Kwanini Waafrika wengi hupitia malezi ya "kinidhamu" sana lakini huwa watu wazima wa ovyo

Kwanini Waafrika wengi hupitia malezi ya "kinidhamu" sana lakini huwa watu wazima wa ovyo

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Malezi ya waafrika nyumbani hadi shuleni huwa ya kuwanyoosha wawe watu wenye nidhamu. Hupewa adhabu kali iwapo watashindwa kufuata nidhamu.

Sasa inakuwaje watu kama hawa wakiwa watu wazima hugeuka watu wa hovyo. Huwa wezi na mafisadi. Wabinafsi wanaojali matumbo yao tu, waongo kupindukia. Wadokozi. Wasiojali maadili. Waliokosa nidhamu ya kazi.

Kuna haja ya kureform namna tunavyolelewa na kufunzwa utotoni ili tuje kuwa watu bora?
 
Malezi ya waafrika nyumbani hadi shuleni huwa ya kuwanyoosha wawe watu wenye nidhamu. Hupewa adhabu kali iwapo watashindwa kufuata nidhamu.

Sasa inakuwaje watu kama hawa wakiwa watu wazima hugeuka watu wa hovyo. Huwa wezi na mafisadi. Wabinafsi wanaojali matumbo yao tu, waongo kupindukia. Wadokozi. Wasiojali maadili. Waliokosa nidhamu ya kazi.

Kuna haja ya kureform namna tunavyolelewa na kufunzwa utotoni ili tuje kuwa watu bora?


Waafrika katika mifumo ya Kimagharibi na mila za kimagharibi wanatakiwa watawaliwe kijeshi .

Kutawala na kumuongoza kinyanya mtu aliyezoea ukorofi na adhabu kali ni tatizo sana .

Ndio maana wazungu walituletea dini kwanza maana binadamu kwa hulka yake ni mbinafsi mpaka pawe na sheria yenye adhabu kali dhidi yake .

Mafano tu kipindi cha JPM sheria zilifuatwa sana ,uhalifu ukapungua sana . Mauaji ya wazee ,watoto , albino na imani za kishirikina na utapeli vilipungua sana . Ufisadi na janjanja za wakwepa kodi zikapungua .

Kupanga ni kuchagua kama tunaona kuna ufisadi basi ni jukumu la serikali ya CCM kuondoa ufisadi na kama waleshindwa tuwaondoe wao vkwenye kura halali au bora Wale wakina Traore watawale tunyoshane kidogo .

Laini pia kuna jambo moja lipo wazi Binadamu ameumbwa na Mungu hivyo kuna hulka fulani ya kimungu ndani yake .

Mfano : Mwalimu Melvi, Mzinzi ,mfiraji na asiyejihashimu hata akimuadhibu mtoto kamwe hawezi kumbadilisha maana anayetoa adhabu mwenyewe aliyakiwa awe amefukuzwa Kazi mapema maana hastahili kabisa kuwepo kazini .

Hali ladhalika Mahakama na vyombo vya dola ,vinaongozwa na watu waovu wasiotii sheria kabisa wala matendo yao hayafai ,wavunja sheria maka za maadili na hata sheria za asili achilia mbali sheria za kazi zao . Watu kama hao kwa karma ya asili ya ulimwengu na uumbaji hawawezi kubadili jamii ikawa na watu wema.

Waovu wakitawala watu huugua. Ubaya kuna wakati unapewa nafasi ili kuwafanya watu wote waishi kwa wasiwasi na hofu kuu bila kujali elimu ,utajiri au umaskini . Jamii yenye watu waovu inaishi katika uovu wake ili watu wote waugue kwenye mioyo na nafsi zao.

Safisheni kikombe kwa ndani kabla ya nje ndipo muweke kinywaji .

Mfumo ulezoeleka kwa sababu CCM imejiwekea kakundi kake kadogo na kila anayesujudu mbele yao anaishi bila kufuata sheria na anakua salama .
Ufisadi umekua ni mazoea na wanaoupinga wafu wanawashangaa.
Walimu enzi za mkoloni walikua ni watu smart sana wenye tabia na mwenendo unaofaa kuigwa na jamii nzima . Siku hizi utasikia mwalimu kalawiti mwanfunzi wa kidato cha kwanza halafu chama cha walimu kinamtetea mpaka kuweka wakili na gharama zake lakini maslahi ya walimu chama hicho hakina habari nayo kinageuka kuwa chama cha machawa .
 
mada ngumu sijawahi kuona

mimi nadhani;

tunafundishwa kuzoea umasikini, kujua/kuzoea shida ni sifa, kwahiyo wale viongozi hawaoni uzito wa suala zima la umasikini

"they don't know what's at stake"
 
Malezi ya waafrika nyumbani hadi shuleni huwa ya kuwanyoosha wawe watu wenye nidhamu. Hupewa adhabu kali iwapo watashindwa kufuata nidhamu.

Sasa inakuwaje watu kama hawa wakiwa watu wazima hugeuka watu wa hovyo. Huwa wezi na mafisadi. Wabinafsi wanaojali matumbo yao tu, waongo kupindukia. Wadokozi. Wasiojali maadili. Waliokosa nidhamu ya kazi.

Kuna haja ya kureform namna tunavyolelewa na kufunzwa utotoni ili tuje kuwa watu bora?
Masikini huwa hana uwezo wa kujitambua hadi anafukiwa shimoni.
 
Malezi ya waafrika nyumbani hadi shuleni huwa ya kuwanyoosha wawe watu wenye nidhamu. Hupewa adhabu kali iwapo watashindwa kufuata nidhamu.

Sasa inakuwaje watu kama hawa wakiwa watu wazima hugeuka watu wa hovyo. Huwa wezi na mafisadi. Wabinafsi wanaojali matumbo yao tu, waongo kupindukia. Wadokozi. Wasiojali maadili. Waliokosa nidhamu ya kazi.

