Kwanini ssra haijabadili formula za mafao kandamizi za mafao ya nssf na ppf?

Kwanini ssra haijabadili formula za mafao kandamizi za mafao ya nssf na ppf?

Kimla

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2008
Posts
3,810
Reaction score
6,599
Nashangaa mpaka sasa mafao ya uzeeni yatolewayo na NSSF na PPF ni kidogo ukininganisha na mchango we Mwanachama.Angalia mfano wa kweli hapa chini:

i)Juma Alistaafu tarehe 30/6/2012 baada ya kuchangia kwenye mfuko wa NPF na baadaye NSSF kuanzia 30/6/1988 kwa jumla ya miaka 24 (miezi 288). Mshahara wake wa mwisho ukiwa sh. 1,830,000 kwa mwezi. Kiasi alichochagia kwa kipindi hicho ni sh. 25,387,924 kabla ya kuweka faida na ukiweka faida ni zaidi ya sh. 28,000,000.

(ii) NSSF ilimlipa fedha ya mkupuo (commuted pension gratuity) sh. 9,805,908.32 na pensheni ya kila mwezi sh. 408,621.18. Hii ina maana kuwa ili achukue fedha zake zote zilizoko NSSF itamchukua miezi 44 sawa na miaka 4. Hii ni dhuluma ya hali ya juu.

(iii) Mwanachama wa PSPF aliyestaafu wakati mmoja na yeye na mwenye mshahara, kisomo na muda wa kuchangia kwenye mfuko sawa na yeye amepewa fedha za mkupuo (commuted gratuity) sh.90,782,284.80 na pensheni ya kila mwezi sh. 488,076.80. JE KWANINI SRA HAIOYAONI MANYANYASO HAYA?.KWA NINI WASIWEKE SHERIA YA MTU KUHAMIA MFUKO MWINGINE WENYE MAFAO BORA???
 
Basi wadau tupeane uelewa zaidi ili tuwa na maamzi ya busala katika kuchagua mifuko ya kujiunga
 
Back
Top Bottom