Kwanini wanakomalia laini kukatwa kodi?

Kwanini wanakomalia laini kukatwa kodi?

OLS

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2019
Posts
426
Reaction score
685
Mara ya kwanza mbunge wa Gairo alishauri laini zitozwe TSh 200 kila mwezi. Na sasa huyu mwingine ameshauri laini itozwe Tsh 50. Kwanini wanaona ni muhimu kutoza laini za simu? Ni rahisi lakini je kitendo hiki ni halali kwa watanzania ambao wanahangaika kumiliki simu nk. Je hatuoni kuwa zitaongeza mgawanyo wa kidigitali?

Ninachokiona kwa ushauri wa kutoza kodi laini za simu ni kusema tumeshindwa kuona namna sahihi ya kupata kodi kwenye maeneo ambayo yanafedha nyingi na kuja kuwakamua raia kwenye huduma hii muhimu. Mawasiliano ni jambo muhimu na la haki ambalo linatakiwa lipatikane kwa gharama nafuu, haya maneno ya mara kwa mara ya kutaka kutoza kodi yatawanyima watu haki ya kuwasiliana kwa hawa watanzania ambao anakaa mwezi hajaweka salio zaidi ya kubipu tu ili apigiwe.

Kwasasa watu wengi wamekuwa wakishare video ya Magufuli akiwalaumu TRA kuwa wanakosa ubunifu wa kukusanya kodi. Nadhani ni kweli, na tunapoendea kuna uwezekano mkubwa wa watu wasio na fedha kulipa kodi kubwa huku wanaotakiwa kulipa kodi za kuinua nchi wakaachwa wanainjoi maisha yao.

Nitoe wito kwa TRA, Wizara ya fedha nk, hebu itisheni papers halafu muone mawazo makali ya ukusanyaji kodi mtakayoyapata kutoka kwa wadau badala ya kukimbilia kutoza kodi kwenye laini.

Wito wangu kwenu ni kuwa, kwa wakati huu inabidi tuitumie digitali kupata kodi, sio kuitoza kodi digitali.

Nawasilisha

PIA SOMA
- Mbunge Santiel Kirumba: Kila laini ikatwe Tsh. 50 tujenge barabara
 
Unatoza vipi kodi katika laini wakati mwenye laini akinunua vocha,akituma pesa,akitoa kote huku serikali inabeba kodi yao.

Lakini pia laini ni mali ya kampuni ndio maana wakiamua kuifunga wanaifunga pale utakapowakosea jambo.

Hayo makampuni yanalipa kodi haipaswi mwanachi nae alipe.

Kumkandamiza mwanachi nae ailipie kila mwezi huu ni wizi usiopaswa kuvumilika.

Tumezikubali tozo ili zisaidie nchi lakini nazo zinaonekana hazitoshi.

Mbona yapo mengi tu yakusaidia mapato yaongeze.Wafute posho zao wanazojilipa mabilioni maana hazina ulazima.
 
Ukiona ivo ujue wataiweka wao wanapiga mahesabu za lain ziko ngapi. wanazidisha kwa hela wakiona ni hela nzr wanaweka.
 
Mimi nataka serikali itoze kodi kila vocha 50 na line ya simu 50 jumla 100, lakini waje na uwekezaji wa viwanda na ajira kwa vijana. Bila ya kodi hakuna maendeleo
 
Huku ni ukosefu wa ubunifu wa Wizara ya fedha Pamoja na TRA ambacho kinasimamia ukusanyaji wa mapato ya Nchi.

Kukosekana ubunifu wa kitaaluma ndiko kumemfanya waziri wa fedha kuanza kutangatanga kubuni mbinu kandamizi kwa WANANCHI walala hoi.

Hebu fikiria mfano huu mdogo tu hapa,Mwananchi huyo umemuwekea tozo kwenye miamala ya M-PESA, HALOPESA, AIRTEL Money, TIGO Pesa n.k.Bado anapoweka luku tozo ya pango la nyumba toka Elfu moja kwa mwezi mpaka elfu moja na miatano.
Leo KUPITIA laini za simu hizohizo ambazo zinautitiri wa tozo za SERIKALI,Mwananchi huyohuyo unataka umpe mzigo mwingine kwa kumuongezea tozo nyingine ya kumkata kila mwezi. Huu waziri siyo ubunifu,bali ni ukandamizaji.
 
Unatoza vipi kodi katika laini wakati mwenye laini akinunua vocha,akituma pesa,akitoa kote huku serikali inabeba kodi yao.

Lakini pia laini ni mali ya kampuni ndio maana wakiamua kuifunga wanaifunga pale utakapowakosea jambo.

Hayo makampuni yanalipa kodi haipaswi mwanachi nae alipe.

Kumkandamiza mwanachi nae ailipie kila mwezi huu ni wizi usiopaswa kuvumilika.

Tumezikubali tozo ili zisaidie nchi lakini nazo zinaonekana hazitoshi.

Mbona yapo mengi tu yakusaidia mapato yaongeze.Wafute posho zao wanazojilipa mabilioni maana hazina ulazima.
Unamjua mtu aliyeshiba mkuu... Huwa haelewi kabisa kuwa Kuna njaa. Ndio hawa Wabunge wetu sasa
 
Nchi tumewakabidhi wanyonyaji, empty set kichwani, majizi. Hawawezi kufikiri nje ya box.