Kuna haja ya kureform namna tunavyolelewa na kufunzwa utotoni ili tuje kuwa watu bora?
Mkuu; Hapo ujue:
1. Yale waliyokuwa wanadhibitiwa (walizuiwa) wasiyatende utotoni ndo wanayafidia (compensate) wakiwa ukubwani kwani ktk umri huo wako huru.
2. Ukubwani; Waafrika wengi wanagundua kwamba mengi kati ya yale waliyokuwa wanazuiwa kutenda ilikuwa ni halali na haki yao kuyatenda. Lakini kwa sasa muda umeshapita na hawakujifunza lolote la maana zaidi ya Nidhamu ya Woga na muda wao umepotea bure. Ni katika hali hiyo wanakuwa na disguised frustrations, confused guys, chuki/nyongo/roho ya kutu katika jamii kana kwamba hiyo jamii ndo iliwatenda na imewafikisha hapo. Hawamwoni mtu wa kumlalamikia directly kuwa ndiye kisababishi kwa hali yao.
 
Mwafrika unakuta mzazi anapiga mtoto viboko au makofi kisa anacheza
Akirudi mchafu anapigwa kama kibaka
Akifeli mtihani anapigwa haswa ila hasaidiwi makosa yake ila ni kudunda tu

Hiyo nidhamu unayoisema ni ipi hapo?
Mtoto mdogo anahitaji msaada mkubwa sana wa kujua mabaya na mazuri kwa kusimamiwa na kufundishwa
Mzazi anakuwa adui mkubwa wa mtoto sasa wizi utakosekanaje hapo
Ukiwa adui na mtoto atafanya mabaya yote akijua ndio furaha yake

Wazazi lazima tuwe na ukaribu na watoto na kuwafundisha mema na kuwalataza mabaya
Mzazi ana matusi balaa kila dogo akifanya kosa ni matusi na kipigo

Halafu mnaita eti nidhamu
Hiyo sio nidhamu bali ni ujinga wa baadhi ya wazazi na hawajui malezi

Mtoto ni lazima acheze na wewe kama mzazi mwangalie na huku ukimuonya hatari zinazoweza kutokea
 
Tatizo la mwafrika mshipa wa haja kubwa na ubongo vimeungana na kadri tunavyokuwa huo mshipa unazid kutanuka na kusababisha uharibifu wa akili.
 
Waafrika katika mifumo ya Kimagharibi na mila za kimagharibi wanatakiwa watawaliwe kijeshi .

Kutawala na kumuongoza kinyanya mtu aliyezoea ukorofi na adhabu kali ni tatizo sana .

Ndio maana wazungu walituletea dini kwanza maana binadamu kwa hulka yake ni mbinafsi mpaka pawe na sheria yenye adhabu kali dhidi yake .

Mafano tu kipindi cha JPM sheria zilifuatwa sana ,uhalifu ukapungua sana . Mauaji ya wazee ,watoto , albino na imani za kishirikina na utapeli vilipungua sana . Ufisadi na janjanja za wakwepa kodi zikapungua .

Kupanga ni kuchagua kama tunaona kuna ufisadi basi ni jukumu la serikali ya CCM kuondoa ufisadi na kama waleshindwa tuwaondoe wao vkwenye kura halali au bora Wale wakina Traore watawale tunyoshane kidogo .

Laini pia kuna jambo moja lipo wazi Binadamu ameumbwa na Mungu hivyo kuna hulka fulani ya kimungu ndani yake .

Mfano : Mwalimu Melvi, Mzinzi ,mfiraji na asiyejihashimu hata akimuadhibu mtoto kamwe hawezi kumbadilisha maana anayetoa adhabu mwenyewe aliyakiwa awe amefukuzwa Kazi mapema maana hastahili kabisa kuwepo kazini .

Hali ladhalika Mahakama na vyombo vya dola ,vinaongozwa na watu waovu wasiotii sheria kabisa wala matendo yao hayafai ,wavunja sheria maka za maadili na hata sheria za asili achilia mbali sheria za kazi zao . Watu kama hao kwa karma ya asili ya ulimwengu na uumbaji hawawezi kubadili jamii ikawa na watu wema.

Waovu wakitawala watu huugua. Ubaya kuna wakati unapewa nafasi ili kuwafanya watu wote waishi kwa wasiwasi na hofu kuu bila kujali elimu ,utajiri au umaskini . Jamii yenye watu waovu inaishi katika uovu wake ili watu wote waugue kwenye mioyo na nafsi zao.

Safisheni kikombe kwa ndani kabla ya nje ndipo muweke kinywaji .

Mfumo ulezoeleka kwa sababu CCM imejiwekea kakundi kake kadogo na kila anayesujudu mbele yao anaishi bila kufuata sheria na anakua salama .
Ufisadi umekua ni mazoea na wanaoupinga wafu wanawashangaa.
Walimu enzi za mkoloni walikua ni watu smart sana wenye tabia na mwenendo unaofaa kuigwa na jamii nzima . Siku hizi utasikia mwalimu kalawiti mwanfunzi wa kidato cha kwanza halafu chama cha walimu kinamtetea mpaka kuweka wakili na gharama zake lakini maslahi ya walimu chama hicho hakina habari nayo kinageuka kuwa chama cha machawa .
Asante sana kwa kushare andiko hili. Utawala unaojiita wa kidemokrasia huku ukiwa sio, ni mzizi wa udanganyifu kwenye kila sekta ya maisha yetu.

Sasa sababu unafaidika na utazidi kufaidika na ujinga na habari nyenyepesi kuhusu watu wake huku mzizi wa yote hayo ni mkubwa sana hakuna ambae anayeweza kuthubutu kupambana nao kuutoa sababu kila mmoja alishawahi kushiriki, hivo wanabaki kuuendeleza hivo hivo japo wana maumivu makubwa huku wakistaafu wakitamani wangekua na guts za kufanya kitu flani kwa taifa lao. CCM unlike CCP in china haijawekeza kwenye technology na nguvu zao za utawala wamekeza kwenye cheap propaganda na ujinga wa jamii yetu kitu ambacho sio endelevu. CCM inabidi iwekeze kwenye Elimu na Technology japo ikiwadhuru wao lakini kwa faida ya Taifa letu. Elimu,Elimu,Elimu.
 
