Kwanini umzuie mke wako kuwa na simu ya mkononi wakati wewe unayo?

Kwanini umzuie mke wako kuwa na simu ya mkononi wakati wewe unayo?

GM7

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2009
Posts
492
Reaction score
24
Waheshimiwa sana wanaJF,
Nawauliza hasa wanaume, kwanini usimruhusu mke wako au mpenzi wako wa kike kuwa na simu ya mkononi wakati wewe unayo?

Katika tembeatembea nilikumkuta dada mmoja ambaye tunafahamiana, ana mtoto wake mmoja na ana mume. Katika maongezi mbalimbali nikamwambia siku hizi karibu mtu ana simu ya mkononi sasa kwa nini wewe huna simu kwa ajili ya mawasiliano wakati simu nyingine zinauzwa mpaka sh.10,000 tu? Akasema "ninue simu baba J atanielewa? Si atafikiri nawasiliana na wanaume wengine?"

Siku nyingine akaja mama mmoja kununua vocha kwangu. Katika maongezi naye akasema "mume wangu hajui kama nina simu ya mkononi, maana akijui tu nyumbani patakuwa hapatoshi. Yaani hapendi kabisa niwe na simu ya mkononi ila yeye tu awe anayo"

Swali kwa wanaume: Kwanini wanaume hawapendi wake zao kuwa na simu? Kuna tatizo gani mke wako kuwa na simu wakati wewe unayo?

Swali kwa wanawake:Kwa nini waume zenu hawawaamini mkiwa na simu? Mna matatizo gani yanayosababisha msiaminiwe kuhusu hili suala?

Karibu tuendelee kuchangia mada.
 
hayo yapoa sana, au anakwambia utatumia ya kwangu kutuma msg na kupitga,
Haoa ni wanaume wasiojiamini wala kuamini wake zao na wana wivu kupita kiasi.
Halafu wana mambo yao wanafanya nje, kwa hiyo anaogopa ukiwa na simu unaweza ukapata hata mtu wa kukutumia msg kukuambia mume wako yuko na fulani siku hizi au muda huu yuko mahali fulani,
wanaume wengi wanaonyima wake zao wasiwe na simu ni ambao utulivu 0 siyo waaminifu
 
Namshukru sana alieleta post hii maana jumamosi nilikutana dada mmoja nikamwuliza bado hujanunua simu akaniambia naogopa nikiwa na simu baba fulani hatutaelewana,nikamwuliza kwa nini msielewane yaani simu tu jamani akaniambia ndo hivyo,nikajaribu kufikiri kwa nini hataki kumnunulia mke wake simu?kuna kitu gani kinaendelea? kwa kweli sikupata majibu,labda hapa nitapata majibu,nakushukuru ulieanzisha hii mada.
 
Waheshimiwa sana wanaJF,
Nawauliza hasa wanaume, kwanini usimruhusu mke wako au mpenzi wako wa kike kuwa na simu ya mkononi wakati wewe unayo?

Katika tembeatembea nilikumkuta dada mmoja ambaye tunafahamiana, ana mtoto wake mmoja na ana mume. Katika maongezi mbalimbali nikamwambia siku hizi karibu mtu ana simu ya mkononi sasa kwa nini wewe huna simu kwa ajili ya mawasiliano wakati simu nyingine zinauzwa mpaka sh.10,000 tu? Akasema "ninue simu baba J atanielewa? Si atafikiri nawasiliana na wanaume wengine?"

Siku nyingine akaja mama mmoja kununua vocha kwangu. Katika maongezi naye akasema "mume wangu hajui kama nina simu ya mkononi, maana akijui tu nyumbani patakuwa hapatoshi. Yaani hapendi kabisa niwe na simu ya mkononi ila yeye tu awe anayo"

Swali kwa wanaume: Kwanini wanaume hawapendi wake zao kuwa na simu? Kuna tatizo gani mke wako kuwa na simu wakati wewe unayo?

Swali kwa wanawake:Kwa nini waume zenu hawawaamini mkiwa na simu? Mna matatizo gani yanayosababisha msiaminiwe kuhusu hili suala?

