KERO Kwanini TANESCO hamna utaratibu mzuri wa kurejesha unit za mtu za umeme pale mnapobadili mita?

KERO Kwanini TANESCO hamna utaratibu mzuri wa kurejesha unit za mtu za umeme pale mnapobadili mita?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Wiki kadhaa zilizopita TANESCO walikuja kwangu kubadili mita (niliwaita kutengeneza kutokana na mita kuwa inajizima yenyewe, walipoitazama wakasema lazima iwekwe mpya) hivyo wakasema watakuja watu wataoweka hiyo mita.

Kesho yake mapema wakaja watu wengine kuniwekea mita, wakaangalia umeme uliopo Wakakuta nina unit nyingi, wakasema inabidi tusibadili maana una umeme mwingi na tukiweka nyingine hautaupata na kama ukiupata utakuwa umeteseka vya kutosha na utatumia muda mrefu mpaka uje kupata huo umeme.

Wakasema nitumie zikibaki unit kuanzia chache wakanitajia kiwango niwaambie waje, mmoja wao akaniachia namba kuwa nitapiga kuwajulisha, zilipobaki hizo walizosema nikawajulisha wakaja, Walipokuja wakasema mita wanayoweka ina unit kidogo na hizo unit nitatakiwa kuzilipa kila nikiweka umeme watakata 3000, nikawauliza vipi kuhusu hizi unit zangu chache mnazozichukua wakasema fanya kusamehe maana kuzipata ni mchakato mrefu na zitakutoa jasho.

Nikaongea katika utani kuwa siyo kwamba ndio inakuwa fidia maana zimelingana na mnazonipa hapa wakasema hapana hizo fanya tu kusamehe.

Nilichogundua wao wamejiwekea utaratibu wa kurudisha zao wanazokupa wakibadili ila hawana utaratibu mzuri wa kurejesha wanazochukua, na wanasumbua mpaka uziache.

Pia soma:
 
Watakuambia hilo ni suala technical sana
 
Mimi ilinitokea last year, walibadili mita wakaniambia niende kwenye ofisi zao nitapewa muongozo ili kupata Unit zangu za kwenye mita ya zamani, nikaenda ofisi yao ya pale kimara bucha nikawaelezea wakanipa form nikaijaza then nilikaa almost kama 2weeks nikatumiwa token
 
Aisee hii pia ilinitokea nilishindwa pa kupeleka malalamiko yangu kwa vile unit zilibak kama 15 hivi ila roho iliniuma.wenyewe zile za kwao unazozikuta kwenye mita yao chap ukiisha umeme unazilipa ..kwanini wao wanajiwekea kipaumbele kuliko walaji jamani?? Hii inch haina huruma...hicho hicho kidogo ulichonacho wanapita nacho wenye vikubwa
 
Pole mtoa mada hakika hiyo ni Tanesco ya awali lakini Kwa sasa hakuna tena mlolongo wa re-fund Kwa units , taja sehemu unapohudumiwa na Tanesco ili tuliweke sawa.
 
Back
Top Bottom