Asante sana kwa kushare andiko hili. Utawala unaojiita wa kidemokrasia huku ukiwa sio, ni mzizi wa udanganyifu kwenye kila sekta ya maisha yetu.

Sasa sababu unafaidika na utazidi kufaidika na ujinga na habari nyenyepesi kuhusu watu wake huku mzizi wa yote hayo ni mkubwa sana hakuna ambae anayeweza kuthubutu kupambana nao kuutoa sababu kila mmoja alishawahi kushiriki, hivo wanabaki kuuendeleza hivo hivo japo wana maumivu makubwa huku wakistaafu wakitamani wangekua na guts za kufanya kitu flani kwa taifa lao. CCM unlike CCP in china haijawekeza kwenye technology na nguvu zao za utawala wamekeza kwenye cheap propaganda na ujinga wa jamii yetu kitu ambacho sio endelevu. CCM inabidi iwekeze kwenye Elimu na Technology japo ikiwadhuru wao lakini kwa faida ya Taifa letu. Elimu,Elimu,Elimu.


Mimi siamini katika Demokrsia ya Kitapeli inayofanywa na watawala wa Afrika .
Haitatufikisha mbali zaidi ya kuurudisha Ukoloni kwa mgongo wa nyuma huku wao wakijiwekea sheria za kujitajirisha wao na familia zao kwa vizazi na vizazi .

Hata ulaya na Marekani haikuingia kwenye Demokrsia kitapeli . Walitokea watu wanaoamini na kuiiishi demokrasia ndio wakaleta mapinduzi ya kisiasa .
Kama hatuwezi kupigania demokrasia ya kweli tukamweka madarakani mtu kama Tundu Lisu anayeamini katika Demokrsia basi ni bora pasiwe na huu ujinga wa Demokrasia yenye Raia wanaoamrisha Jeshi kutumia mabavu dhidi ya wananchi wake .

Yaani unakua na chama Tawala kinachopandikiza wanajeshi makada kwa ajili ya kupambana na wapinzani. Hii ni hatari sana maana panakua na kufitiniana ndani kwa 'ndani kwenye vyombo vya dola . Matokeo yake ni kujipendekeza kwa kufanya ubaya badala ya kusimamia majukumu ya vyombo hivyo .Wale wanaoonekana kutorudhishwa na mfumo huo wanafinywa kimya kimya matokeo yake ni udumavu mkubwa wa Demokrasia
Sasa kwa nini tuwe na matumaini ya kupata demokrasia kwenye mfumo wa kijeshi unaojivika koti la demokrasia huku yanayofanyika ni mabaya zaidi ya nchi za kijeshi.

Uganda sio nchi ya Kijeshi ni nchi ya kiraia na kidemokrasia ya vyama vingi .
Rwanda sio nchi ya kijeshi ni nchi ya kidemokrasia ya vyama vingi kama ilivyo Tanzania.

Zote Rwanda ,Uganda na Tanzania zinafanya chaguzi za maigizo huku ziki poteza fedha nyingi bila sababu. Kama wanajua kuwa hawataki kushindwa basi wasipoteze pesa za umma kufanya uchaguzi .

Teknolojia ni kipaji kinachoweza kutokea popote kwa sababu inafumula zake . Kinachotakiwa ni uwekezaji na kuwatumia wataalam wa ndani.
Hivi kiwanda cha Tairi kilikufa kwa sababu ya teknolojia au usimamizi mbovu ?
Kiwanda cha viberiti kilikufa kwa sababu ya nini ?
Je ,CCM inajua tu kupambana na akina Dr. Slaa lakini sio wezi wa mali za umma ?
Kiwanda cha Tan bond kilikufaje wakati wasomi wakiwa wachache kilifanya kazi ,wasomi na soko limekua kubwa kiwanda kinakufa .
Watawala wanashirikiana na wawekezaji kutoka nje kuua mali za umma.
Tulikua na kiwanda cha redio ,kiwanda cha baiskeli cha swala. Kiwanda cha kuunganisha magari ya Scania . Kiwanda cha Jeshi cha Nyumbu cha kutengeneza magari . Kiwanda cha nyama kinakufa wakati soko linaongezeka .
Kilifanya kazi soko likiwa
Mwafrika unakuta mzazi anapiga mtoto viboko au makofi kisa anacheza
Akirudi mchafu anapigwa kama kibaka
Akifeli mtihani anapigwa haswa ila hasaidiwi makosa yake ila ni kudunda tu

Hiyo nidhamu unayoisema ni ipi hapo?
Mtoto mdogo anahitaji msaada mkubwa sana wa kujua mabaya na mazuri kwa kusimamiwa na kufundishwa
Mzazi anakuwa adui mkubwa wa mtoto sasa wizi utakosekanaje hapo
Ukiwa adui na mtoto atafanya mabaya yote akijua ndio furaha yake

Wazazi lazima tuwe na ukaribu na watoto na kuwafundisha mema na kuwalataza mabaya
Mzazi ana matusi balaa kila dogo akifanya kosa ni matusi na kipigo

Halafu mnaita eti nidhamu
Hiyo sio nidhamu bali ni ujinga wa baadhi ya wazazi na hawajui malezi

Mtoto ni lazima acheze na wewe kama mzazi mwangalie na huku ukimuonya hatari zinazoweza kutokea

Watoto haohao walikua wanakua walimu na makisi . Kama sio neema ya Mungu basi wanakua walimu katili sana na mapolisi katili sana .

Mwalimu anamchapa mwanafunzi kwa hasira na wakati mwingine anakua na chuki kabisa na mwanafunzi tena wa Nursary . Wanafunzi nao wangekuwa kuwa wahalifu wakiwa shuleni .

