Kwanini Serikali imekuwa kimya sana kwa wazee wa Simba na Yanga

sammosses

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2011
Posts
1,687
Reaction score
1,111
KWANINI SERIKALI IMEKUWA KIMYA SANA KWA WAZEE WA SIMBA NA YANGA.

Tumetoka mbali sana na timu zetu za Simba na Yanga,kiumri ni sawa na timu hizi kuwa babu sisi wajukuu,timu zimeanzishwa miaka 1930's mpaka kufikia hapa si suala dogo.

Kwa miaka ya karibuni, kumeibuka wimbi la wapinga Maendele ambao hujiinua na kujifanya wanamiliki na hizi timu,kuliko mtu yeyote, hali inayo zorotesha maendeleo ya soka nchini .

Tumeona serikali kupitia BMT ikinyamazia sintofahamu hizi, ilihali ikifurahia mafanikio ya vilabu hivi kimataifa, wakati ikishindwa kuziunga mkono juhudi kufikia kilele cha mafanikio katika changamoto na figisu wanazo kumbana nazo.

Hizi si timu za mtaani, ni timu za wanachama zilizoko kihalali kwa mujibu wa sheria ya usajili wa vilabu vya michezo. Lakini mbali na kuwa vilabu vya michezo vinabaki kuwa taasisi ambazo zitakuwa za kibiashara zitakazo ingizia mapato serikali.

Kwa kuwa timu hizi zipo kisheria na mlezi wao ni Baraza La Michezo la Taifa, na kwa kuwa kufikia hatua ya kuzifanya kampuni hupitia mchakato wa vikao vya wanachama kwa mujibu wa katiba zao na sheria zilizowekwa na serikali, kwanini linapotokea suala la Kilomoni na Akilimali serikali inarudi nyuma.

Nasema Uakilimali na Ukilomoni umekuwa unakua kwa kasi na kurudisha nyuma sera ya michezo nchini ilihali serikali ipo kimya.

Tumeona viongozi wa vilabu wako magereza kwa kesi za utakatishaji pesa, lakini wahujumu uchumi wa mali za vilabu wenye kung'ang'ania hatimiliki za majengo wapo nje wanatembea. Hii si sawa katika misingi ya utawala bora.

Leo taifa linanufaika kwa maamuzi ya wanachama kukubali kuifanya club kuwa kampuni,uwakilishi wetu kimataifa umeongezeka, tumefungua wigo mpana wa utalii na uwekezaji nchini kupitia mpira, iweje mtu mmoja au kikundi kimoja kiturudishe kwa kuhodhi maazimio ya wengi.

Waziri mwenye dhamana ya michezo, chonde chonde, hatuna nafasi ya kupigania hatimiliki, tunataka hili suala liwekwe kisheria kwa maslahi mapana ya nchi zetu, tumechoka kubadilishana migogoro ya majungu kila mwaka kwa maslahi binafsi. Hizi ni timu za wananchi ziendeshwe kwa mujibu wa sheria na kanuni.
 
hao wazee ndio waanzilishi wa hizo timu, bila wao simba na yanga zingekuwa zimekufa siku nyingi toka enzi za mkoloni
 
Mkuu unataka serikali iingilie maamuzi ya club?? Hivyo vilabu havina chombo cha maamuzi (mkutano mkuu). Labda nizungumzie kuhusu simba, hivi simba ina mdhamini au mwekezaji?? Halafu kuna jambo sijaelewa, mnasema mo anahisa ya asilimia 41 na wanachama 51 je katika hizo 51 za wanachama wamefanya nn mpaka leo labda kulipa mshahara au kusajili mchezaji yeyote?? Kugharamia uendeshaji wa timu?? M naona mumuuzieni tu mo hiyo timu.
 
 
MO ni mfanyabiashara yuko simba kwa maslahi yake binafsi.
Tuongee kitaalamu, MO ni mwekezaji sawa, shareholder mwenzake ni wanachama, makubaliano aweke bilioni 20 kwa 49%,wanachama ukasema Mali zenu zinafikia B 22 ambazo hisa zenu 51% lakini tathimini ya mali za wanachama B 3.8 ,haya turudi kimahesabu ratio iko wapi, haya mwenye B 20 kasema lete hati yenu pamoja na mtaji wenu mdogo, ninyi mnataka aweke pesa ninyi muweke maneno si bora anunue bank!
 
