Da Vinci XV
JF-Expert Member
- Dec 7, 2019
- 3,862
- 6,438
Na Da Vinci XV
Nyakati fulani wakati nadurusu maandiko matakatifu nilipata kukutana na andiko moja lililandikwa na watu miongoni mwa watu mashuhuri sana walioishi nyakati zile kabla ya Masiku tele.
Andiko lilipata kusema " KWA MAANA JINSI HII MUNGU ALIUPENDA ULIMWENGU, HATA AKAMTOA MWANAWE WA PEKEE......"
Kifungu hiki kikahitimisha dhana yangu ya kwamba Mungu huyu anaupenda sana Ulimwengu, na kuubariki vitu mbalimbali na watu mbalimbali.
kuja kuiishii hii dunia yake.
Bwana Mungu huyu amekuwa na desturi ya kuubariki na kutoa watu ambao mara nyingi wamekua wakombozi kwenye Dunia yake hii aliyoitengeneza mwenyewe.
Ameshaibariki dunia Kiumbe aitwaye dhul qarnain aliyeujenga Ukuta mkubwa wa china (Great Wall) karne 4 kabla ya kuzaliwa Bwana Yesu.(BC)
Akaibariki dunia kwa kuipatia mchoraji nguli sana miaka ya 1448, muitaliano Domenico Ghirlandaio, ambae aliisanifu dunia hii kwa michoro adhimu sana ya mkono wake
Lakini akaibariki dunia kwa kuipatia mwanafizikia na mwanahisabati nguli sana kutoka kule India , Bwana Satyendra Nath bose miaka ya 1894.
Na imekuwa ni desturi na tamaduni ya huyu Mungu kuupendelea ulimwengu kwa kuleta wanadamu wenye talanta na silka tofauti ambazo nyingi nadra kwa viumbe wengine kuwa navyo
Ilipofika 1960 , Huyu Bwana Mungu akaibariki tena dunia kwa kumleta Mwandishi nguli sana wa Filamu , Nyimbo pamoja na vitabu aitwaye Neil Gaiman.
Muingereza huyu, ni mtalamu sana wa maandishi kama ilivyo kwa waingereza wengi , vitabu vyake vingi vya kufikirika hukusogeza katika dimbwi la ukweli fikrani.
kazi yake moja iliyonishawishi kumhusudu mwamba huyu ni kitabu chake cha mwaka 2001 kiitwacho American Gods.
Miongoni mwa nukuu nyingi za nguli huyu gaiman kuna nukuu ya pendwa sana inasema
"You know what the really scary thing about bad dreams? It's that something's going on in your head, and you can't control it. I mean, It's like there's these bad worlds inside you. But it's just you... it's like you're betraying yourself"
Neil Gaiman
Kwa tafsiri isiyo Rasmi Nguli Gaiman anahoji
"Unajua jambo gani la kuogofya kuhusu ndoto mbaya???..Ni kwamba kuna jambo linaendelea kichwani mwako na uwezi kulidhibiti.
Ninamaanisha ni kama kuna Ulimwengu (tofauti) mbaya ndani yako, Lakini ni wewe mwenyewe tu.. ni kama unajisaliti vile"
Na nukuu ya mwamba huyu imenipa ari ya kuandika hii mada lakini kwa mlengo wa tofauti kidogo.
Kama tunavyoujua nature yetu imeundwa katika mfumo ambao usiku ndio muda wa kupumzika ni mfumo wa maisha, maendeleo ya sayansi na teknolojia pamoja na mabadiliko ya Tabia ya Nchi ndivyo vimefanya wanadamu tubadilike katika mfumo mzima wa maisha hivyo kutulazimu kutafuta rizki hadi usiku wakati mwingine amabao ndio muda tunatakiwa kupimzika hivyo kulazimisha ciycle na mfumo mzima wa maisha kubadilika.
Scientifically, wanasema Kulala nyakati za mchana wakati mwingine kunaweza kusababisha ndoto mbaya kwa sababu mzunguko wako wa kulala unaweza kubadilishwa katika mfumo wake wa kawaida, na kukufanya uingie katika usingizi mzito katika hatua ya Rapid Eye Movement (REM) hatua ambayo ndoto nyingi hutokea, ukiwa usingizini.
Na jambo hili lina uwezekano wa kusababisha ndoto mbaya zaidi, hasa ukiwa tayari na mchoko wa shughuli za siku.
Tafsiri yake ni kwamba usingizi wa mchana unaweza kuwa mfupi na usio na muundo na mfumo kama tulalavyo usiku ,na hivyo kusababisha usingizi wa mafungu zaidi na kuongeza uwezekano wa kupata njozi mbaya.
MAMBO MENGINE YANAYOSABABISHA NDOTO MBAYA WAKATI WA MCHANA
•Usumbufu wa mzunguko wa usingizi.
Unapolala wakati wa mchana, mzunguko wako wa kulala unaweza kuwa mfupi, na kusababisha uingie katika hatua REM haraka kuliko kawaida kwa kuwa unapata usingizi mzito ndani ya muda mfupi, ambapo hatua hii inaweza kusababisha ndoto za wazi zaidi na wakati mwingi huwa ni mbaya kutokana na mfumo mbovu wa mzunguko wa usingizi hivyo kuupa ubongo shughuli ya ziada.