Mfano shule nyingi za boding za serikali ,wanafunzi hasa wa kidato cha nne wakimaliza shule wanaharibu miundo mbinu ya shule .Wanavunja taa za umeme ,wanavunja vioo,wanavunja ,koki za bomba ,wanavunja swichi na kufanya fujo nyingi .Yaani wanakosa malezi ya kupenda mali ya umma. Na walimu wanashindwa kuwaandaa kwa kuwafundisha umuhimu wa Kulinda na kuthamini mali za umma.

Siku hizi kila idara watu ni waoga wa kutaja neno haki na uzalendo.

Yaani mwalimu alitaja uzalendo anaonekana ni mpinzani /Chadema hivyo ni rahisi kushughulikiwa maana walimu wengi wamekua machawa hasa wale wenye elimu kubwa zaidi . Yaani kama ni shule ya msingi akishapata kadiploma au kadigrii anageuka kuwa Chawa ili mambo yake yaende.
Mwalimu akichaguliwa kuwa Mjumbe wa CWT anageuka kuwa Kada ili akila pesa za chama cha walimu asiguswe na ukihoji sana wanakuchongea wewe ni Chadema.
Hali kadhali ndani ya Polisi na vyombo vingine vyote vya Dola mpaka mahakama . Ukizungumzia haki na uzalendo unaitwa mpinzani . Yaani CCM haipo tena kwa ajili ya kusimamia sheria na haki katika nchi hii .
CCM imetekwa na genge la wahalifu wenye silaha kama basi linavyoweza kutekwa na majambazi .
Basi lilitekwa na majambazi hata wakisema vua nguo mbele ya mama mkwe na baba mkwe inabidi uvue na ukikataa wanakuua . CCM imetekwa na genge la mafisadi wachache ambao wanalindana na wanashindana kujilimbikizia mali . Yaani kuna familia sasa zinashindana kujilimbikizia mali kupitia fedha za umma . Na hao sasa wanamtumia De.Samia kama mlinzi wao kwa sababu ana majeshi nyuma yake na mahakama inaogopa kutoa haki maana ukizungumzia haki basi wewe ni Chadema .

Ndio maana leo wakristo wote wanaonekana ni Chadema kwa sababu wito mkubwa wa ukristo ni kutenda haki na kuwa na kiasi , Kutoa kodi kwa haki , kupenda wengine kama nafsi yako ,kuwatendea wengine kile ambacho wewe unakipenda utendewe na kufurahia uhuru ndani ya Kristo . Sasa Maaskofu na wachungaji wa kweli wanaonekana ni Chadema kwa sababu wanhubiri injili inayozungumzia Haki . Waislam wale wenye jitihada zao binafsi za kujitafutia riziki na uwezo wa kupambanua mambo na kusimama kwenye Ukweli uliopo ndani ya Quran na hadithi za mtume nao pia wamekua wakipigwa vita na hata kuawa kama Ally Kibao kwa sababu tu wanasema Ukweli kuwa Uislama kwa karne nyingi ulipigania Haki ya waarabu mpaka wakajikomboa . Lakini kinachotokea ni CCM kutekwa na matajiri waotoa rushwa na mapesa mengi kwenye nyumba za ibada na kujenga nyumba za ibada.
Mbaya zaidi ni kutafsiri vibaya sadaka zinazotolewa na fedha chafu kuwa zinafuta dhambi zote .
Kama ni kweli kuwa sadaka zinafuta dhambi zote basi tuseme chini ya CCM Tanzania inaangamia kwa kasi kubwa sana.

Magaidi hua wanatengenezwa na genge la matajiri ndani ya mifumo . Haya tuliyaona awamu ya Nne wakati JK anakaribia kumaliza Muda wake . Ugaidi ulipamba Moto mpaka Jeshi la Wananchi kushirikiana na vikosi maalum vya polisi vikaingilia kuwasaka baada ya Magufuli kuingia . Ina maana kuwa kama JPM angezubaa nchi ingegawanyika na isibgetawalika wakati huo huo kuna watu walikua wanapewa matrilon ya pesa toka Uarabuni kwa sababu ya kuivuruga nchi ndio maana JPM alizuia pesa zote kutoka nje ili magaidi wakose wadhamini na misaada . Majeshi yetu chini ya Mzalendo Magufuli wakafanikiwa kuwaondoa magaidi mengine yakakimbilia Msumbiji. Genge lao liliojaribu kuingiza nchi kwenye ugaidi wengi wapo sasa na wameinua mikia juu kwa furaha kuu. Vyombo vya dola vikiichekea hii CCM isiyotaka uchaguzi wa kura vitakuja kupata kazi kubwa sana huko mbeleni kwa sababu CCM haijali tena ustawi wa nchi zaidi ya kujichotea mali za umma .

Jeshi na polisi wamekaa kimya Bandari zinauzwa kwa Watu ambao kwa historia waliwahi kugawana rasilimali zetu kwa damu za watu na kuzifanya kuwa zao kwa ajili ya kujitajirisha.

Kama karne kumi na mbili zilizopita waarabu waliwaza kuja kuchukua Pembe za ndovu na dhahabu na mbao Tanganyika leo karne ya ishiri na moja unategemea lile wazo limepotea ?

Bila shaka waarabu hawakuondoka Tanganyika kwa kupenda bali waliondoka baada ya uhuru . Mbaya zaidi wana ndugu wengi humu wanaotumika sasa kuhujumu nchi.

Hata kwenye mitandoa kuna wahuni wengi na machawa wengi wenye asili ya kigeni kazi yao ni kujenga chuki na kutukana watu matusi makubwa sana . Wanamtulaka mpaka baba wa Taifa aliyeanzisha Jeshi la wananchi wa Tanzania kwa heshima kubwa . Aliyeanzisha Usalama wa Taifa kwa heshima kubwa . Aliyelinda rasilimali za nchi hii kwa ajili ya vizazi vyetu kwa heshima kubwa . Leo wametokea wahuni wanamtukana Nyerere ,wanawatukana maaskofu , wanawatukana Wanaharakati na kuwatukana watu wote wanaozungumzia habari ya haki ,uhuru,utu,umoja na mshikamano wetu uliokuwepo ,uzalendo na ulinzi wa rasilimali zetu.
Chaa ajabu hao wahuni hawakamatwi bali anayakamatwa na kunyanyaswa ni Dr. Slaa .
Unaachia magaidi yaliyochoma moto makanisa Zanzibar na kuua mapadri na kuwamwagia tindikali halafu unamfunga Padri Slaa anayeonya kuhusu ufisadi unaofanywa na wahuni kwenye nchi yetu . Inawezekana yale magaidi ndiyo yamegeuka kuwa machawa mitandoani .
 
