Kwanini tusiamini kuwa kufa kupo?

Kwanini tusiamini kuwa kufa kupo?

Miwatamu

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2012
Posts
1,450
Reaction score
489
Nimeamua kuamka na swali hili baada ya ile habari ya wana ndugu wa marehemu aliyefariki tangu Ijumaa ya wiki hii kukataa kuamini kuwa amekufa na kuamua kumpeleka katika Kanisa la Ufufuo na Maombezi ili arudi kuwa hai. Je, pamoja na sisi kushinda na kukesha makanisani na misikitini bado tu hatuamini kuwa kuna kuzaliwa na kufa?
 
Samahani mkuu, hii nayo ni siasa?..[/QUOTE]

Hippo; Siasa ni imani na imani inatokana na kuamini yale yatarajiwayo ambayo tunayapata katika vitabu vitakatifu. Waumini wa IMANI ya DINI ndio waumini wa SIASA. Karibu twende kwenye uchaguzi.
 
Hao wanapingana na agizo la Bwana wa Majeshi. Angalikuwa hai wangalifunga na kuomba Mungu angalikubali angaliahirisha kwa muda tu lakini kufa ni hakika.
 
Kwanza kama wanampeleka akaombewe ili awe hai, maana yake wanakubali kwamba amekwisha kufa, vinginevyo hayo maombezi ni usumbufu kwa wachungaji, waombolezaji na Mungu mwenyewe. Haya basi, kufa si swala la kuamini ni swala la ufahamu. Tanaamini yale ambayo hatuna uhakika wa kisayansi nayo, lakini kufa tunaweza kuhakikisha. Kwa nini tujisumbue kuamini? Ngoja ufe, halafu uendelee kuwa na mashaka kama umekufa au bado!!
 
Samahani mkuu, hii nayo ni siasa?..[/QUOTE]

Hippo; Siasa ni imani na imani inatokana na kuamini yale yatarajiwayo ambayo tunayapata katika vitabu vitakatifu. Waumini wa IMANI ya DINI ndio waumini wa SIASA. Karibu twende kwenye uchaguzi.

Mkuu Miwatamu, niliuliza kwani swali limekaa kama hoja!

Anyway nadhani kuna jambo fulani( Ujinga-kutokuwa na ufahamu au uelewa wa jambo fulani).

Kwa kawaida katika Kuomboleza(Mourning) kuna kupitia hatua tano..

Denial, Anger, Bargaining, Depression, Acceptance.

1.Denial(Kutokubali)
Ambayo huwa kama temporary defense kuwa, hii haiwezi kutokea(Wakati mwingine hata kama watu walitarajia kifo hicho)


2. Anger(Hasira):
Hasira huja hasa, mtu/watu wakijiuliza kwanini mimi/sisi?,
kwamba hakuna usawa katiak hili(it's not fair)..mtu/watu huwa na hasira dhidi ya wengine au wao wenyewe!

3. Bargaining(Kuomba):
Mtu huwa radhi kufanya chochote, ..mawazo na mtazamo wa nitauza hata nyumba yangu/gari/ nitatumia akiba yangu yote kufanya/kuepuka kutotokea kwa kifo!

4.Depression🙁Kudhoofu kwa kusononeka)
Mtu huepuka wale wanaokuja kumuona kwa kusudi la kumfariji(kuhani), marafiki na jamaa..mara nyingi huwana mawazo hasi kuhusu msiba, "kwa nini kuhangaika kote anyway?" ,"Haitasaidia lolote", "Ni kazi bure" n.k


Acceptance:
Mtu hukubali kuwa yaliyotokea yametokea, na hana uwezo wa kuyabadilisha ila kuendelea na maisha na kujifunza kutokana na msiba(kifo) hicho!


So, naamini baada ya muda "wanandugu hao wataelewa"..POLE kwao kwa msiba.
 
Nimeamua kuamka na swali hili baada ya ile habari ya wana ndugu wa marehemu aliyefariki tangu Ijumaa ya wiki hii kukataa kuamini kuwa amekufa na kuamua kumpeleka katika Kanisa la Ufufuo na Maombezi ili arudi kuwa hai. Je, pamoja na sisi kushinda na kukesha makanisani na misikitini bado tu hatuamini kuwa kuna kuzaliwa na kufa?

Amepekwa kwa Bwana ili amfufue.

Sent from my GT-I9300 using Tapatalk 2
 
Labda wanamdai,sasa wanahisi amevunga kufa!!
 
Back
Top Bottom