KWANINI waraka wa Dr. Kitila na wenzie siyo uhaini na Chadema inazikwepa hoja za kimsingi

KWANINI waraka wa Dr. Kitila na wenzie siyo uhaini na Chadema inazikwepa hoja za kimsingi

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
219,468
Reaction score
911,184
Tuhuma za uhaini zinahitaji tafsiri sahihi ya msamiati wa "uhaini" kabla haujatumika kuadhibu wale ambao Chadema au kikundi chochote kile ambacho kinatofautiana na watuhumiwa husika. Uhaini ni kufanya mipango ya siri ya kuleta mageuzi ambayo yanapingana na utaratibu uliopo wa kuleta mageuzi ndani ya taasisi au nchi yoyote ile.

Tukiangalia waraka wa Dr. Kitilya akiwa mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema waraka wake aliutoa ndani ya Kamati Kuu ya Chadema ili ujadiliwe hivyo haukuwa siri na hauwezi ukaitwa ni uhaini. Pili Kamati Kuu ya Chadema ilikuwa na uwezo wa kuukubali au kuukataa bila ya kuathiri masilahi ya mjumbe wa Kamati Kuu ambaye alikuwa amewapa changamoto.

NIONAVYO MIMI:-


BAADHI YA KHOJA ZA MSINGI AMBAZO CHADEMA NI LAZIMA IZITOLEE MAJAWABU ni hizi zifuatazo:-

1) Marekebisho ya Katiba ya Chadema kwenye nyanja hizi hayakwepeki.

a) Kura za maoni za wanachama zitumike kuteua viongozi wa ngazi zote wanaogombea nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama au serikalini badala ya kutegemea vikao vya wachache ambavyo siyo shirikishi na demokrasia yake ni kiduchu kabisa.

b) Viongozi wataondolewa madarakani kwa vikao vilivyowateua badala ya Kamati Kuu ambayo siyo chombo cha uteuzi. Kamati Kuu hujivika gamba la kuwanyang'anya nyadhifa viongozi wasiowapenda wakati wao hawakushiriki katika kuwachagua na kwa kufanya hivyo misingi ya kidemokrasia inakuwa imekiukwa kabisa.


c) Watendaji ndani ya chama wawe ni wataalamu wakiajiriwa kushika nafasi hizo kwa vipindi visivyozidi miaka mitano.

d) Wanasiasa wasishikilie nafasi za kiutendaji ili kutofautisha nafasi za kisiasa na kiutendaji kwa malengo ya kuboresha tija ya uwajibikaji.


e) Asiwepo kiongozi mwenye kofia mbili ndani ya chama ili kutoa mwanya wa kupanua wigo la ushiriki wa wanachama wengi zaidi katika nafasi ya kukiongoza chama chao.

f) Taarifa za mapato na matumizi ya chama zijadiliwe, kuhakikiwa na kupitishwa pia na vikao vya chama kuanzia kata badala ya sasa kuwa ni hodhi ya wakubwa wachache katika kamati Kuu ya chama.

2) Kuvumiliana ndiyo ukomavu wa kisiasa.


Maoni waliotoa akina Dr. Kitilya ni changamoto ambazo zilipaswa zipelekwe ndani ya vikao vyote vya chama kuanzia kata ili vijadiliwe na maoni yapatikane ya kuboresha utendaji wa chama badala ya Kamati Kuu kukimbilia kwenye vyombo vya khabari na kuutusi kuwa waraka ule ulikuwa ni uhaini!


3) Hakuna ambaye ni mkamilifu.


Inashangaza sana kuona wale ambao wanatuhumiwa kwa wizi na ubadhirifu wa mali za chama ikiwemo kujilimbikizia mali wanakua mstari wa mbele kuwanyoshea kidole wale ambao wanawakosoa kuwa ni wezi wa mali ya umma!

4) Misingi ya haki na ya kidemokrasia ndiyo itawaimarisha siyo kuwadhoofisha



Ipo dhana potofu ndani ya Chadema kuwa kupanua wigo la demokrasia kutakaribisha mahasimu wao wa CCM kuitumia kuwavurugia na hivyo kuwadhoofisha na hivyo kujenga utaratibu wa vikao vya juu kuwa na hadhi ya "wenye chama"!
Khali hii kamwe haitakiimarisha Chama bali kukidhoofisha kwa sababu wanachama wa kawaida huwezi tu kwenye majukwaa ukawasifia kuwa nguvu iko kwao yaani "PEOPLE'S POWER" wakati huwashirikishi kwenye maamuzi ya kukiendesha chama chao hususani ya kuteua, kudhibiti na kuwaasa viongozi wao ambao waliwachagua wao wenyewe.
 