•Mkazo au uchovu
Ikiwa tayari unahisi uchovu au mkazo kutokana shughuli za siku hiyo, matokeo ya hisia hizi yanaweza kujidhihirisha katika ndoto zako wakati wa unajipumzusha wakati wa mchana.
•Kwenda kinyume na Ratiba ya kawaida ya kulala
Kulala mara kwa mara wakati wa mchana, haswa ikiwa haijaratibiwa mara kwa mara, kunaweza kuharibu muundo wako wa usingizi kwa ujumla, na kuchangia shughuli nyingi za ubongo kinyume na shughuli zake za kawaida hivyo basi kupelekea maono mabovu
•Kutopata usingizi wa kutosha wakati wa Usiku.
Kama hautopata usingizi wa kutosha wakati wa usiku , kutokana na shughuli mbalimbali kama kazi , mawazo na mengineyo, mwili wako utahitaji kufidia kiwango cha usingizi ambacho kilikosekana wakati wa usiku na kupelekea kuingia katika hatua ya REM kwa haraka sana endapo utalala wakati wa mchana na kusababisha ndoto mbaya
MAMBO MACHACHE UNAYOWEZA KUFANYA KUEPUKANA NA HILI
•Muda wa kulala usingizi
Jaribu kulala mapema siku ambayo mzunguko wako wa kulala ni wa kawaida zaidi, ili kupata mda wa kutosha wa kulala na kutengeneza mzuko sahihi wa usingizi wako.
•Mazingira tulivu
Unda mazingira na muda tulivu kwa ajili ya usingizi wako ili kuboresha usingizi na uwe usingizi mtulivu.
•Chunguza (Observe) Aina ya Ndoto zako usingizini.
Ikiwa una changamoto ya ndoto mbaya unapolala iwe mchana au usiku, jaribu kubaini mzunguko wako wa usingizi na muda unaopata usingizi ikiwa vyote viko sawa na bado una changamoto ya njozi mbaya basi onana na wataalamu juu ya hili.
What is the cause of bad dreams spiritually?????
NB: Nyakati hizi ni za kutafuta sana dunia haitaki watu lelemama, usiofanya kazi kwa mahangaiko hutokula wala kutunza familia , hivyo kupelekea watu kukosa mda mwingi sana kwa ajili ya kupumzisha bongo zao na miili yao kwa ajili ya faida ya baadae.
QUR'AN 78:9
NA TUKAFANYA KULALA KWENU NI MAPUMZIKO
Nyakati fulani wakati nadurusu maandiko matakatifu nilipata kukutana na andiko moja lililandikwa na watu miongoni mwa watu mashuhuri sana walioishi nyakati zile kabla ya Masiku tele.
Andiko lilipata kusema " KWA MAANA JINSI HII MUNGU ALIUPENDA ULIMWENGU, HATA AKAMTOA MWANAWE WA PEKEE......"
Kifungu hiki kikahitimisha dhana yangu ya kwamba Mungu huyu anaupenda sana Ulimwengu, na kuubariki vitu mbalimbali na watu mbalimbali.
kuja kuiishii hii dunia yake.
Bwana Mungu huyu amekuwa na desturi ya kuubariki na kutoa watu ambao mara nyingi wamekua wakombozi kwenye Dunia yake hii aliyoitengeneza mwenyewe.
Ameshaibariki dunia Kiumbe aitwaye dhul qarnain aliyeujenga Ukuta mkubwa wa china (Great Wall) karne 4 kabla ya kuzaliwa Bwana Yesu.(BC)
Akaibariki dunia kwa kuipatia mchoraji nguli sana miaka ya 1448, muitaliano Domenico Ghirlandaio, ambae aliisanifu dunia hii kwa michoro adhimu sana ya mkono wake
Lakini akaibariki dunia kwa kuipatia mwanafizikia na mwanahisabati nguli sana kutoka kule India , Bwana Satyendra Nath bose miaka ya 1894.
Na imekuwa ni desturi na tamaduni ya huyu Mungu kuupendelea ulimwengu kwa kuleta wanadamu wenye talanta na silka tofauti ambazo nyingi nadra kwa viumbe wengine kuwa navyo
Ilipofika 1960 , Huyu Bwana Mungu akaibariki tena dunia kwa kumleta Mwandishi nguli sana wa Filamu , Nyimbo pamoja na vitabu aitwaye Neil Gaiman.
Muingereza huyu, ni mtalamu sana wa maandishi kama ilivyo kwa waingereza wengi , vitabu vyake vingi vya kufikirika hukusogeza katika dimbwi la ukweli fikrani.
kazi yake moja iliyonishawishi kumhusudu mwamba huyu ni kitabu chake cha mwaka 2001 kiitwacho American Gods.
