Keynez
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 2,428
- 3,937
Watanzania wenzangu, mnisamehe kwa kuwaambia UKWERI huu. Nimetafakari na kufuatilia suala hili kwa muda mrefu sana na ninapokuja mbele yenu kwa 'conclusion' hii, naomba mchukue muda mjitafakari vizuri.
Tukikaa wenyewe kwa wenyewe, tunasemana kuwa "kabila fulani ni washamba!". Wengine wanasema "kabila fulani ni wabishi!". Mwingine atasema "kabila fulani ni wajuaji sana!". Ila nimewaangalia 'across the board', sisi watanzania wote tuna kiwango kikubwa cha 'sifa' hizi. Nitaepuka kutoa mifano hai ili msije mka 'dogosha' hili jambo ninaloleta mbele yenu.
Uzuri baada ya muda ushamba huwa unatoweka, ila ubaya wake ni kuwa ushamba ukishatoweka una hatari ya kufuatiwa na ujuaji. Yaani mtu anatunisha kifua kabisa wakati jana tu alikuwa mbumbumbu wa jambo lile. Yaani ukute mtu ushamba bado anao, halafu akajua kidogo, mbona utamkoma!!
Hivi hii ni hulka yetu au tukikua tutaacha?
Tukikaa wenyewe kwa wenyewe, tunasemana kuwa "kabila fulani ni washamba!". Wengine wanasema "kabila fulani ni wabishi!". Mwingine atasema "kabila fulani ni wajuaji sana!". Ila nimewaangalia 'across the board', sisi watanzania wote tuna kiwango kikubwa cha 'sifa' hizi. Nitaepuka kutoa mifano hai ili msije mka 'dogosha' hili jambo ninaloleta mbele yenu.
Uzuri baada ya muda ushamba huwa unatoweka, ila ubaya wake ni kuwa ushamba ukishatoweka una hatari ya kufuatiwa na ujuaji. Yaani mtu anatunisha kifua kabisa wakati jana tu alikuwa mbumbumbu wa jambo lile. Yaani ukute mtu ushamba bado anao, halafu akajua kidogo, mbona utamkoma!!
Hivi hii ni hulka yetu au tukikua tutaacha?