................Tukiangalia waraka wa Dr. Kitilya akiwa mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema waraka wake aliutoa ndani ya Kamati Kuu ya Chadema ili ujadiliwe hivyo haukuwa siri na hauwezi ukaitwa ni uhaini. Pili Kamati Kuu ya Chadema ilikuwa na uwezo wa kuukubali au kuukataa bila ya kuathiri masilahi ya mjumbe wa Kamati Kuu ambaye alikuwa amewapa changamoto..............
mkuu nina mashaka makubwa na hii taarifa, kwa uelewa wangu ule waraka haukuletwa kwa hiari mbele ya kamati kuu ili ujadiliwe, na zaidi ule waraka unajieleza kabisa kuwa ni waraka wa siri kubwa na unajulikana kwa watu wane tu yaani MM, M1, M2 na M3,
 
Nadhani kosa kubwa ambao wachambuzi wa sakata hili wanalifanya ni kuassume kwamba viongozi wajuu wa Chadema wana good intention.

Kutokana na kufanya kosa hili, wachambuzi wengi wamekuwa wakitoa ushauri ambao basically unafaa, lakini hauko useful kwa sababu sio kwamba viongozi wa juu wa Chadema hawajui kitu gani ni sahihi. Wanachokosa viongozi hao ni political will ya kufanya jambo sahihi kwa sababu they dont have good intention.

Ndani ya chadema hakuna haki na usawa. Kila mtu anahukumiwa kwa msaafu watakaoamua watoa hukumu, hakuna msaafu mmoja wa hukumu. Ndio maana Slaa amefunga mjdala wa sakata hili lakini Lema ameenda jukwaani kuuendeleza. Lema hatachukuliwa hatua yoyote, ingawa ni dhahiri kuwa amekiuka maelekezo ya Katibu Mkuu.

Katika hali kama hii tunaweza kutoa ushauri kurasa milioni moja, lakini hakuna msaada tutakaoutoa zaidi ya kuweka kumbukumbu kwenye historia kwamba tulitoa ushauri.
 
mkuu nina mashaka makubwa na hii taarifa, kwa uelewa wangu ule waraka haukuletwa kwa hiari mbele ya kamati kuu ili ujadiliwe, na zaidi ule waraka unajieleza kabisa kuwa ni waraka wa siri kubwa na unajulikana kwa watu wane tu yaani MM, M1, M2 na M3,
Mkuu ni vema umelileta hilo hapa.

Mtoa hoja amekosea katika hoja yake ya kwanza kabisa aliyoitumia kujengea hoja kuwa
................Tukiangalia waraka wa Dr. Kitilya akiwa mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema waraka wake aliutoa ndani ya Kamati Kuu ya Chadema ili ujadiliwe hivyo haukuwa siri na hauwezi ukaitwa ni uhaini. Pili Kamati Kuu ya Chadema ilikuwa na uwezo wa kuukubali au kuukataa bila ya kuathiri masilahi ya mjumbe wa Kamati Kuu ambaye alikuwa amewapa changamoto..............
Ukweli ni kuwa waraka huo ulipatikana kutoka kwenye laptop ya Mwigamba baada ya uongozi kutonywa na baadhi ya walioandaa waraka huo kwa siri juu ya uwepo wa mipango hiyo ya siri siri.

Ukweli ni kwamba Kitila alikiri kuwa yeye ni mmoja wa wahusika wa kutayarisha waraka huo, na alijua kuwa alikuwa amevunja taratibu za kinidhamu, na akawa ameamua ajiuzulu mwenyewe. Hata hivyo Kamati Kuu ikamkatalia na kumvua vyeo vyake ndani ya chama.

Katiba ya Chadema toleo la 2006. Katika Kanuni za Uendeshaji Kazi za Chama. Sura ya 10, Ibara ya ix, imeandikwa:

"Kiongozi asijihusishe au kushiriki na vikundi vya kuchonganisha au kuzua migogoro ndani ya Uongozi wa Chama au Wanachama wake."

Na katika Katiba hiyo hiyo Sura ya 7 kuhusu kazi za Kamati Kuu, Ibara ya 7,

Ibara ndogo t, imeandikwa:
"Kufanya uamuzi juu ya mapendekezo ya kufukuza Mwanachama."

Na Ibara ndogo v, imeandikwa:
"Kumwachisha ujumbe wa Kamati Kuu mjumbe mteule ambaye ataenda kinyume na Katiba, Kanuni na Maadili au kushindwa kukidhi matakwa ya kuteuliwa kwake."
 
