Wakuu poleni na majukumu ya kujitafutia kipato,mimi swali langu ni kwa wahusika wa TRC (SGR)hivi ni kwa nini mtu akitaka kukata tiketi kwa ajili ya train ya sgr mnamtaka lazima awe na kitambulisho tena cha Nida naomba kufahamishwa,na je ingetokea nini kama tungekuwa tunakatiwa ticket bila hiyo nida na kwa watu ambao hawana hicho kitambulisho cha nida mmeweka utaratibu gani usiokuwa na usumbufu wa mtu kupata ticket na kusafiri: naomba muelewe kwamba utaratibu mliouweka wa vitambulisho unawakosesha sana abiria