Waafrika the babaric race hamfundishwi nidhamu au utu,bali mnafundishwa UWOGA NA KUSISITIZWA KUTOHOJI.Hii inakoma pale mtu anapopata LIFE INDEPENDENCE/FINANCIAL FREEDOM.Hapo mtu kama alikuwa hapendi kwenda kanisani au msikitini ataanza kujionyesha wazi.Kama alikuwa hanywi pombe atafungulia bomba n.k.

Kwahiyo hakuna lakushangaza ni mfumo wa kurithi toka kwenye ukoloni kwa kiasi flani na toka katika mila na tamaduni za mtu mweusi.Mfumo huu unawataka muwe submissive all time kwa mamlaka zilizo juu yenu.
 
Mimi siamini katika Demokrsia ya Kitapeli inayofanywa na watawala wa Afrika .
Haitatufikisha mbali zaidi ya kuurudisha Ukoloni kwa mgongo wa nyuma huku wao wakijiwekea sheria za kujitajirisha wao na familia zao kwa vizazi na vizazi .

Hata ulaya na Marekani haikuingia kwenye Demokrsia kitapeli . Walitokea watu wanaoamini na kuiiishi demokrasia ndio wakaleta mapinduzi ya kisiasa .
Kama hatuwezi kupigania demokrasia ya kweli tukamweka madarakani mtu kama Tundu Lisu anayeamini katika Demokrsia basi ni bora pasiwe na huu ujinga wa Demokrasia yenye Raia wanaoamrisha Jeshi kutumia mabavu dhidi ya wananchi wake .

Yaani unakua na chama Tawala kinachopandikiza wanajeshi makada kwa ajili ya kupambana na wapinzani. Hii ni hatari sana maana panakua na kufitiniana ndani kwa 'ndani kwenye vyombo vya dola . Matokeo yake ni kujipendekeza kwa kufanya ubaya badala ya kusimamia majukumu ya vyombo hivyo .Wale wanaoonekana kutorudhishwa na mfumo huo wanafinywa kimya kimya matokeo yake ni udumavu mkubwa wa Demokrasia
Sasa kwa nini tuwe na matumaini ya kupata demokrasia kwenye mfumo wa kijeshi unaojivika koti la demokrasia huku yanayofanyika ni mabaya zaidi ya nchi za kijeshi.

Uganda sio nchi ya Kijeshi ni nchi ya kiraia na kidemokrasia ya vyama vingi .
Rwanda sio nchi ya kijeshi ni nchi ya kidemokrasia ya vyama vingi kama ilivyo Tanzania.

Zote Rwanda ,Uganda na Tanzania zinafanya chaguzi za maigizo huku ziki poteza fedha nyingi bila sababu. Kama wanajua kuwa hawataki kushindwa basi wasipoteze pesa za umma kufanya uchaguzi .

Teknolojia ni kipaji kinachoweza kutokea popote kwa sababu inafumula zake . Kinachotakiwa ni uwekezaji na kuwatumia wataalam wa ndani.
Hivi kiwanda cha Tairi kilikufa kwa sababu ya teknolojia au usimamizi mbovu ?
Kiwanda cha viberiti kilikufa kwa sababu ya nini ?
Je ,CCM inajua tu kupambana na akina Dr. Slaa lakini sio wezi wa mali za umma ?
Kiwanda cha Tan bond kilikufaje wakati wasomi wakiwa wachache kilifanya kazi ,wasomi na soko limekua kubwa kiwanda kinakufa .
Watawala wanashirikiana na wawekezaji kutoka nje kuua mali za umma.
Tulikua na kiwanda cha redio ,kiwanda cha baiskeli cha swala. Kiwanda cha kuunganisha magari ya Scania . Kiwanda cha Jeshi cha Nyumbu cha kutengeneza magari . Kiwanda cha nyama kinakufa wakati soko linaongezeka .
Kilifanya kazi soko likiwa


Watoto haohao walikua wanakua walimu na makisi . Kama sio neema ya Mungu basi wanakua walimu katili sana na mapolisi katili sana .

Mwalimu anamchapa mwanafunzi kwa hasira na wakati mwingine anakua na chuki kabisa na mwanafunzi tena wa Nursary . Wanafunzi nao wangekuwa kuwa wahalifu wakiwa shuleni .

Mfano shule nyingi za boding za serikali ,wanafunzi hasa wa kidato cha nne wakimaliza shule wanaharibu miundo mbinu ya shule .Wanavunja taa za umeme ,wanavunja vioo,wanavunja ,koki za bomba ,wanavunja swichi na kufanya fujo nyingi .Yaani wanakosa malezi ya kupenda mali ya umma. Na walimu wanashindwa kuwaandaa kwa kuwafundisha umuhimu wa Kulinda na kuthamini mali za umma.

Siku hizi kila idara watu ni waoga wa kutaja neno haki na uzalendo.