Wanachokosa viongozi hao ni political will ya kufanya jambo sahihi kwa sababu they dont have good intention.
Hiyo assumption yako haiwezi kubandikwa hapa (Great thinkers) bila ushahidi ulio wazi na usio na mashaka na ikakubalika tu kama msingi wa kujengea hoja.

Mpaka pale utakapoitolea ushahidi wa kutosha, hatuwezi kuitumia kwenye jukwaa la GREAT THINKERS, hasa ukizingatia assumption hiyo inatolewa na mtu ambaye hakubaliani na hao anaowatuhumu karibu katika kila jambo, na ameshakiri humu JAMIIFORUMS kutowapenda hao viongozi.

It is a BIASED AND WRONG ASSUMPTION mpaka ushahidi uthibitishe hivyo.
 
Hiyo assumption yako haiwezi kubandikwa hapa (Great thinkers) bila ushahidi ulio wazi na usio na mashaka na ikakubalika tu kama msingi wa kujengea hoja.

Mpaka pale utakapoitolea ushahidi wa kutosha, hatuwezi kuitumia kwenye jukwaa la GREAT THINKERS, hasa ukizingatia assumption hiyo inatolewa na mtu ambaye hakubaliani na hao anaowatuhumu karibu katika kila jambo, na ameshakiri humu JAMIIFORUMS kutowapenda hao viongozi.

It is a BIASED AND WRONG ASSUMPTION mpaka ushahidi uthibitishe hivyo.

Mkuu,

Ushahidi gani wa ziada unaotaka zaidi ya kile nilichoandika kwenye post yangu? Hivi unaamini kwamba ni too difficult question kwa Chadema kujua kuwa Lema amevunja kauli ya Katibu Mkuu hadharani na anastahili kupewa angalau onyo? Kwanini Lema haadhibiwi? Kwa sababu hakuna good intention.

Waraka wa kumchafua Zitto umesambazwa muda mrefu, Chadema haijatoa tamko lolote la kuupinga ingawa waraka huo ulisema kuwa umetoka ofisi ya makao makuu chadema. Unadhani ni too dofficult question kwa chadema kujua kuwa waraka huo haujatoka ofisini kwao? Kwanini hawajatoa kauli ya kuupinga? Hawakuwa na good intention.

Lema alipochafuliwa, Mzee Mtei mapema sana alitoa kauli ya kupinga kitendo hicho cha kishenzi. It was correct and timely. Kwanini hakufanya hivyo kwenye waraka wa kumchafua Zitto? hakukuwa na good intention.

Watu kama hawa ambao hawana good intention hata ukiwapa ushauri ni bure tu. Hawataufuata, itabaki tu kwenye historia kwamba wameshawahi kupewa ushauri sahihi.

Hivi unadhani Chadema hawajui kwamba Henry Kilewo anastahili kuadhibiwa kwa kumchafua Zitto kwenye website yake? Kwanini Henry Kilewo hajapewa hata onyo? Kwa sababu hakuna good intention. Sio kwamba hawajui nini cha kufanya, ni kwamba hawataki kufanya yaliyo sahihi.
 
Mkuu,

Ushahidi gani wa ziada unaotaka zaidi ya kile nilichoandika kwenye post yangu? Hivi unaamini kwamba ni too difficult question kwa Chadema kujua kuwa Lema amevunja kauli ya Katibu Mkuu hadharani na anastahili kupewa angalau onyo? Kwanini Lema haadhibiwi? Kwa sababu hakuna good intention.

Waraka wa kumchafua Zitto umesambazwa muda mrefu, Chadema haijatoa tamko lolote la kuupinga ingawa waraka huo ulisema kuwa umetoka ofisi ya makao makuu chadema. Unadhani ni too dofficult question kwa chadema kujua kuwa waraka huo haujatoka ofisini kwao? Kwanini hawajatoa kauli ya kuupinga? Hawakuwa na good intention.

Lema alipochafuliwa, Mzee Mtei mapema sana alitoa kauli ya kupinga kitendo hicho cha kishenzi. It was correct and timely. Kwanini hakufanya hivyo kwenye waraka wa kumchafua Zitto? hakukuwa na good intention.

Watu kama hawa ambao hawana good intention hata ukiwapa ushauri ni bure tu. Hawataufuata, itabaki tu kwenye historia kwamba wameshawahi kupewa ushauri sahihi.

Hivi unadhani Chadema hawajui kwamba Henry Kilewo anastahili kuadhibiwa kwa kumchafua Zitto kwenye website yake? Kwanini Henry Kilewo hajapewa hata onyo? Kwa sababu hakuna good intention. Sio kwamba hawajui nini cha kufanya, ni kwamba hawataki kufanya yaliyo sahihi.
Kwa hiyo wewe good intention unaipima ukimwangalia Zitto tu?

