Kwanini wachezaji wa Mbao Fc wamepata soko kubwa?

Kwanini wachezaji wa Mbao Fc wamepata soko kubwa?

Truth Matters

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2013
Posts
2,302
Reaction score
4,603
Wachezaji wa timu ya Mbao FC wanaonekaba kugombewa na timu kubwa za Bongo hali ya kuwa hawa kufanya vizuri kwenye ligi nusura waishushe ligi timu yao..? Ni kweli wana kiwango au ni upepo na ulimbukeni tuu.?
 
Na ndio maana mpira wa bongo itakuwa kazi kukua. Timu ikifanya vizuri msimu ukiisha wachezaji wote wanaenda kwenye Vilabu vinavyoitwa vikongwe nchini.

Mi ni mpenzi wa moja ya hivi vilabu vya kariakoo lakini hii tabia ya Simba na Yanga kuhodhi mpira na nchi hii sidhani kama itatupeleka popote.
 
Wengi umri mdogo na wameonyesha kiwango kizuri, wana nafasi zaidi ya vipaji vyao kukua.
 
Wachezaji wa timu ya Mbao FC wanaonekaba kugombewa na timu kubwa za Bongo hali ya kuwa hawa kufanya vizuri kwenye ligi nusura waishushe ligi timu yao..? Ni kweli wana kiwango au ni upepo na ulimbukeni tuu.?
Mbona kawaida tu! Kipa wa Sunderland ya England aliwindwa na vilabu vingi vikubwa kabla hajasain Everton lakin alikuwa miongoni mwa walioishusha timu yao daraja! Hayo ni mambo ya kawaida kwani timu kufanya vibaya kuna mambo mengi yanayochangia!
 
Hakuna kitu pale ni ulimbukeni wa viongozi wa soka la kibongo
 
Wachezaji wa timu ya Mbao FC wanaonekaba kugombewa na timu kubwa za Bongo hali ya kuwa hawa kufanya vizuri kwenye ligi nusura waishushe ligi timu yao..? Ni kweli wana kiwango au ni upepo na ulimbukeni tuu.?
Hili liwe fundisho kwa wachezaji wengine wa vilabu vidogo. Mkiwakazia Yanga na Simba mnajitengenezea nafasi kwenda mbele. Msikubali rushwa na kutumika kama daraja za vilabu vingine kujipatia point tatu.
 
Back
Top Bottom