Yaani mwalimu alitaja uzalendo anaonekana ni mpinzani /Chadema hivyo ni rahisi kushughulikiwa maana walimu wengi wamekua machawa hasa wale wenye elimu kubwa zaidi . Yaani kama ni shule ya msingi akishapata kadiploma au kadigrii anageuka kuwa Chawa ili mambo yake yaende.
Mwalimu akichaguliwa kuwa Mjumbe wa CWT anageuka kuwa Kada ili akila pesa za chama cha walimu asiguswe na ukihoji sana wanakuchongea wewe ni Chadema.
Hali kadhali ndani ya Polisi na vyombo vingine vyote vya Dola mpaka mahakama . Ukizungumzia haki na uzalendo unaitwa mpinzani . Yaani CCM haipo tena kwa ajili ya kusimamia sheria na haki katika nchi hii .
CCM imetekwa na genge la wahalifu wenye silaha kama basi linavyoweza kutekwa na majambazi .
Basi lilitekwa na majambazi hata wakisema vua nguo mbele ya mama mkwe na baba mkwe inabidi uvue na ukikataa wanakuua . CCM imetekwa na genge la mafisadi wachache ambao wanalindana na wanashindana kujilimbikizia mali . Yaani kuna familia sasa zinashindana kujilimbikizia mali kupitia fedha za umma . Na hao sasa wanamtumia De.Samia kama mlinzi wao kwa sababu ana majeshi nyuma yake na mahakama inaogopa kutoa haki maana ukizungumzia haki basi wewe ni Chadema .

Ndio maana leo wakristo wote wanaonekana ni Chadema kwa sababu wito mkubwa wa ukristo ni kutenda haki na kuwa na kiasi , Kutoa kodi kwa haki , kupenda wengine kama nafsi yako ,kuwatendea wengine kile ambacho wewe unakipenda utendewe na kufurahia uhuru ndani ya Kristo . Sasa Maaskofu na wachungaji wa kweli wanaonekana ni Chadema kwa sababu wanhubiri injili inayozungumzia Haki . Waislam wale wenye jitihada zao binafsi za kujitafutia riziki na uwezo wa kupambanua mambo na kusimama kwenye Ukweli uliopo ndani ya Quran na hadithi za mtume nao pia wamekua wakipigwa vita na hata kuawa kama Ally Kibao kwa sababu tu wanasema Ukweli kuwa Uislama kwa karne nyingi ulipigania Haki ya waarabu mpaka wakajikomboa . Lakini kinachotokea ni CCM kutekwa na matajiri waotoa rushwa na mapesa mengi kwenye nyumba za ibada na kujenga nyumba za ibada.
Mbaya zaidi ni kutafsiri vibaya sadaka zinazotolewa na fedha chafu kuwa zinafuta dhambi zote .
Kama ni kweli kuwa sadaka zinafuta dhambi zote basi tuseme chini ya CCM Tanzania inaangamia kwa kasi kubwa sana.

Magaidi hua wanatengenezwa na genge la matajiri ndani ya mifumo . Haya tuliyaona awamu ya Nne wakati JK anakaribia kumaliza Muda wake . Ugaidi ulipamba Moto mpaka Jeshi la Wananchi kushirikiana na vikosi maalum vya polisi vikaingilia kuwasaka baada ya Magufuli kuingia . Ina maana kuwa kama JPM angezubaa nchi ingegawanyika na isibgetawalika wakati huo huo kuna watu walikua wanapewa matrilon ya pesa toka Uarabuni kwa sababu ya kuivuruga nchi ndio maana JPM alizuia pesa zote kutoka nje ili magaidi wakose wadhamini na misaada . Majeshi yetu chini ya Mzalendo Magufuli wakafanikiwa kuwaondoa magaidi mengine yakakimbilia Msumbiji. Genge lao liliojaribu kuingiza nchi kwenye ugaidi wengi wapo sasa na wameinua mikia juu kwa furaha kuu. Vyombo vya dola vikiichekea hii CCM isiyotaka uchaguzi wa kura vitakuja kupata kazi kubwa sana huko mbeleni kwa sababu CCM haijali tena ustawi wa nchi zaidi ya kujichotea mali za umma .

Jeshi na polisi wamekaa kimya Bandari zinauzwa kwa Watu ambao kwa historia waliwahi kugawana rasilimali zetu kwa damu za watu na kuzifanya kuwa zao kwa ajili ya kujitajirisha.

Kama karne kumi na mbili zilizopita waarabu waliwaza kuja kuchukua Pembe za ndovu na dhahabu na mbao Tanganyika leo karne ya ishiri na moja unategemea lile wazo limepotea ?

Bila shaka waarabu hawakuondoka Tanganyika kwa kupenda bali waliondoka baada ya uhuru . Mbaya zaidi wana ndugu wengi humu wanaotumika sasa kuhujumu nchi.

Hata kwenye mitandoa kuna wahuni wengi na machawa wengi wenye asili ya kigeni kazi yao ni kujenga chuki na kutukana watu matusi makubwa sana . Wanamtulaka mpaka baba wa Taifa aliyeanzisha Jeshi la wananchi wa Tanzania kwa heshima kubwa . Aliyeanzisha Usalama wa Taifa kwa heshima kubwa . Aliyelinda rasilimali za nchi hii kwa ajili ya vizazi vyetu kwa heshima kubwa . Leo wametokea wahuni wanamtukana Nyerere ,wanawatukana maaskofu , wanawatukana Wanaharakati na kuwatukana watu wote wanaozungumzia habari ya haki ,uhuru,utu,umoja na mshikamano wetu uliokuwepo ,uzalendo na ulinzi wa rasilimali zetu.
Chaa ajabu hao wahuni hawakamatwi bali anayakamatwa na kunyanyaswa ni Dr. Slaa .
Unaachia magaidi yaliyochoma moto makanisa Zanzibar na kuua mapadri na kuwamwagia tindikali halafu unamfunga Padri Slaa anayeonya kuhusu ufisadi unaofanywa na wahuni kwenye nchi yetu . Inawezekana yale magaidi ndiyo yamegeuka kuwa machawa mitandoani .
Umeandika mengi ya ukweli lakini tukiacha yote kumbuka nidhamu hainunuliwi hao hao waalimu wanaofundisha masomo tu bila nidhamu ndio hao hao wanaoiba mpaka lunchbox za watoto wakija nazo shuleni huu ni ukweli kwa mujibu wa wanafunzi
Waalimu walikuwa wanawalimisha watoto mashamba yao kwa lazima na matokeo yake watoto wanaenda kuiba mahindi kumkomoq mwalimu
Nakumbuka kuna shule wanafunzi walisubiri yakauke wakapiga kiberiti
Unafundisha chuki shuleni kwa kuwapa shughuli kwa manufaa ya mwalimu mkuu