Karibu tuendelee kuchangia mada.


Hao wanawake wote waliofanyiwa hivyo wana tabia mbaya

sana .

Mabwana zao washastukia hilo ndo maana wamewapiga stop

kununua simu!

Hata mimi ningekuwa na mke wa hivyo ningemmeza

nikimwona na simu!

Sasa ona huyo mwingine, amekatazwa na bwanaake, bado

ametafuta ingine kwa siri na anaitumia pasipo bwanake

kujua! kweli hiyo inaswihi?

Hakuna wivu wala nini, ni wanawake hao ni wahuni too

much!

We unataka kuwasiliana na nani na huo usiri wako? Ni kwa

tija ya familia au ni kuwabania pua akina Fidel180?

Sh*iiit!
 
Wanawake wasio na simu wakati waume zao wanazo nafikiri wana mtindio wa ubongo, wewe inakuwaje huaminiki kwa mumeo? Au wewe mwanaume inakuwaje humwamini mkeo? Hayo maisha na mbagumu sana watu inaibidi kukemea tabia fulani kabla haijaota mizizi, ukiona mkeo anaenda kusiko piga kelele aache. Hata asipokuwa na simu kuna vibanda ataenda atapiga wakati hupo atafanya yote anayotaka then wewe unaonekana mjinga.

heheheheh
 
Waheshimiwa sana wanaJF,
Nawauliza hasa wanaume, kwanini usimruhusu mke wako au mpenzi wako wa kike kuwa na simu ya mkononi wakati wewe unayo?


Ndugu yangu wanawake wengine ni vicheche vya kutupa, kuwanyima mawasililiano ni njia mmojawapo ya kujipunguzia presha japo haisaidii sana kwa sababu wana namna zingine, kama huyo aliyetajwa anayo simu mumewe hajui!
 
Ndugu yangu wanawake wengine ni vicheche vya kutupa, kuwanyima mawasililiano ni njia mmojawapo ya kujipunguzia presha japo haisaidii sana kwa sababu wana namna zingine, kama huyo aliyetajwa anayo simu mumewe hajui!
Hii naona ni mojawapo ya sababu.
 
mmmm hii kali nilkuwa sijasikia wala kufikiria kuna mijiume ya ain hii... simu hata wewe mwnenyewe ukitaka kuwasiliana na mkeo jamani itakuwaje hapo? kama kuna dharura je? utaanza kupiga simu kwa jirani? wanaume wakware ndio wenye hii tabia wasije wakshikwa. mmm nayo teknology ndio mwisho mama anapata simu na anaiweka permanently on silent mode utajuaje?????
 
mmmm hii kali nilkuwa sijasikia wala kufikiria kuna mijiume ya ain hii... simu hata wewe mwnenyewe ukitaka kuwasiliana na mkeo jamani itakuwaje hapo? kama kuna dharura je? utaanza kupiga simu kwa jirani? wanaume wakware ndio wenye hii tabia wasije wakshikwa. mmm nayo teknology ndio mwisho mama anapata simu na anaiweka permanently on silent mode utajuaje?????

Halafu wengine waliobahatika kuwa na simu basi kila siku mume/mke anakagua simu ya mwenzake kuona nani kapiga simu au kutuma meseji. Halafu tena kuna wanaume wengine ukiangalia phonebook yake utakuta majina ya wanaume tu ili mkewe akiangalia asiwe na wasiwasi.
Kwa mfano mtu anaitwa Juliana lakini kwenye simu anaandika Julius. Kweli siku hizi uaminifu haupo.
 
KWa staili hiyo hata maendeleo yako nyumbani yatakuwa Magumu. Je ingekuwa vipi kama ungelipata kazi zambia mshahara milioni nne , kwa mwezi na huendi na mkeo ,kurudi nyumbani kila baada ya miezi mitatu contract duration ,2 years?
Wivu kupita kiasi ni hatari kwa maisha yako na kwa maendeleo ya familia pia .
THANKS JF MEMBERS FOR EDUCATING THE COMMUNITY
 
Back
Top Bottom