Watanzania tunapenda kulipa kodi shida wanazitumia hovyo, mtu anabeba wasanii karibia 20 anaenda kuomba mkopo wa bilioni kadhaa, UPUUZI mtupu.
 
Unamjua mtu aliyeshiba mkuu... Huwa haelewi kabisa kuwa Kuna njaa. Ndio hawa Wabunge wetu sasa
Hawa wabunge wetu wamezidi sana dharau kwasababu wanalipwa pesa nyingi ambazo hawajazifanyia kazi ya maana.

Hakuna mtu mwenye akili timamu anaeweza kuleta hoja za kumnyonya mwanachi.

Tuna mabilioni mengi sana yanatumika kulipa watu posho huku walimu na taaluma zingine hawawapi mapesa mengi kama wanayojilipa wao.

Ni muda sasa wajipunguzie posho na mishahara yao ili waone uhalisia wa maisha.
 
Wakiweka hiyo, mimi nina laini 3, nitavunja mbili na kubakiza moja, kwa hiyo target yao itafeli na laini zitapungua
 
Uhalali wa kuwakilisha wananchi kigezo cha elimu kingehusika, haiwezekan kigezo mpaka Leo hii iwe std7 uingie bungeni kuwakilisha shahada na maPHD's...... Nchi ina bahari kubwa na misitu serikali haiwazi kiwekeza huko bali kila uchwao mwanachi no chanzo cha mapato.... Tuoneeni huruma jamanii 😭😭😭😭😭😭😭😭😭
 
Si halali laini ikatwe kodi kwa Mwananchi. Mana mwananchi huyo Ununua hiyo laini kwa Kampuni husika. Ni haki kampuni ndio zikatwe Kodi na sio kila Laini ya Mtanzania ikatwe sio kweli nasio haki katika hali ya kiuchumi..

Na kufanya Hivyo ni Kudhurumu haki za kiuchumi kwa Mmiliki wa simu. Mana wakiweka Kodi leo itakuja baadae itapanda itakua ni faida kwa serikali na nihasara kwa Mtanzania alihiyo ni unyonyasaji...
 
Mimi ninaona kama Taifa na bara kwa ujumla bado tunasafari ndefu sana katika swala zima la kupiga hatua kutoka hapa tulipo kuingia japo hata kwenye njia ya kwenda kule tunapopatazamia ,,
Tofauti na hilo wanaloliongelea kuna mambo mengi sana ambayo yangefanyika na kuokoa baadhi ya gharama na pengine kuleta pesa nyingi kwa muda Fulani kama ifuatavyo :

1. Katika kipindi nilichotembea baadhi ya mikoa hapa Tanzania kwa mihangaiko ya maisha , nimekuta mabango ya kutoa heko kwa raisi juu ya ufanyaji kazi , mabango ambayo kwanza yatatengenzwa kwa gharama kubwa na pia yasingekuwepo ingeleta fursa ya mengine ya kibiashara kuwekwa na watu binafsi na kuleta ushuru.. RAISI KAMA KALETA MAJI MIMI NITAJUA ,KAMA KALETA UMEME NITAONA TU , SASA NINAUMIA SANA NINAPOONA MARKETING STRATEGIES ZINATUMIKA KWENYE SIASA TENA YA URAIS.

2. Sijui kama nakosea lakini , binafsi naona kama taifa tunatumia gharama kubwa sana zisizo za msingi kwa viongozi, ambayo yamkini ikawa sawa lakini haiendani na Pato letu , haiwezekani sisi na baadhi ya mataifa yaliyoendelea tuwe tofauti afu eti viongozi wetu waishi kama kule hatuwezi endelea hata kidogo , Kuna waziri mmoja aliyetenguliwa alisema hawezi kutembelea gari ya kawaida kwenye ziara ataumiza mgongo na kiuno , huku soko la mabibo jijini dar es salaam Kuna watu kutwa kuchwa wanabeba magunia na bado maisha yanaenda,, sijamaanisha kumlazimisha waziri aishi kwa kujibana kwa sababu ya nchi lakini mantinki yangu ni kwamba kama hawezi kufanya kazi kwa maslahi madogo yanayoendana na uwezo wa nchi aache watu wapo watafanya kazi bila lawama na mambo yataenda ,, HIVYO MASLAHI TUNAYOTOA KWA VIONGOZI YAPUNGUZWE YAPELEKWE KWENYE MAMBO YA MSINGI.

3. Wananchi tumekuwa vipofu pia katika kukemea uovu wa viongozi, na hata wanaoona wameshakata tamaa wakidai kuwa watafanya nini sasa ,
Kwa mantinki hiyo viongozi hawatoacha kutujeruhi sisi na pia kutengeneza hatari kwa Tanzania ya baadae.. Watanzania wenzangu, tuamke tufuatilie mwenendo wa nchi , kwa umoja wetu tukemee maovu ya viongozi, lakini tusiweke uadui na tutumie hekima kana kwamba kiongozi akifanya vizuri tuone na vibaya pia tuone pia , sio Ile mwana CCM haoni mabaya na mpinzani kamwe haoni mazuri kitu hii pia inatuumiza sana japo siwezi elezea hapa ..

Ningependa kuandika mengi sana lakini naomba niishie hapa ,,ISHI SANA TANZANIA, ISHI SANA AFRIKA.💪💪💪
 
Back
Top Bottom