Nyerere alisaidia nchi sana na kulikuwa na nidhamu wakati huo kwani mimi nilizaliwa kabla ya Uhuru hivyo ninajua mengi pia
Watu wameuwa viwanda kwa sababu hakuwa na watu wema na hata kifo cha Sokoine wengi walifurahia sana
Hayo yalipita
Leo hata aje dictator lakini kama baraza la mawaziri au wakurugenzi hawaendi kwa kasi anayoitaka Rais itakuwa ni kazi bure naakibaki peke yake nae anaacha mambo yaende mnavyotaka kwa kuogopa atauwawa
Hata Lissu Leo akiwa kiongozi wa Taifa na atapinga rushwa na wizi wa mali ya umma bila timu kama yeye atakuwa anatwanga maji tu
Fikiria kulikuwa na watu wenye Dini tena wenye heshima kwa jamii lakini mzee Ruge aliwamwagia mabilioni na wao bila aibu wakazipokea tena alionyesha udini kabisa lakini ilikuwa ni aibu kubwa kwa Makanisa na serikali pia
Kulikuwa na watu wanatamba na kusema hivyo vijisenti
Kauli za hivyo tumezisikia sana kwa sababu watu wanathamini hela zaidi kuliko dini wala utu
Sijui JKT huwa wanafundishwa nini maana vijana wakitoka huko wanakuambia tulikuwa tunaimbishwa usiku mzima huku tukiwa tumekaa chini nje
Sasa nyimbo ndio nidhamu je zinazuia wizi?
Bila kuwa wazalendo wa haki hamtafika popote
 
Umeandika mengi ya ukweli lakini tukiacha yote kumbuka nidhamu hainunuliwi hao hao waalimu wanaofundisha masomo tu bila nidhamu ndio hao hao wanaoiba mpaka lunchbox za watoto wakija nazo shuleni huu ni ukweli kwa mujibu wa wanafunzi
Waalimu walikuwa wanawalimisha watoto mashamba yao kwa lazima na matokeo yake watoto wanaenda kuiba mahindi kumkomoq mwalimu
Nakumbuka kuna shule wanafunzi walisubiri yakauke wakapiga kiberiti
Unafundisha chuki shuleni kwa kuwapa shughuli kwa manufaa ya mwalimu mkuu

Nyerere alisaidia nchi sana na kulikuwa na nidhamu wakati huo kwani mimi nilizaliwa kabla ya Uhuru hivyo ninajua mengi pia
Watu wameuwa viwanda kwa sababu hakuwa na watu wema na hata kifo cha Sokoine wengi walifurahia sana
Hayo yalipita
Leo hata aje dictator lakini kama baraza la mawaziri au wakurugenzi hawaendi kwa kasi anayoitaka Rais itakuwa ni kazi bure naakibaki peke yake nae anaacha mambo yaende mnavyotaka kwa kuogopa atauwawa
Hata Lissu Leo akiwa kiongozi wa Taifa na atapinga rushwa na wizi wa mali ya umma bila timu kama yeye atakuwa anatwanga maji tu
Fikiria kulikuwa na watu wenye Dini tena wenye heshima kwa jamii lakini mzee Ruge aliwamwagia mabilioni na wao bila aibu wakazipokea tena alionyesha udini kabisa lakini ilikuwa ni aibu kubwa kwa Makanisa na serikali pia
Kulikuwa na watu wanatamba na kusema hivyo vijisenti
Kauli za hivyo tumezisikia sana kwa sababu watu wanathamini hela zaidi kuliko dini wala utu
Sijui JKT huwa wanafundishwa nini maana vijana wakitoka huko wanakuambia tulikuwa tunaimbishwa usiku mzima huku tukiwa tumekaa chini nje
Sasa nyimbo ndio nidhamu je zinazuia wizi?
Bila kuwa wazalendo wa haki hamtafika popote
Nanukuu:
"Sijui JKT huwa wanafundishwa nini maana vijana wakitoka huko wanakuambia tulikuwa tunaimbishwa usiku mzima huku tukiwa tumekaa chini nje
Sasa nyimbo ndio nidhamu je zinazuia wizi?"
Ukweli ni kwamba JKT ipo-ipo tu Serikali imeshindwa kuifuta au wamekosa namna au kipengele cha kuitupilia mbali kwani ipo ki-Katiba. JKT ya miezi 3 !!!??? Ndo mana vijana wanasema ukweli: "Tulikuwa tunaimbishwa usiku mzima......."
Lengo la kuanzishwa mafunzo ya JKT halizingatiwi tena.
 
Umeandika mengi ya ukweli lakini tukiacha yote kumbuka nidhamu hainunuliwi hao hao waalimu wanaofundisha masomo tu bila nidhamu ndio hao hao wanaoiba mpaka lunchbox za watoto wakija nazo shuleni huu ni ukweli kwa mujibu wa wanafunzi
Waalimu walikuwa wanawalimisha watoto mashamba yao kwa lazima na matokeo yake watoto wanaenda kuiba mahindi kumkomoq mwalimu
Nakumbuka kuna shule wanafunzi walisubiri yakauke wakapiga kiberiti
Unafundisha chuki shuleni kwa kuwapa shughuli kwa manufaa ya mwalimu mkuu

