Kwanini watahiniwa wakujitegea hufeli?

NyaniMwekundu

Member
Joined
Jul 17, 2013
Posts
22
Reaction score
5
Wapendwa poleni na majukumu ya kilasiku. Mwenzenu ninapenda kujua katika swala hili . kwanini watahiniwa wengi wa kujitegemea hawafanyi vizuri katika mitihani yao? Pili kuna tofauti zozote za usahishaji kati ya watahiniwa binafsi na watahiniwa wa shule. Tatu ni kwelikwamba umaarufu wa kituo cha mtihan ni kigezo moja wapo cha mtahiniwa binafsi kufanya vyema? Msaada wenu tafadhali
 
wanakuwa na mambo mengi wengi waoundua hilo.mi nimekaa na watu tofauti wanaorudia mitiani pia huwa wengi hawakubali makosa waliofanya mwanzo, wanaona walionewa hivo hupiga msuli kama wa mara ya kwanza na kutumia notes zilezile au kujisomea mwenyewe akiamini alishavipitia ni marudio tu,lakini ukweli ni kwamba ukikubali kosa na kutafuta wenzako wakutoe ujinga kama huo kifikra basi kazi kwisha.NOTE IT.PROVED 60%
 
Wengi huwa hawana maandalizi ya kutosha wanaamini kuwa wanapiga sasa ili kung'arisha tu ufahamu wao. Pia kuna wengine ambao wanachovuna ndio uwezo wao jamani lawama kwa wasahihishaji tuzipunguze kwasababu wao wanaongozwa na sheria wala hawana upendeleo kama wengi wanavyoamini.
Wapo watu wengi ambao wamesoma na kufanya mtihan kama private candidate na wamefanya vizuri kwakuwa wamelijiandaa vizuri na wana uwezo mzuri.
Naomba nimalizie hivi watanzania wenzangu tusing'ang'ania kufaulu mitihani wakati maandalizi hayafanani na ufaulu tunaotaka na sio lazima kila mmoja asome afike chuo kikuu wengine wana vipaji vya ufundi tuwapeleke huko sio kuwang'ang'aniza tu kurudia mitihani watazeekea kwenye vyumba vya mitihani huku mkiwachamba hawana akili au kulaumu usahihishaj, sikatai mfumo wa elimu yetu ni mbovu lkn nasi tusiwe na mawazo mabovu tubadilike.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…