako ni afya.
 
Wabadilishe kwani wao ndio walio draft...by the way watu washasaini tayari....na wa kula washakula.
 
Back
Top Bottom