Kwanini Tanzania tunakataza watu kulima Bangi? Au tunasubiri mabeberu watuelekeze?

Kwanini Tanzania tunakataza watu kulima Bangi? Au tunasubiri mabeberu watuelekeze?

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2019
Posts
762
Reaction score
6,984
Kilimo Cha Bangi kinatumika nchi Mbalimbali na jinsi siku zinavyokwenda ndivyo Mataifa mengi zaidi yanaruhusu kulima n kuvuta Bangi. Tanzania sisi msimamo wetu ni kuwafunga wavutaji na wauzaji miaka 30, kuchoma moto mashamba nakutumia mabiliaoni kupambana na raia wanaolima wakauze kwenye soko la Dunia.

Naomba anayejua Kwanini sisi tunadhani Bangi siyo zao la biashara? Je, kesho Dunia ikipitisha Bangi kuwa zao la biashara tutaendelea na msimamo wetu? Ni yapi madhara ya watu wetu kulima Bangi?

Mapombe makali tunaruhusu watu wetu wanywe, sigara hata zisizo na vichingi tunaruhusu ziingie nchini kisa wamezalisha wazungu, lakini gongo na pombe nyingine za kienyeji tunapiga marufuku badala yakuzitengenezea ubora na vifungashio, tumelogwa?

Hivi ni wapi wavuta Bangi wameonekana kuwa na madhara kuliko walevi wa pombe Kali za viwandani ikiwemo viroba?

Tunasubiri Bangi izalishwe Kwa wingi na kuingizwa kwenye viwanda vya madawa kutengeneza tiba ndipo tuanze kulima? Tunasubiri watupangie Bei? Uganda wanalima bangi na kuuza Ulaya na ni ndugu zetu wa karibu, je wao wamekuwa vichaa kuliko sisi? Kwanini tunaishi hapa Duniani kukomoana na kukaririshana maisha?
 
Ni ufala hii nchi!! Miaka ya 1997 bangi ilikua inalimwa tz kama zao la chakula!! Na hapo raia walikua hasa vijijin hawajajua kama kuna watu huko mujini wako wanavuta[emoji23][emoji23]

Nchi masikini kama hii muzungu akiwambia kunya n kuchafua mazingira n serikali itaziba watu iyo naniii!!

Tuko kwene nchi ambazo hazina self determination no values !! Zinasubir order za kupokea abroad!
 
Atakuja kijana mdogo tu mwenye diploma kutoka ubeberuni na atawa convince watawala wetu wenye master's na umri umesogea kwamba mbangi Ni dili kesho yake utawasikia wakisifu kilimo Cha bhangi na mirungi.
 
Atakuja kijana mdogo tu mwenye diploma kutoka ubeberuni na atawa convince watawala wetu wenye master's na umri umesogea kwamba mbangi Ni dili kesho yake utawasikia wakisifu kilimo Cha bhangi na mirungi.
😁😁😁😁
 
Inaweza kulimwa na makampuni private kwa usimamizi mkali kama ambavyo TRA wanasimamia bonded warehouse
 
Back
Top Bottom