Na je Zitto mwenyewe kwa aliyokwishayafanya ndani ya CHADEMA ya kutengeneza NA KUONGOZA vikundi ambavyo vilishadhihirika mara tatu ndani ya CHADEMA vyenye malengo ya kuvuruga chama

  1. Wakati wa mgogoro wa akina KAFULILA.
  2. Mgogoro wa M7 masalia uliopelekea akina JULIANA SHONZA na MTELA MWAMPAMBA kuvuliwa uanachama
  3. Huu mgogoro wa sasa wa kutengeneza kikundi cha siri ndani ya chama
Hayo yote ni kinyume na katiba
Sura ya 10, Ibara ya ix:

"Kiongozi asijihusishe au kushiriki na vikundi vya kuchonganisha au kuzua migogoro ndani ya Uongozi wa Chama au Wanachama wake."
Huyu ndiye unashinda humu jamvini unamtetea kuwa ana nia njema wa kuvumiliwa kufanya chochote ndani ya chama?

Zitto ndiye chanzo cha migogoro hii ya sasa ya CHADEMA, na akishughulikiwa na vikao halali kwa mujibu wa katiba mnaona nongwa.

Sura ya 7 kuhusu kazi za Kamati Kuu, Ibara ya 7,
Ibara ndogo t, imeandikwa:
"Kufanya uamuzi juu ya mapendekezo ya kufukuza Mwanachama."

Na Ibara ndogo v, imeandikwa:
"Kumwachisha ujumbe wa Kamati Kuu mjumbe mteule ambaye ataenda kinyume na Katiba, Kanuni na Maadili au kushindwa kukidhi matakwa ya kuteuliwa kwake."

ZeMarcopolo kuwa mkweli, mwogope Mungu japo kidogo
 
Kwa hiyo wewe good intention unaipima ukimwangalia Zitto tu?

Na je Zitto mwenyewe kwa aliyokwishayafanya ndani ya CHADEMA ya kutengeneza NA KUONGOZA vikundi ambavyo vilishadhihirika mara tatu ndani ya CHADEMA

  1. Wakati wa mgogoro wa akina KAFULILA.
  2. Mgogoro wa M7 masalia uliopelekea akina JULIANA SHONZA na MTELA MWAMPAMBA kuvuliwa uanachama
  3. Huu mgogoro wa sasa wa kutengeneza kikundi cha siri ndani ya chama


Hayo yote ni kinyume na katiba
Huyu ndiye unashinda humu jamvini unamtetea kuwa ana nia njema wa kuvumiliwa kufanya chochote ndani ya chama?

Zitto ndiye chanzo cha migogoro hii ya sasa ya CHADEMA, na akishughulikiwa na vikao halali kwa mujibu wa katiba mnaona nongwa.

Sura ya 7 kuhusu kazi za Kamati Kuu, Ibara ya 7,
Ibara ndogo t, imeandikwa:
"Kufanya uamuzi juu ya mapendekezo ya kufukuza Mwanachama."

Na Ibara ndogo v, imeandikwa:
"Kumwachisha ujumbe wa Kamati Kuu mjumbe mteule ambaye ataenda kinyume na Katiba, Kanuni na Maadili au kushindwa kukidhi matakwa ya kuteuliwa kwake."

ZeMarcopolo kuwa mkweli, mwogope Mungu japo kidogo

Hapo sasa unachanganya mambo.

Swala la Zitto kushutumiwa halihalalishi wale wanaomchafua kuachwa bila kupewa hukumu. Vilevile haifanyi Chama kikae kimya pale unapotoka waraka unaoeleza kuwa umetoka makao makuu ya Chadema kumchafua Zitto. This is simple knowledge wala haihitaji mtu anayejiita great thinker ashauri nini cha kufanya katika mazingira haya. Kutokufanya kitu sahihi katika haya kunadhihirisha kuwa hakuna good intention. This is beyond any reasonable doubt...
 
Hapo sasa unachanganya mambo.

Swala la Zitto kushutumiwa halihalalishi wale wanaomchafua kuachwa bila kupewa hukumu. Vilevile haifanyi Chama kikae kimya pale unapotoka waraka unaoeleza kuwa umetoka makao makuu ya Chadema kumchafua Zitto. This is simple knowledge wala haihitaji mtu anayejiita great thinker ashauri nini cha kufanya katika mazingira haya. Kutokufanya kitu sahihi katika haya kunadhihirisha kuwa hakuna good intention. This is beyond any reasonable doubt...
Sioni mantiki ya ukiandikacho.

