Kwanini unamiliki chuma

believer

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2012
Posts
639
Reaction score
216
Kuna kila dalili kuwa sasa wamiliki wa vyuma(bastola) mjini wamekuwa wengi,ikitokea kutoelewana kidogo kati ya mtu na mtu iwe ni bar,kwenye foleni,club nk,chuma kinatolewa na mara nyingine kutumiwa,ukiangalia mazingira ya kwann chuma imetumika hupati mantiki kabisa,sifungamani upande wowote,nataka kupata exposure zenu wadau,swali langu linakuja hivi,unamiliki chuma kwa kuwa
1.usalama sasa nchini ni mdogo?

2.imekuwa fashion kuwa na chuma?

3.for prestige?

4.to justify your status?

5.gap kati masikini na tajiri limepanuka?

6.vyuma vinapatikana kwa urahisi?

7.wababe wamekuwa wengi hivyo chuma ndo mkombozi......

wadau fungukeni
 
No:7 vijana wengi sasa ni watunisha misuli, ubabe nje nje,
 
Sababu zote ulizoorodhesha ndiyo sababu zinazofanya watu wamiliki Bastola...
 
Sababu ulizotoa hapo juu karibu zote sawa ....

Ila kuna wajinga wajinga wengi sana .... kutembea na kutongoza wake za wenzao ....kuingilia deal za wengine.....kujifanya wao ndio wapo juu.... sasa kuwapunguza hawa DAWA nunua MANATI YA MZUNGU tu .....akisikia paaaaa imemkosa
 
Kuna sababu kuu hujaiweka hapo, wezi wamekuwa wengi sana zama hizi na hali ya usalama Tanzania sio kama zamani!
 


Hukawii kuabishwa mbele ya mama mkwe,unakuta mmekwaruzana kidogo kwenye traffic jam,kosa lake labda kachomekea,kwasababu ni mwili jumba anatoka akuchape,hapo chuma mwokozi.
 
Hukawii kuabishwa mbele ya mama mkwe,unakuta mmekwaruzana kidogo kwenye traffic jam,kosa lake labda kachomekea,kwasababu ni mwili jumba anatoka akuchape,hapo chuma mwokozi.

Tena hapo mama mkwe atafurahi sana kuona mume wa mwanaye ana chamoto hivyo usalama upo nyumbani.....na atamwambia mwanae aache tabia mbaya kama alikuwa nazo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…