Fresh tu we shida yako nn.
MO ni mfanyabiashara yuko simba kwa maslahi yake binafsi.
MO ni mfanyabiashara yuko simba kwa maslahi yake binafsi.
MO ni mfanyabiashara yuko simba kwa maslahi yake binafsi.
 
Watu mmekuwa mbumbu sana elimu ni muhimu sana.Simple question Abromovich yuko chelsea kwa maslai ya nani?
 
Unajua namna uanachama wa yanga ulivyokuwa unapatika miaka ya 1960.-1970 hivi, wengi kwasasa tungeshindwa kwa hz kadi za posta, niltaka kusema hao wazee tuwaheshimu kwa kuzfikisha hizi mpaka sasa.
Kuhusu mafanikio ya sasa nmabadlko ya kikanuni ya CAF, hii hatua ya simba sio hatua Mpya kwa vilabu vya tanzania, tena bila wawekezaji.
Mafanikio ya hao wazee.
Akilimali amefanikisha kufanyika kwa uchaguzi wa yanga,angalau wanayaona matumaini msimu ujao.
Kilomoni ,ameweza kutusaidia kujua imekuwaje MO awe mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya simba kabla ya kuweka pesa.
Pia yeye ana 49 aslmia, na wanachama 51,nani anastahili kumliki hati,? Au no anauziwa timu? Maana kama ni hizo liability na assets, uongozi tu unatosha kumuambia, Mo! Anafanya hoja za akina kilomon zpate nguvu.
 
Hivi tunajua maana ya uwekezaji? Mwekezaji hawezi kuwekeza pesa zake. Bila kuakikishiwa usalama wa pesa zake.

wewe una ngangania hati wakati hunataka pesa ziwekwe halafu zikipotea bila dhamana yeyote?

hata unapokwenda kukopa pesa lazima kuwe na kitu cha kuweka kama dhamana ili upate pesa.

swala la hati linapotoshwa sana na watu wa yanga kwa umbumbu usiojua kwamba kinachotakiwa ni dhamana ya mtaji na icho ni kitu cha kawaida.
 
Kama kung'ang'ania hati kwa Mzee Kilomoni ingekuwa uhujumu uchumi, basi angekuwa mahakamani. Acha demokrasia ichuke mkondo wake kwenye vilabu hivi. Binafsi simpendi Mzee Akilimali, lakini kamahavunji sheria, basi anayo haki kutoa mawazo yake ya ajabu ajabu.
 
Mzee Kilomoni usitoe hiyo hati tuone Mo na mbumbumbu wake maslahi watakufanya nini! Ukitaka hata ulinzi wewe sema tu! Tutakuletea makomandoo wetu wa pale Jangwani wakulinde masaa 24.
 
Mzee Kilomoni usitoe hiyo hati tuone Mo na mbumbumbu wake maslahi watakufanya nini! Ukitaka hata ulinzi wewe sema tu! Tutakuletea makomandoo wetu wa pale Jangwani wakulinde masaa 24.
Mbeleko ya chuma si mchezo, haya wale wa viti maalumu
 
UKWELI NI HUU,HATA SIKU MOJA SERIKALI HAITAKI HIZI TEAMS ZIWE STRONG KUPITIA MTU MMOJA,YALE YA MOISE KATUMBI NA TP MAZEMBE YAKE KUWA WORSHIPPED KAMA MUNGU HADI KUTAKA URAISI NI SOMO TOSHA.KINA MO DEWJI KINA MANJI HAWAKUBALIKI HATA SIKU MOJA KUWA JUU YA HIZI TEAMS THATS WHY HAT WALINYIMWA KUPATA SHARE YA 51 PERCENT WAKALAZIMISHWA KUWA NA 49.HIVYO VIZEE SIYO VIJINGA KUNA WATU NYUMA YAO
 
Aisee,kwahiyo serikali haitaki maendeleo ya mpira wa kwa taifa lake! Tuna safari ndefu sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…