Miongoni mwa nukuu nyingi za nguli huyu gaiman kuna nukuu ya pendwa sana inasema
"You know what the really scary thing about bad dreams? It's that something's going on in your head, and you can't control it. I mean, It's like there's these bad worlds inside you. But it's just you... it's like you're betraying yourself"
Neil Gaiman
Kwa tafsiri isiyo Rasmi Nguli Gaiman anahoji
"Unajua jambo gani la kuogofya kuhusu ndoto mbaya???..Ni kwamba kuna jambo linaendelea kichwani mwako na uwezi kulidhibiti.
Ninamaanisha ni kama kuna Ulimwengu (tofauti) mbaya ndani yako, Lakini ni wewe mwenyewe tu.. ni kama unajisaliti vile"
Na nukuu ya mwamba huyu imenipa ari ya kuandika hii mada lakini kwa mlengo wa tofauti kidogo.
Kama tunavyoujua nature yetu imeundwa katika mfumo ambao usiku ndio muda wa kupumzika ni mfumo wa maisha, maendeleo ya sayansi na teknolojia pamoja na mabadiliko ya Tabia ya Nchi ndivyo vimefanya wanadamu tubadilike katika mfumo mzima wa maisha hivyo kutulazimu kutafuta rizki hadi usiku wakati mwingine amabao ndio muda tunatakiwa kupimzika hivyo kulazimisha ciycle na mfumo mzima wa maisha kubadilika.
Scientifically, wanasema Kulala nyakati za mchana wakati mwingine kunaweza kusababisha ndoto mbaya kwa sababu mzunguko wako wa kulala unaweza kubadilishwa katika mfumo wake wa kawaida, na kukufanya uingie katika usingizi mzito katika hatua ya Rapid Eye Movement (REM) hatua ambayo ndoto nyingi hutokea, ukiwa usingizini.
Na jambo hili lina uwezekano wa kusababisha ndoto mbaya zaidi, hasa ukiwa tayari na mchoko wa shughuli za siku.
Tafsiri yake ni kwamba usingizi wa mchana unaweza kuwa mfupi na usio na muundo na mfumo kama tulalavyo usiku ,na hivyo kusababisha usingizi wa mafungu zaidi na kuongeza uwezekano wa kupata njozi mbaya.
MAMBO MENGINE YANAYOSABABISHA NDOTO MBAYA WAKATI WA MCHANA
•Usumbufu wa mzunguko wa usingizi.
Unapolala wakati wa mchana, mzunguko wako wa kulala unaweza kuwa mfupi, na kusababisha uingie katika hatua REM haraka kuliko kawaida kwa kuwa unapata usingizi mzito ndani ya muda mfupi, ambapo hatua hii inaweza kusababisha ndoto za wazi zaidi na wakati mwingi huwa ni mbaya kutokana na mfumo mbovu wa mzunguko wa usingizi hivyo kuupa ubongo shughuli ya ziada.
•Mkazo au uchovu
Ikiwa tayari unahisi uchovu au mkazo kutokana shughuli za siku hiyo, matokeo ya hisia hizi yanaweza kujidhihirisha katika ndoto zako wakati wa unajipumzusha wakati wa mchana.
•Kwenda kinyume na Ratiba ya kawaida ya kulala
Kulala mara kwa mara wakati wa mchana, haswa ikiwa haijaratibiwa mara kwa mara, kunaweza kuharibu muundo wako wa usingizi kwa ujumla, na kuchangia shughuli nyingi za ubongo kinyume na shughuli zake za kawaida hivyo basi kupelekea maono mabovu
•Kutopata usingizi wa kutosha wakati wa Usiku.
Kama hautopata usingizi wa kutosha wakati wa usiku , kutokana na shughuli mbalimbali kama kazi , mawazo na mengineyo, mwili wako utahitaji kufidia kiwango cha usingizi ambacho kilikosekana wakati wa usiku na kupelekea kuingia katika hatua ya REM kwa haraka sana endapo utalala wakati wa mchana na kusababisha ndoto mbaya
MAMBO MACHACHE UNAYOWEZA KUFANYA KUEPUKANA NA HILI
•Muda wa kulala usingizi
Jaribu kulala mapema siku ambayo mzunguko wako wa kulala ni wa kawaida zaidi, ili kupata mda wa kutosha wa kulala na kutengeneza mzuko sahihi wa usingizi wako.
•Mazingira tulivu
Unda mazingira na muda tulivu kwa ajili ya usingizi wako ili kuboresha usingizi na uwe usingizi mtulivu.
•Chunguza (Observe) Aina ya Ndoto zako usingizini.
Ikiwa una changamoto ya ndoto mbaya unapolala iwe mchana au usiku, jaribu kubaini mzunguko wako wa usingizi na muda unaopata usingizi ikiwa vyote viko sawa na bado una changamoto ya njozi mbaya basi onana na wataalamu juu ya hili.
What is the cause of bad dreams spiritually?????
NB: Nyakati hizi ni za kutafuta sana dunia haitaki watu lelemama, usiofanya kazi kwa mahangaiko hutokula wala kutunza familia , hivyo kupelekea watu kukosa mda mwingi sana kwa ajili ya kupumzisha bongo zao na miili yao kwa ajili ya faida ya baadae.
QUR'AN 78:9
NA TUKAFANYA KULALA KWENU NI MAPUMZIKO