Mtu ameshadhihirika kuvuruga chama wewe bado unasema unajaribu kumlinda kwa kisingizio cha KUCHAFULIWA!!!

Zitto is not innocent kama unavyodhani, lengo lake ni kutafuta madaraka kwa namna yoyote ile hata kama ni kwa kuua chama. Tena anafanya hivyo kwa njia zilizo kinyume cha katiba ya chama, na kuna ushahidi mwingi wa kumhusisha na ninyi wana CCM. Mojawapo ni haya mapenzi makubwa uliyonayo wewe mwana CCM kwa Zitto japo huipendi CHADEMA kwa nguvu zako zote.

Let us agree to disagree.
 
Sioni mantiki ya ukiandikacho.

Let us agree to disagree.

Huwezi kuona kitu ukiwa umefumba macho.

Kabla ya kumsaidia mtu kutatua tatizo ni vyema kujiuliza je, mtu huyo ana lengo la kupata utatuzi unaofaa au utatuzi unaomfaa. Viongozi wa Chadema kwenye hili wanataka utatuzi unaowafaa sio utatuzi unaofaa.

Wanazuoni mbalimbali wanatoa utatuzi unaofaa lakini hautawasaidia Chadema kwa sababu huo sio utatuzi unaowafaa viongozi.
 
Huwezi kuona kitu ukiwa umefumba macho.

Kabla ya kumsaidia mtu kutatua tatizo ni vyema kujiuliza je, mtu huyo ana lengo la kupata utatuzi unaofaa au utatuzi unaomfaa. Viongozi wa Chadema kwenye hili wanataka utatuzi unaowafaa sio utatuzi unaofaa.

Wanazuoni mbalimbali wanatoa utatuzi unaofaa lakini hautawasaidia Chadema kwa sababu huo sio utatuzi unaowafaa viongozi.
Wewe ZeMarcopolo ninayekufahamu hujawa na nia ya kuisaidia CHADEMA hata siku moja, kwa kuwa daima unaitakia mabaya. Ila ndani ya CHADEMA yeyote anayevuruga na kuanzisha migogoro huyo ni shujaa kwako, na unamtetea ili migogoro ikue na upate unachokitamani (kusambaratika kwa chama).

Hapo hatuwezi kukubaliana hata kidogo.
 
Wewe ZeMarcopolo ninayekufahamu hujawa na nia ya kuisaidia CHADEMA hata siku moja, kwa kuwa daima unaitakia mabaya. Ila ndani ya CHADEMA yeyote anayevuruga na kuanzisha migogoro huyo ni shujaa kwako, na unamtetea ili migogoro ikue na upate unachokitamani (kusambaratika kwa chama).

Hapo hatuwezi kukubaliana hata kidogo.

Mkuu,

Haya unayoandika yako nje ya mada iliyo mbele yetu.

Nilichosema kwenye post hii ni kwamba mgogoro ndani ya Chadema usingefika hapa ulipofika iwapo viongozi wa juu wangekuwa na nia njema ya kutenda haki kwa maslahi ya chama. Nimekuonyesha mifano ya matukio kadhaa ambayo viongozi wakuu wa chama waliyafumbia macho kwa makusudi.

Viongozi wa namna hiyo hata ukiwapa ushauri gani hawatanufaika nao.
 
Mkuu,

Haya unayoandika yako nje ya mada iliyo mbele yetu.

Nilichosema kwenye post hii ni kwamba mgogoro ndani ya Chadema usingefika hapa ulipofika iwapo viongozi wa juu wangekuwa na nia njema ya kutenda haki kwa maslahi ya chama. Nimekuonyesha mifano ya matukio kadhaa ambayo viongozi wakuu wa chama waliyafumbia macho kwa makusudi.

Viongozi wa namna hiyo hata ukiwapa ushauri gani hawatanufaika nao.
Maslahi ya chama ni pamoja na kuchukulia hatua wanaodhihirika kuvuruga chama, na Zitto ameshathibitika kuvuruga chama.

Why wewe always against CHADEMA, but always for Zitto! Is Zitto an angel? Is Zitto infallible?
 
Maslahi ya chama ni pamoja na kuchukulia hatua wanaodhihirika kuvuruga chama, na Zitto ameshathibitika kuvuruga chama.

Why wewe always against CHADEMA, but always for Zitto! Is Zitto an angel? Is Zitto infallible?

Sipingi Zitto kupewa adhabu iwapo amefanya kosa. Ila ninapinga pale viongozi wanapofunga macho na masikio pale wengine kama Lema wanapofanya makosa.
Viongozi wa namna hawana nia njema...
 
Back
Top Bottom