Kwanini Simba wameshindwa kumsajiri Feisal Salum?

ESPRESSO COFFEE

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2014
Posts
6,170
Reaction score
7,665
Habari,

Kwa mwenendo ulivyo katika Timu ya Simba hasa upande wa kikosi, nilifikiri katika maboresho ya kikosi chao ili kuweza kufanya vizuri kimataifa na ligi ya ndani walikuwa wanahitaji mchezaji mzawa kama Feisal Toto.

Hili sakataka la Feisal Toto lilivyokuwa linakwenda ulikuwa ni wakati mzuri wa timu kubwa kuingilia kati na kumchukua Feisal juu kwa juu.

Simba ni wapi tutapata mchezaji mzawa aina ya Feisal Toto? Je, ni kwamba viongozi wetu hawakuona umuhimu wa kumchukua Feisal? Kwa misimu miwili sasa tumekuwa tukisajiri wa ndani kutoka Zanzibar na bara lakini wote wamekuwa hawaoneshi uwezo ule tunao utegemea. Huu ulikuwa ni wakati mzuri wa kulamba dume kwa Feisal Toto kwani ana uwezo ule ambao tunauhitaji katika timu yetu.

Itakuwa ni upuuzi kutafuta mchezaji mgeni wa aina ya Feisal Toto wakati tumemuacha ameenda Azam.

Huu sio wakati wa Simba kuzidiwa na Azam katika sajili, Azam alitakiwa kupigwa kanzu na sie kumchukua huyu kijana.

Naamini Simba tutakumbuka haya makosa ya mapema tunayo yafanya katika wachezaji wazawa.
 
Simba hawakushindwa kumsajili/kumnunua Feisal kwa vile hawataki mgogoro na Yanga juu ya kuchukuliana wachezaji kwani ingeonekana(na wengine walishasema hivyo) kuwa wao ndiyo wamemrubuni Feisal kuiasi timu yao.
 
Utachukuaje mchezaji amekaa miezi 6 bila kucheza mechi za mashindano,angechukuliwa ungekuwa upimbi wa kupindukia
 
Kwanza unatakiwa ujue Yanga haikuwa tayari kuruhusu Feisali aende Simba.

Hata mkataba wake unadaiwa kuna kipengele ambacho limewekwa sharti kuwa "hata endapo itatokea utaondoka Azam basi usiende Simba"

Ni kama mkataba wa Luis Miquoson ulivyowekwa, kuwa endapo atakuja hapa Tanzania basi priority ya kwanza ni Simba
 
Huu ndo ukweli hizo nyingine ni porojo tu. Kwa jinsi sakata lilivyokuwa ingekuwa kichekesho Simba kujitokeza na kuonekana ndo chanzo cha mgogoro. Na hata baada ya mgogoro kwenye mkataba mpya ilitegemewa kipengele cha kutoruhusu mchezaji kwenda timu wasiyoitaka kingewekwa. Miquisone aliwekewa kigingi akitoka Al Ahly lazima Simba iulizwe kama inamhitaji au la.
 
Fei anaenda kulipa deni, zile hela alizowalipa yanga zilikua za azam..alipofeli mpango ulea ndiomana alichanganyikiwa.
Hatahivyo fei hawezi kua kama alivyokua yanga.azamu kwa fei ni hasara na fei kwa azam ni hasara. Hasara pande zote.
Mbaya zaidi fei hawezi kupata ubora kama alioupata kwa nabi.
 
pale SSC kuna Mchezaji kasajiliwa dirisha dogo ingali ametoka kukaa Nje 2 yrs! Au
Sbb ni Foreigner?
 
Uwezo wenu ni kusajili wachezaji aina ya Nassoro Kapama. Hivyo siyo vizuri kuanza kutamani mambo yaliyo juu ya uwezo wenu.
 
Mcheki yule kocha wao scoobidoo anayeshangilia kwa kujiangusha kama yale mafisi ya lion king, namba yake 0754374093
 
hii ni plan ya azam simba wataingiaje?
 
Kwanini yanga walishindwa kumsjili chama.?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…