Kwanini Tumpongeze huyu Professor wa chuo!!!

Kwanini Tumpongeze huyu Professor wa chuo!!!

DASA

JF-Expert Member
Joined
Jan 6, 2011
Posts
1,031
Reaction score
302
Waziri wa afya na ustawi wa jamii Dr. Hussein A. Mwinyi alimteua Prof. Samwel Victor Manyele wa UDSM, kuwa mkemia mkuu wa serikali kuanzia tarehe 21/1/2013. nafasi hiyo ilikuwa wazi baada ya aliyekuwa mkemia mkuu wa serikali marehemu Dr. Ernest Mashimba kufariki tarehe 19 septemba, 2010.

Kutokana na uteuzi huo Professor wetu mpendwa amekuwa akipongezwa sana. Sina wivu na hizo pongezi. Najaribu tu kufikiria kwanini anapongezwa. Je ni kwamba huko kuna masilahi makubwa zaidi??, nafasi aliyoteuliwa ina heshima zaidi kuliko aliyokuwa nayo awali??.

Je Serikali nayo ipongezwe kwa kumteua??. Ni wapi huyu Proffesor alikuwa anahitajika zaidi??. Au kazi aliyokuwa anafanya haikuwa na umuhimu zaidi kuliko hiyo aliyoteuliwa.

Je......?, Je........? ..................

Good day .
 
Nampa pole huyu Prof maana si kazi ya kataalam kwa mda huu wa ccm
 
Sidhani kweli kama anahitaji hizo pongezi. Nahisi kuna tatizo mahali. Labda ni kwasababu ya masilahi.
 
Anapongezwa kwa sababu ingawa ni wengi wangestahili nafasi hiyo,yeye amebahatika kuonekana kufaa zaidi!Ni heshima kuliko hapo alipokuwa mwanzo.Hata mie nimemfahamu tu baada ya kuteuliwa kwa nafasi hiyo,bila shaka na wengine wengi, hivyo yeye ni mtu maarufu kwa sasa.Anastahili pongezi!
 
Mimi sidhani kama mkemia mkuu inahitaji professor, c wangetangaza??haya mambo ndo hatuyataki tena??ona wenzetu kenya wanavyopata wakuu wa idara/mashirika ya serikali..wanatangaza then wanawafanyia interview...Hizi kazi za kupeana hovyo kabisa, amkeni watanzania wenzangu
 
Waziri wa afya na ustawi wa jamii Dr. Hussein A. Mwinyi alimteua Prof. Samwel Victor Manyele wa UDSM, kuwa mkemia mkuu wa serikali kuanzia tarehe 21/1/2013. nafasi hiyo ilikuwa wazi baada ya aliyekuwa mkemia mkuu wa serikali marehemu Dr. Ernest Mashimba kufariki tarehe 19 septemba, 2010.

Kutokana na uteuzi huo Professor wetu mpendwa amekuwa akipongezwa sana. Sina wivu na hizo pongezi. Najaribu tu kufikiria kwanini anapongezwa. Je ni kwamba huko kuna masilahi makubwa zaidi??, nafasi aliyoteuliwa ina heshima zaidi kuliko aliyokuwa nayo awali??.

Je Serikali nayo ipongezwe kwa kumteua??. Ni wapi huyu Proffesor alikuwa anahitajika zaidi??. Au kazi aliyokuwa anafanya haikuwa na umuhimu zaidi kuliko hiyo aliyoteuliwa.

Je......?, Je........? ..................

Good day .

Naona kama upo sawa, maana sasa ifikie kipindi tuondoe hizi pongezi maana zinasababisha watu wafanye kazi kwa mazoea kwa kuwa wanaona watapata maslahi zaidi, ifikie kipindi tuwape pole maana kazi wanazoenda kufanya ni nyeti na akiboronga rungu linamshukia, ikifikia hali hiyo uchapakazi utarejea na watu watahofu hata kufanya ufisadi, inakera mkuu unakuta mtu amepewa dhamana na serikali kufanya kazi fulani akiboronga utasikia amepewa adhabu ya kuhamishiwa Tandahimba, au kijiji fulani, na hii inaashiria kuwa serikali ina ubaguzi wa kubagua baadhi ya maeneo Tanzania, something which is very bad.
 
Back
Top Bottom