Kwanini tunaendelea kujivuta kuhusu chanjo za Corona? Tunahitaji tubembelezwe kuhusu kuyathamini maisha yetu wenyewe?

Toa ndoto za alinacha hapa!
Wanakufa kwa sbb chanjo hazina uwezo wa kukinga badala yake zenyewe ndio zinaongeza madhara! After all, they are experimental 'vaccine'! More over, they are not vaccines at all...but human genetic engineering 😭😑! Mfyuuuuuu 😑!
 
I
Hii habari unapata wapi? Haina ukweli hata kidogo. Ni watu gani wanaorudia uvumi bila msingi?
Wimbi la tatu linaanza sasa kuumia Afrika (ambako chanjo ziko hache mno) na kushambulia pia vijana
India si ndiko chanjo wanatengeneza! Hili wimbi la 3 linatoka wapi kama sio India😑! Sasa kwa nini ndio vifo vingi viripotiwe wakati chanjo walichanjwa😑!?
We kama unataka saaana hilo wimbi likuelekee na ww, πŸ˜‚...ww agiza kwa DHL dozi yako ya chanjo ujichanje mwenyewe na familia yako, au cross border uingie uganda ukachanjwe kama nguruwe tunavyowalazimishaga kuchanjwa.. hapo ndio utakapolielewa wimbi hilo la 3 linaspeed na kimo gani😜!
 
Jamani! Ni vigumu kuelewa kwamba si kitu kama chanjo kipo nchini lakini hakipo ndani za mwili wa mtu? Uhindi walimaliza chanjo chini ya asilimia kumi ya watu wao walipopigwa na wimbi la maambukizi. Waliopata chanjo tayari na kukamilika dozi mbili hawana tatitizo, waliokufa ni kutoka hao wengine ambayo ni milioni mamia bado.
Ni kweli wanatengeneza chanjo, na baada wimbi kuenea walisimamisha mauzo yote nje ya nchi. Hii hatari kwa nchi nyingine, hasa Afrika kwa sababu sasa kuna tatizo kupata chanjo sokoni.

Kaka wewe bila shaka umepata chanjo kadha, maana hii ni kawaida hapa nchini, hasa dhidi ya magonjwa 5 yanayoua watoto. Sijui umri wako, lakini wazee wanakuambia vifo vya watoto vimepungua sana tukilinganisha na zamani. Kwa nini???? Shauri ya chanjo hizo.
Sasa unaleta lugha ya ajabu kuhusu chanjo.
 
Ok sawa.
 
Kaka usitumie maneno ambayo hujui maana yake. Chanjo zina uwezo wa kukinga kabisa. Tunaona matokeo katika nchi zote walipofaulu kufikia asilimia kubwa ya watu. Angalia takwimu ya Marekani:

(chanzo: US COVID-19 cases and deaths by state)
Kwenye takwimu unaona vifo vilipanda mwaka jana hadi Aprili walipoweka utaratibu wa kukaa mbali na watu, kubana idadi ya watu wanaoruhusiwa kukutana, kufunga vilabu, sinema, kwa muda pia shule na vyuo, lockdown... Vifo vimeshuka. Masharti yamelegezwa mahali pengi, vifo vimeanza kupanda tena tangu Novemba, mwaka huu vinashuka tangu kuanzishwa kwa chanjo na kufikia zaidi ya nusu ya wakazi wote.
Kwa nini nchi karibu zote zinashindana kupata chanjo, ila hapa Tanzania ujinga unaota majani mapya?

(nyongeza ndogo tu: idadi ya vifo Marekani ni juu kidogo katika maeneo ambako wengi sana walimpigia kura bwana Trump, kwa sababu walimwamini aliposema "Covid si shida!" - katika majimbo hayo hadi leo asilimia kubwa kidogo inasita kupokea chanjo...)
 
Wanasema huu ugonjwa ni wakuja na kuondoka.
 
Unauliza maswali mazuri. Nchi za Afrika idadi ya vifo vinavyotangzwa inategemea vipimo. Pasipo na vipimo (au kama vipimo vinafichwa kwa makusudi) utaona idadi rasmi ya vifo vya Covid ni ndogo kama hapa Tanzania, rasmi wametangaza vifo ni 21 tu tangu mwaka jana. Uganda inaonekana wanapima zaidi, hivyo wanataja idadi kubwa zaidi (hakika si wote).
Ukipenda kujifariji kwa namba bandia, sawa azimio lako.
Hata Uganda namba ya vifo ni ndogo, kama karibu kote Afrika. Kwa nini?
a) Afrika wananchi wengi ni watoto na vijana . Waliokufa hadi sasa duniani ni hasa wazee (Marekani: asilimia 60 za vifo ni watu juu ya 75; ukiangalia watu juu ya 65 umefika tayari kwa asilimia 80 ya vifo). Naongeza takwimu chini.
b) Waafrika wengi bado wanaishi vijijini hawasafiri sana. Nchi nyingine zilipaswa kuweka sheria ya social distancing. kama watu wankaa kwa miezi mfululizo kijijini bila kutoka, matokeo ni yaleyale bila sheria.

Ona takwimu vifo vya Covid Marekani na umri wa marehemu:

COVID-19 Deaths by Age (namba za Februari 2021)
 
Hivi unaamini upuuzi hui unaochapishwa kuhadaa ulimwengu!? Huoni siasa na biashara ndani yake ktk machapisho hayo!?
Data zenyewe ni hewa kama majeneza hewa ya covid-19 victims uganda!
πŸ‘‡





 

Attachments

  • VID-20210611-WA0004.mp4
    5.6 MB
Unataka kuonyesha nini kwa picha ya takwimu ya Uingereza?
Naona kuna wanasiasa kadhaa wanaojitahidi kuficha ukweli kuhusu ugonjwa huu kwa sababu wanataka kuonyesha mafanikio tu. Trump alikuwa vile, nimeambiwa nchi ya Afrika ya Mashariki alikuwepo mmoja pia (kweli?), yule Bwana wa Uturuki, Korea Kaskazini, Tajikistan. Turkmenistan serikali iliagiza kuchoma manyasi kama dawa la kienyeji, Belorussia rais Lukachenko alishauri kunywa Vodka na kuoga ....
Kwa jumla naona akina "mabepari" wanashindana kati yao kupata chanjo, hata wakipaswa kuvunja mapatano ya kugawana.

Ninachoona mimi ni nchi tajiri zilihakikisha wanapata chanjo wenyewe, nchi maskini wamepata kidogo sana au kunyimwa.
Kwa hiyo - nani anahadaa ulimwengu , tena kwa kusudi gani?
(Utatueleza pia eti Covid na chanjo ni jaribio la mabepari kuangamiza Afrika ?)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…