Kwanini Tanzania hatuchapishi sarafu za dhahabu?

Kwanini Tanzania hatuchapishi sarafu za dhahabu?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Nchi nyingi, hasa zile zinazozalisha dhahabu huwa zinachapisha sarafu za dhahabu na kuuza. Sarafu hizi zina mambo mengi. Kwanza watu hununua kama kito kutokana na uzuri wake.

Pili watu hununua kama ni pesa na wanaweza kuitumia kama pesa. Tatu nchi hufanya export ya kitu kilichoongezwa thamani na kujipatia pesa.

Nne zinatumika kutangaza mambo ya nchi, hasa utalii. Tano na muhimu zaidi, watu hununua ili kulinda utajiri wao dhidi ya mfumuko wa bei.

Nchi nyingi hutengeneza sarafu hizi zikiwa na uzito wa ounce(oz) moja ambayo ni sawa na 31g. Ikiwa ni 99.99 pure gold. Bei ya oz moja ya dhahabu kama hiyo kwa sasa ni dola 1,900. Wanatengeneza pia sarafu zenye uzito wa chini.

Nchi kama Rwanda wanatengeneza sarafu zao za dhahabu toka 2018. Na wakongwe wa hizo kazi ni SA, USA, Australia, Canada na Austria. Hizi sarafu zinafaida nyingi kama tulivyoona, na nchi yetu ina dhahabu ya kutosha. Na sasa tunazo refineries. Kwa nini hatutengenezi hizi coins, labda serengeti, ngorongoro, kilimanjaro etc, na kuwauzia raia na wageni pia?

ibrua02305_1.jpg
ibrua02305_2.jpg
ibrua02205_1.jpg
2022-1-oz.-GML_REV.png
kr10_2020_a.png
800px-1_oz_Vienna_Philharmonic_2017_averse.png
1-american-eagle-front_800-600x600.jpg
1-american-eagle-front_800-600x600.jpg
 
Nchi nyingi, hasa zile zinazozalisha dhahabu huwa zinachapisha sarafu za dhahabu na kuuza. Sarafu hizi zina mambo mengi. Kwanza watu hununua kama kito kutokana na uzuri wake.

Pili watu hununua kama ni pesa na wanaweza kuitumia kama pesa. Tatu nchi hufanya export ya kitu kilichoongezwa thamani na kujipatia pesa.

Nne zinatumika kutangaza mambo ya nchi, hasa utalii. Tano na muhimu zaidi, watu hununua ili kulinda utajiri wao dhidi ya mfumuko wa bei.

Nchi nyingi hutengeneza sarafu hizi zikiwa na uzito wa ounce(oz) moja ambayo ni sawa na 31g. Ikiwa ni 99.99 pure gold. Bei ya oz moja ya dhahabu kama hiyo kwa sasa ni dola 1,900. Wanatengeneza pia sarafu zenye uzito wa chini.

Nchi kama Rwanda wanatengeneza sarafu zao za dhahabu toka 2018. Na wakongwe wa hizo kazi ni SA, USA, Australia, Canada na Austria. Hizi sarafu zinafaida nyingi kama tulivyoona, na nchi yetu ina dhahabu ya kutosha. Na sasa tunazo refineries. Kwa nini hatutengenezi hizi coins, labda serengeti, ngorongoro, kilimanjaro etc, na kuwauzia raia na wageni pia?

View attachment 2551814View attachment 2551815View attachment 2551816View attachment 2551817View attachment 2551818View attachment 2551819View attachment 2551820View attachment 2551820
Mbona hiyo ya America ni kama mamba anataka kulimeza bara la Africa
 
Coin moja thamani USD 1,900 nzuri sana na rahisi kuhifadhi.
Zipo hata za 10g ambazo zitakuja kama dola mia sita na kitu. Lakini hizi huwa wanaongeza bei kidogo, haziwi sawa na Dhahabu halisi ambayo haijachapwa.
 
Nafikiri unaweza kutengeneza ukihitaji,twende na vipaumbele vya msingi ndugu
 
Nadhani huku ndo dunia itakapo eleke hawa wa makaratasi si muda watakosa wateja
 
Muda si mrefu dhahabu itapanda sana maana mrusi na mchina wanataka kuachana na USD ambayo kimsingi haina kitu nyuma yake zaidi tu ni sababu ni ya Marekani. Ikiwa Saudia ataacha kuuza mafuta kwa USD na nchi nyingi zikaanza kufanya biashara kwa Chines Yuan na sarafu zao basi dola itashuka na mbadala wake ni gold itarud kwenye hatamu.

Zimbabwe wameanza kutumia hizo gold coin kupunguza mfumuko lakini kiranja wa dunia kupitia IMF wamemuonya aache kufanya hivyo.
 
Back
Top Bottom