Nyerere alisaidia nchi sana na kulikuwa na nidhamu wakati huo kwani mimi nilizaliwa kabla ya Uhuru hivyo ninajua mengi pia
Watu wameuwa viwanda kwa sababu hakuwa na watu wema na hata kifo cha Sokoine wengi walifurahia sana
Hayo yalipita
Leo hata aje dictator lakini kama baraza la mawaziri au wakurugenzi hawaendi kwa kasi anayoitaka Rais itakuwa ni kazi bure naakibaki peke yake nae anaacha mambo yaende mnavyotaka kwa kuogopa atauwawa
Hata Lissu Leo akiwa kiongozi wa Taifa na atapinga rushwa na wizi wa mali ya umma bila timu kama yeye atakuwa anatwanga maji tu
Fikiria kulikuwa na watu wenye Dini tena wenye heshima kwa jamii lakini mzee Ruge aliwamwagia mabilioni na wao bila aibu wakazipokea tena alionyesha udini kabisa lakini ilikuwa ni aibu kubwa kwa Makanisa na serikali pia
Kulikuwa na watu wanatamba na kusema hivyo vijisenti
Kauli za hivyo tumezisikia sana kwa sababu watu wanathamini hela zaidi kuliko dini wala utu
Sijui JKT huwa wanafundishwa nini maana vijana wakitoka huko wanakuambia tulikuwa tunaimbishwa usiku mzima huku tukiwa tumekaa chini nje
Sasa nyimbo ndio nidhamu je zinazuia wizi?
Bila kuwa wazalendo wa haki hamtafika popote

Ni kweli lakini Mtu mweusi ni muoga sana .
Ndio maana tulitawaliwa kirahisi sana na hata leo tunataaliwa na watu mafisadi kwa kutumia vyombo vya dola kwa sababu ya woga .

Akija Rais kama Tundu Lisu hali itabadilika sana kwa sababu ya kubadili mifumo .
Katiba itabadilika.

Katiba ikibadilika italeta Uhuru wa mahakama .
Uhuru wa kujieleza
Uhuru wa vyombo vya habari .
Uhuru wa Bunge .
Tume huru ya uchaguzi
Tume huru ya maadili .
Taasisi yenye meno ya kupambana na Rushwa .
Jeshi huru la Polisi lenye uwezo wa kumkamata mtu yeyote aliyetenda uhalifu bila kujali chama chake .

Leo hii Taasisi ya rushwa inaamrishwa na mafisadi .
Polisi inapewa amri na watoa rushwa wakubwa , wezi wa mali za umma na wezi wa kura .
Unakumbuka wakati fulani Chalamila akitaka kuliamrusha jeshi la Wananchi likafanya usafi Kariakoo lakini hawakuonyesha kuitikia huo wito kutokana na ukweli kuwa sauti ya Wakati wa JPM na Makonda ilikua inapata kibali kwa Mungu na wanadamu katika suala zima la uzalendo .

Nyerere alipamba sana na rushwa lakini alisahau suala la katiba kuwa nguvu ilikua kwake peke yake lakini tasisi nyingene za kuzuia rushwa zilikua dhaifu .
Tume ya maadili imekua ni tume ya kusafisha madili ya watu . Haina meno wala mikono .
Lakini Ikija serikali yenye nia ya dhati na bunge lililochaguliwa na wananchi basi kulomesha ufisadi ni rahisi sana .
Sheria tu ya kutaifisha mali zinazoatikana kinyume na kipato cha mtu na sio mfanya biashara .

Hapa unaunda tume yenye meno inayokagua mali zote za watumishi wa umma na pia unatunga sheria ya kutaifisha mali kwa mtu yeyote atakayebainika kubwa anakwepa kodi . Kuondoa kabisa misamaha yote ya kodi kwa kila idara . Hapa unapunguza kodi na sio kusamehe kodi. Masamaha wa kodi ni ufisadi unaoumiza watu wa chini.

Taasisi za dini zilio kodi ndogo na sio kusamehewa maana ile ni michango na sadaka za wananchi au waumini hivyo kuondoa kodi ni kuwaumiza waumini hao hao maana watakamuliwa katika shughuli na kazi zao kufidia misamaha ambayo wakati mwingine haina manufaa kwa jamii zaidi ya kulipia tena gharama ya huduma hizo hizo .

Yaani Kanisa mfano linajenga hoteli halafu linataka msamaha wa kodi ,wakati hoteli hiyo haitoi huduma bure . Sasa kwa nini ipate msamaha wa kodi .? Je ,hicho sio kichaka cha watu kupiga madili yao ?

Kwanza unatenganisha uwaziri na ubunge halafu unatoa nafasi za uwaziri na ukurugenzi na teuzi zote kwenye tangazo wati watume maombi na waandike kama watalifanyia nini wizara na kipi wanaona hakiendi sawa na watakirekebishaje ?

Yaani haya mambo ya CCM unamteua tu makamu wa Rais au Waziri Mkuu wao waziri au Mkurugenzi au mkuu wa idara bila kujua anachowaza kichwani ni tatizo kubwa sana ndio maana wanaona kama ni fursa ya kupiga pesa na kumsifia aliyewapa ulaji.

Lakini kama unautaka uwaziri let say wa Viwanda ni lazima uniandikie andiko la namna utakavyoweza kutimiza huo mpango wa serikali maana hatuwezi kuweka waziri wa viwanda bila kuwa na dira imara ya kujenga viwanda . Utaniambia kuwa utafanya mabadliko na mwelekeo mkubwa wa viwanda vikubwa na vidogo katika muda wa miaka mingapi na utahitaji nini na nini kutimiza malengo ya serikali . Na ukishindwa basi ujue ndio mwesho wako wa kupata uteuzi katika nchi hizo.Lakini leo huo mtu anaharibu wizara hii kesho anapelekwa ile na kesho kutwa ile yaani ni kakikundi kwa watu kanazinguka kutafuna mali za umma bila kujali maana anayewateua anawalinda.
Mwenye mawazo mazuri ndiye atateuliwa kuwa waziri.

Mafano Wasira aliwahi kutuhumiwa kwa Rushwa kwenye uchaguzi leo atateuliwa ili kusimamia Rushwa zinazotolewa maana ana uzoefu . Sasa lini rushwa itaisha kama tuliowaamini ndio wanaotoa rushwa baada ya kuipokea wa matajiri wakubwa wa nje

Mtu anatoa gesi na mitungi yake bure lakini hawazi kabisa kuwa bei ya gesi iko juu ipungue iuzwe hata elfu 15 mtungi mdogo badala ya kutoa rushwa ya kupata uongozi
 
Back
Top Bottom