Uchaguzi 2020 Kwanini Watanzania wengi hawana furaha? Hongera CHADEMA kwa kuligundua hilo

Uchaguzi 2020 Kwanini Watanzania wengi hawana furaha? Hongera CHADEMA kwa kuligundua hilo

cutelove

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2017
Posts
3,448
Reaction score
7,972
Ukubali usikubali lakini huu ndo ukweli wenyewe kuwa hakuna kitu kigumu kwenye maisha ya binadamu kama kulipa gharama za matibabu (kuuguliwa)

Kwa kweli gharama za matibabu Tanzania zipo juu sana na mtu binafsi anatakiwa alipe kabla ya huduma au kama huna bima

Yaani ukifika hospital uwe na hela usiwe nayo lazima ulipe kwanza mapokezi ndo huduma zingine ziendelee huku ukiendelea kulipa huduma ya kulazwa na vipimo mbalimbali na madawa

Ugonjwa haukwambii siku wala muda wa kuja kwenye familia yako wala haukwambii ni aina gani ya ugonjwa unakuja

Tunacheka vijiweni, sehemu mbalimbli lakini linapokuja suala la gharama za matibabu kwa sisi wenyewe tukiwa tumeugua au tumeuguliwa hapa watanzania hujikuta na msongo wa mawazo,na watu wengi wanapata stress kwa sababu ya kuuguza

Huku hela ya matibabu hapo hapo mgonjwa ale dah! Kwa kweli sio siri lazima uwe kichaa

Kwenye ugonjwa ndo watu wanajuta kuzaliwa,hasa unayeuguza,halafu binadamu tulivyo, michango ya harusi ipo fasta lakini kwenye matibabu simu hazipatikani,

Uzalendo ni kuwapenda watu wako,Watanzania ni masikini,bima ya afya kwa kila mtu mtawaokoa Watanzania wengi na stress za maisha

Kwa nini watanzania hatuna furaha, kwa nini tuna msongo wa mawazo ni kwa sababu ya kitu hiki

Watu watakwambia bora upatwe na tatizo lingine isipokuwa kuugua au kuuguliwa ,utajuta kuzaliwa,na watu wameuza rasilimali ,watu wamefilisika kwa sababu ya matibabu ,hata Bahati Bukuku analijua hilo

CHADEMA ikazie hiyo sera ya bima ya afya kwa kila mtu,hapo mmewagusa maisha ya watu tangu akiwa tumboni hadi uzeeni,bora umnyime mtu chakula lakini siyo matibabu

Kuuguza bila bima,Lissu okoa Watanzania
 
Inatakiwa nationali insurance kama ya uingereza na nchi za Scandinavia ambapo kila mtu analipia sehem ya Bima ya afya kwenye matumizi au mapato yake. Huitaji kadi namba yako tu ya kitambulisho cha taifa,pia hiyo pesa ikiusanywa unaenda bima kweli . Inawezekana kabisa
 
Wakuu wa Wilaya,mikoa,makatibu wakuu, wakurugenzi,mawaziri, na wengine ambao ni wateule hawana amani,hawajui kesho itakuwaje, hawana Raha,wafanyabiashara ,wakulima,wafungaji ,wahitimu vyuo vikuu na wengine hawana Raha Ni huzuni tu mwaka wa tano Sasa.
 
Inatakiwa nationali insurance kama ya uingereza na nchi za Scandinavia ambapo kila mtu analipia sehem ya Bima ya afya kwenye matumizi au mapato yake. Huitaji kadi namba yako tu ya kitambulisho cha taifa,pia hiyo pesa ikiusanywa unaenda bima kweli . Inawezekana kabisa
Very good idea .
 
Hata obama care imeshindika huko USA kisa pesa seuze hapa Tanzania, chadema wasilete uongo wao .wanasema hawajazindua ilani haya wanayoahidi wanatoa wapi?


USSR
Ulikwepo leo mkutanoni?
 
Chadema ndio hamna furaha asilimia 100 mnsumwa sonona
vijana ambao tulifikiri watakuwa makini kuchambua sera za wagombea na ilani zao for the next 5 years, Ndio Hao Hao wako mitandaoni kubishana nani kajaza uwanja...Smh, Tuna safari ndefu sana fam. Tuko kishabiki zaidi dizaini ya simba na yanga!!
 
Hata obama care imeshindika huko USA kisa pesa seuze hapa Tanzania, chadema wasilete uongo wao .wanasema hawajazindua ilani haya wanayoahidi wanatoa wapi?


USSR

Ila ndege zimewezekana cyo km Tz?Akili zako ziko kwenye huo mtaro wako wa hko chini shwain Mataga
 
Jpm miaka 5 iliyopita tuliamini ataleta furaha na haki kwa watu, mbaya zaidi amezidi kuligawa taifa letu kwa misingi ya kipato, pia kisiasa.Badala ya kuliunganisha taifa kalitenganisha zaidi..
 
Mbona Rwanda wameweza?...CCM buana mna vimawazo mgando mgando tu
Hata Elimu bure msingi hadi sekondari walikataa, ingawaje wao wameleta Elimu bila ada huku ikiongezwa michango kibao.
 
vijana ambao tulifikiri watakuwa makini kuchambua sera za wagombea na ilani zao for the next 5 years, Ndio Hao Hao wako mitandaoni kubishana nani kajaza uwanja...Smh, Tuna safari ndefu sana fam. Tuko kishabiki zaidi dizaini ya simba na yanga!!
Mungu akubariki.
 
Umefanya tafiti? Na umeisabumit wap? Acha ukanjanja wakooo weeee mzeeee, furaha muikose nyie chademaaa baaada ya kuleta mgombea uraisi asiyejiwezaa hadi mpaka mikutano yake wameisusa, halafu unajumulishaa watanzania wote, lisu alidanganywa kiki ya kushambuliwa itampa sifa kubwa matokeo yake anejikuta anasuswa kila kukichaaaaa
 
mtu anaenda kuwakilisha wananchi bungeni mnwatimua uanachama watu wanakuaje na furaha sasa
 
Umefanya tafiti? Na umeisabumit wap? Acha ukanjanja wakooo weeee mzeeee, furaha muikose nyie chademaaa baaada ya kuleta mgombea uraisi asiyejiwezaa hadi mpaka mikutano yake wameisusa, halafu unajumulishaa watanzania wote, lisu alidanganywa kiki ya kushambuliwa itampa sifa kubwa matokeo yake anejikuta anasuswa kila kukichaaaaa
Hili la Lissu kudanganywa umefanya utafiti? Na umeisubmit wapi?
 
Back
Top Bottom