Kwanini tusiwe na maduka ya hadhi nchini ili mawaziri na viongozi wakubwa wasiagize kutoka nje ya nchi?

Kwanini tusiwe na maduka ya hadhi nchini ili mawaziri na viongozi wakubwa wasiagize kutoka nje ya nchi?

Resilience

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2023
Posts
1,096
Reaction score
4,948
Biashara zinaendeshwa Kariakoo kwa sasa hazina tofauti na biashara zilizokuwa zinafanyika miaka ya 1990 za ulanguzi.

Soko linazidi kudorora, maduka yenye hadhi yanazidi kupotea na kuzaliwa vibanda vidogo vidogo visivyo kidhi.

Mpangilio wa biashara nao unachangia soko kukosa mvuto huku bidhaa zenye ubora mdogo zikipewa kipaumbele.

Matokeo yake ni kuibuka kwa wafanyabiashara wachache waliopo serious wanaokwenda kwenye masoko nchi jirani kuchukua bidhaa na kuziingiza nchini kinyemela kisha kuziuza kwa bei kubwa kwa wateja serious.

Upotevu huu wa mapato unachangiwa kwa kiasi kikubwa na kodi nyingi, kukosekana kwa viongozi imara na sera mbovu.

Nchi nzima kuna maduka ya nguo za hadhi yasiyozidi kumi na mengi yanamilikiwa na mtu au kampuni moja. Kwanini tusiwasaidie Watanzania kufungua maduka yaliyopo kwenye ulimwengu wa kwanza hapa nchini?

Mawaziri na viongozi wengine wanaolipwa vizuri wanaenda kununua nguo nje. Kwanini badala ya kununua nje, wasitengeneze mazingira ya biashara kama ya nje? Tulitegemea kwa kuwa na bandari, watu wa madaraja yote wangeingia nchini kufanya biashara, ila sivyo. Tumebaki kutukuza vya Uturuki, Dubai na kadhalika.

Tubadili fikra.
 
Wateja watapatijana tu , maana nguonza kariakoo jama mtu anapiga hesabu vizuri ni hasara sana na very expensive in long run.
Bora hata ununue shati laki lakini lidumu, kuliko kununua shati 20, 000 halafu ukifua mara moja linapauka
Bado still uchumi hauruhusu. Ingekuwa kima cha chini cha mshahara ni million 5 kwa kila Kada huenda watu wangeweza kuvaa nguo za laki au zaidi. Sasa mshahara wa average guy laki 7 anaanzaje kuvaa nguo za laki 2?
 
Biashara zinaendeshwa Kariakoo kwa sasa hazina tofauti na biashara zilizokuwa zinafanyika miaka ya 1990 za ulanguzi.

Soko linazidi kudorora, maduka yenye hadhi yanazidi kupotea na kuzaliwa vibanda vidogo vidogo visivyo kidhi...
Mtanzania anapenda kitu quality kwa bei ya chini , kilichopo ni kumuuzia copy tuu , na mastermind wa huu mchezo ni mchina.. original waachie mafisadi
 
Wanunuzi wenyewe kipato kidogo sana
Wengi wanavaa mitumba na mwenye hela mwenyewe ananunua mradi liwe jipya tu ila sio brand maana hata kariakoo utakuta sandals
zimeandikwa Range Rover unajiuliza Range wanatoa mpaka malapa?
Wabongo wengi tunajisitiri tu hamna anayevaa brand OG hapa. Labda wa ushuani huko ambao wanaenda ulaya kama wanavyoenda Kariakoo.
 
Wateja watapatijana tu, maana nguonza Kariakoo. Jamaa anapiga hesabu vizuri ni hasara sana na very expensive in long run.

Bora hata ununue shati laki lakini lidumu, kuliko kununua shati 20,000 halafu ukifua mara moja linapauka.
Wateja wa kununa nguo moja USD 2500 watapatikana wangapi...
 
Uko sahihi, lakini nani anayejali? Hata Magufuli na kelele zake zote za kuwachukia mabeberu, hakufufua kiwanda hata kimoja cha nguo. Lakini pamba tunalima. Alivaa suti za mabeberu.
Watu sasa wanaangalia faida.ukiyaleta hayo maduka wanunuzi ni wachache na haya yaliyopo yanatosha.simu tu za quality zinatushinda iwe nguo yenye quality.

Labda kila mkoa kuwe na hayo maduka machache sambamba na haya ya akina sisi ya bei rahisi vinginevyo wengine tutarudi kuvaa kaniki kama enzi za zamani.
 
Biashara zinaendeshwa Kariakoo kwa sasa hazina tofauti na biashara zilizokuwa zinafanyika miaka ya 1990 za ulanguzi.

Soko linazidi kudorora, maduka yenye hadhi yanazidi kupotea na kuzaliwa vibanda vidogo vidogo visivyo kidhi...
Biashara haitegemei viongozi tu kama maduka ya middle class income kama mr price yanafunga biashara ndio ujue tz masikini wengi. Tanzania watu wana afford malunya ya vunja bei eti kiatu 10,000
 
Back
Top Bottom