Kwanini UVCCM hamkemei matukio ya watu kutekwa?

Kwanini UVCCM hamkemei matukio ya watu kutekwa?

Bila bila

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2016
Posts
22,168
Reaction score
39,118
Matukio yote ambayo Vijana wanatekwa hasa Wenye mlengo wa kukosoa serikali, UVCCM haijawahi kutoa tamko la kukemea hata kinafiki tu. Tukio la karibuni zaidi ni la kijana Edgar Mwakabela @SATIVA ambaye alitekwa Dar na kutupwa Katavi baada ya kupigwa risasi ya kichwa lakini Mungu mkubwa ikamvunja taya tu.

Alipohojiwa akataja baada ya kutekwa alilazwa karakana ya kituo cha Polisi Oesterbay kisha Arusha na baadaye Katavi ili akauawe. Kwa siku zote kelele zikipigwa mitandaoni huku Polisi wakituhumiwa UVCCM walikuwa kimya utadhani wao ndio Polisi wanaotuhumiwa.

Kinachonishangaza zaidi ni pale Zitto Kabwe aliposema ameongea na Rais Samia na ameahidi kulipia sehemu ya gharama za matibabu na akafanya hivyo, ghafla UVCCM wameibuka na kumpongeza Rais.

Hii ni Aina mbovu ya uhuni na kukosa busara. Unakaa husemi chochote nilipotekwa, Niko hospitali mahutuki uko kimya, ghafla unasikia kiongozi Fulani katoa hela ya matibabu unakurupuka kupongeza.

Ndo màana Kwa ukimya wao hata Mwenyekiti wao alipotoa mchango alirudishiwa mchango wake. Hii ilikuwa sahihi hata vijijini inafanyika. Mtu kapotea kijijini Vijana tunatoka kwenda kumtafuta wewe unakwenda kufungua Duka lako, kesho maiti yake ikipatikana unakuwa wa Kwanza kuleta ramborambi kwenye daftari la Mtaa Kwa nini tusikurudishie?
 

Attachments

  • 20240704_071528.jpg
    20240704_071528.jpg
    179.8 KB · Views: 4
Si kila siku wao wanasema mtu akiisema serekali vibaya na akimsema mama watadili nae, umesahau walitoa hadi tahadhari polisi wasiingilie wakishughulikia watu wanaomsema mama na serekali yake?

Unawatengajishaje na wanaoteka watu waikosoao serekali? Kwa lugha nyingine unataka wajikemee?
 
Nenda Youtube, search ''HAKI TV'' uone jinsi mkazi anayeishi karibu na msitu wa Kongowe anavyolalamika maiti za vijana zinavyotupwa kwenye msitu kila uchao. Hazijulikani ni za kina nani, na zinaletwa na magari. Polisi wakiarifiwa wanawaambia wanakijiji zifukieni.
 
Nenda Youtube, search ''HAKI TV'' uone jinsi mkazi anayeishi karibu na msitu wa Kongowe anavyolalamika maiti za vijana zinavyotupwa kwenye msitu kila uchao. Hazijulikani ni za kina nani, na zinaletwa na magari. Polisi wakiarifiwa wanawaambia wanakijiji zifukieni.
Nilimshangaa Waziri ninayeamini ana uwezo mdogo kuliko wote (Masauni) anasema mpaka Sasa waliotekwa ni 8 tu.
 
Matukio yote ambayo Vijana wanatekwa hasa Wenye mlengo wa kukosoa serikali, UVCCM haijawahi kutoa tamko la kukemea hata kinafiki tu. Tukio la karibuni zaidi ni la kijana Edgar Mwakabela @SATIVA ambaye alitekwa Dar na kutupwa Katavi baada ya kupigwa risasi ya kichwa lakini Mungu mkubwa ikamvunja taya tu.

Alipohojiwa akataja baada ya kutekwa alilazwa karakana ya kituo cha Polisi Oesterbay kisha Arusha na baadaye Katavi ili akauawe. Kwa siku zote kelele zikipigwa mitandaoni huku Polisi wakituhumiwa UVCCM walikuwa kimya utadhani wao ndio Polisi wanaotuhumiwa.

Kinachonishangaza zaidi ni pale Zitto Kabwe aliposema ameongea na Rais Samia na ameahidi kulipia sehemu ya gharama za matibabu na akafanya hivyo, ghafla UVCCM wameibuka na kumpongeza Rais.

Hii ni Aina mbovu ya uhuni na kukosa busara. Unakaa husemi chochote nilipotekwa, Niko hospitali mahutuki uko kimya, ghafla unasikia kiongozi Fulani katoa hela ya matibabu unakurupuka kupongeza.

Ndo màana Kwa ukimya wao hata Mwenyekiti wao alipotoa mchango alirudishiwa mchango wake. Hii ilikuwa sahihi hata vijijini inafanyika. Mtu kapotea kijijini Vijana tunatoka kwenda kumtafuta wewe unakwenda kufungua Duka lako, kesho maiti yake ikipatikana unakuwa wa Kwanza kuleta ramborambi kwenye daftari la Mtaa Kwa nini tusikurudishie?
Tabia ya kichawi .
 
Matukio yote ambayo Vijana wanatekwa hasa Wenye mlengo wa kukosoa serikali, UVCCM haijawahi kutoa tamko la kukemea hata kinafiki tu. Tukio la karibuni zaidi ni la kijana Edgar Mwakabela @SATIVA ambaye alitekwa Dar na kutupwa Katavi baada ya kupigwa risasi ya kichwa lakini Mungu mkubwa ikamvunja taya tu.

Alipohojiwa akataja baada ya kutekwa alilazwa karakana ya kituo cha Polisi Oesterbay kisha Arusha na baadaye Katavi ili akauawe. Kwa siku zote kelele zikipigwa mitandaoni huku Polisi wakituhumiwa UVCCM walikuwa kimya utadhani wao ndio Polisi wanaotuhumiwa.

Kinachonishangaza zaidi ni pale Zitto Kabwe aliposema ameongea na Rais Samia na ameahidi kulipia sehemu ya gharama za matibabu na akafanya hivyo, ghafla UVCCM wameibuka na kumpongeza Rais.

Hii ni Aina mbovu ya uhuni na kukosa busara. Unakaa husemi chochote nilipotekwa, Niko hospitali mahutuki uko kimya, ghafla unasikia kiongozi Fulani katoa hela ya matibabu unakurupuka kupongeza.

Ndo màana Kwa ukimya wao hata Mwenyekiti wao alipotoa mchango alirudishiwa mchango wake. Hii ilikuwa sahihi hata vijijini inafanyika. Mtu kapotea kijijini Vijana tunatoka kwenda kumtafuta wewe unakwenda kufungua Duka lako, kesho maiti yake ikipatikana unakuwa wa Kwanza kuleta ramborambi kwenye daftari la Mtaa Kwa nini tusikurudishie?
Hili jambo linanishangaza sana.

Wao hayawahusu kabisa
 
Back
Top Bottom