Kwanini Tanzania isizishitaki Ujerumani na Uingereza?

Kiparuanda

JF-Expert Member
Joined
Jul 23, 2013
Posts
1,587
Reaction score
2,389
Sina uelewa wa sheria za kimataifa lakini utashi wangu unanipa kwamba vitendo tulivyofanyiwa na nchi hizi mbili wakati wa ukoloni sio haki kabisa.

Wamejitajirisha kwa mali zetu na nguvu za watu wetu, wametutawala kikatili miaka kibao na kutupiganisha vita vyao huko kisha wanatuandikia ktk vitabu vya history kutufundisha waluyotufanyia.

Kwa nn Tanzania tusiwashitaki huko kwenye mahakama zao watulipe fidia na vitu vyetu warudishe?

Naamini hizo sheria wanazotungaga wenyewe lazima kuna nyingine zinafaa kuwageuka hawawezi kutufanyia hivyo kwanza hadi sasa hivi nahisi wanatutawala tu.

Please wanaojua sheria wanipe mwongozo.
 
sasa tukiwashitaki kwenye mahakama zao si tutashindwa kesi
 
Nyie bwana hamaishi maneno, jana nilikuwa nasikiliza wimbo mmoja eti "..TANU ilipoanza mwingereza kafunga vilago". Eti kuna watu wanaamini kuwa wakoloni walifukuzwa na TANU wakati wenyewe ndio walikuja hapa na baada ya miaka kama 30 wakampata kijana wakampeleka kumsomesha huko huko kwao na kumfundisha walichotaka wao ili baadae wamkabidhi nchi!
Wakoloni walikuja kipindi kimoja Afrika nzima na waliondoka almost miaka inatofanana, 1960s, hii haikutokea kwa bahati mbaya bali inawezekekana walikuwa na mpango wa labda miaka 300. Sasa jiulize mpaka leo bado mingapi imebaki wakati mkuu Trump anasema tunapaswa kuongezewa mingine 100!

Haya leo wameshaondoka, nenda Geita ukachimbe hiyo dhahabu tuone kama utaweza. Na hata ukiamua kuwekeza hazina yako yote kununua hizo mashine bado wenyewe ndio wanunuzi wa hiyo dhahabu, wakikataa kuinunua hata ukiwa na tani mia unakufa nazo na njaa! Hapo ndipo huwa tunasema life is not fair!
 

Waingereza walichukua nini kutoka Tanzania?
 
anza kuwashitaki kidogokidogo
 
Ni Nchi gani duniani umeshasikia wamefungua kesi ya namna hyo kwani karibu robo tatu ya dunia zilikuwa ni koloni za nchi kama 7 za ulaya zikiongozwa na Uingereza
 
Gold, silver, ivory, watumwa, maskeleton ya mijusi, vifaru n.k, warudishe vile vinavyofaa kurudisha
Si kweli kuwa Mwingereza alijihusisha na hizo Biashara, Skeleton la Mjusi liko moja tu na lipo German
 
Kama mpaka leo karibu miaka 60 ya uhuru bado tunalia lia sasa uhuru tukiulilia wa nini ?! Hatukustahili kuupata kwa sababu hatuna akili ya kupambana na changamoto. UKWELI MCHUNGU
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…