KWANINI Zitto Kabwe anaonekana ana uchu wa madaraka ya kitaifa?

KWANINI Zitto Kabwe anaonekana ana uchu wa madaraka ya kitaifa?

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
219,468
Reaction score
911,184
Mwanasiasa machachari, kijana na Mbunge wa upinzani Zitto Kabwe amekuwa akihimiza misimamo yenye migongano mingi kimasilahi na kuwapa upepo usiyo wa lazima mahasimu wake kisiasa kumvika joho la uchu wa madaraka ya kitaifa na haya ni baadhi tu ya maeneo ambayo yanamtia hatiani Mheshimiwa huyu:-


1) KWENYE kasheshe ya Buzwagi ambayo ilimweka kwenye chati ya siasa za nchi hii Bungeni alipinga vikali mikataba ya madini akidai ni ya kinyonyaji lakini JK kwa kushawishiwa na BARRICK GOLD alipompa ugali wa kula kwa kuwa mjumbe wa kamati ya Raisi kuchunguza na kushauri kuboresha mikataba ya madini Zitto Kabwe sasa hana matatizo na sheria na mikataba ya madini maana tumbo lake limeshibishwa vilivyo na BARRICK GOLD.

2) KWENYE ulaji wake alipokuwa Mwenyekitebe cha POC alikuwa mstari wa mbele kuhoji migongano ya kimasilahi kwa wabunge kuteuliwa nafasi za kiutendaji ndani ya serikali wanayoisimamia na hata alidiriki kusema hizo ni hongo za kuwaziba midomo wabunge wapelee kuisimamia serikali Bungeni lakini kuteuliwa kwake na JK akiwa mbunge kufanya kazi za kiutendaji kama kuchunguza namna ya kuboresha sheria na mikataba ya madini hakuona kuna migongano ya kimasilahi kwa sababu moja tu tumbo lake lilindwa vilivyo na BARRICK GOLD….

3) KWENYE ufisadi wa DOWANS pale TANESCO; akiwa mwenyekitebe cha POC, aliunga mkono walipwe hata kama hawakufanya kazi na hakuona uhaja ya wale waliotufikisha hatua ile kuaadibishwa! Mashinikizo tajwa ya watendaji wengi serikalini na baadhi ya wabunge kama Zitto yalitokana na kuahidiwa kumegewa kipande cha mkate na DOWANS na ndiyo maana walikuwa wakitetea walipwe.

4) KWENYE ufadhili wa BARRICK GOLD katika miradi mingi kwenye jimbo lake hususani ya elimu, Zitto Kabwe haoni kuna migongano ya kimasilahi kupokea hongo kutoka kwa wawekezaji ambao mikataba yao haramu alishiriki kuichunguza katika kamati teule ya Raisi na kutotoa ushauri wowote ule wenye masilahi kitaifa zaidi ya kusisitiza wahusika wana mikataba ambayo lazima iheshimiwe bila ya kuona mikataba yenyewe ni batili na hivyo haipaswi kuheshimiwa mbali ya kuleta ubaguzi ndani ya sekta ya madini………

5) KWENYE wadhifa wake wa Unaibu katibu Mkuu wa CDM na ujumbe wa kamati kuu ya CDM haoni amejirundikia madaraka wakati yeye pia ni mbunge lakini yuko mstari wa mbele kudai Raisi apunguziwe madaraka kwenye mapendekezo ya katiba batili ya marekebisho! Hajawahi kuhoji uhalali wa Bunge kupitisha sheria ya marekebisho ya katiba ambayo inakinzana na utaratibu ulioanishwa na katiba iliyopo na hivyo kufanya zoezi zima kuwa ni ukiukwaji wa katiba iliyopo!


6) KWENYE wadhifa wake wa Unaibu katibu Mkuu wa CDM na ujumbe wa kamati kuu ya CDM haoni ana migongano ya kimasilahi pale anapohoji CDM kutopeleka mizania yake kwa CAG kwa takribani kipindi cha miaka mitatu huku ni mshiriki wa vikao vyote vya juu vya CDM ambako angeliweza kushauri makosa hayo kama yapo yarekebishwe.

7) KWENYE wadhifa wake wa Unaibu katibu Mkuu wa CDM na ujumbe wa kamati kuu ya CDM hasikii harufu kali ya wizi na ubadhirifu mkubwa unaoendelea ndani ya CDM wa fedha za wafadhili na za ruzuku kutoka serikalini na hajawahi hata kukemea zaidi ya kujitenga na wenzake kwa sababu tu hawamuungi mkono katika azma zake za kugombea Uraisi mwaka 2015.

8) KWENYE wadhifa wake wa sasa wa mwenyekitebe cha PAC amekuwa akihoji sana mishahara ya Raisi na Waziri Mkuu bila ya kutuelezea watanzania kwa sababu zipi bungeni hajawahi kupeleka muswada binafsi wa kutengua mishahara hiyo ikiwemo ya wabunge ambayo kila mwezi hupeperushiwa kwenye akaunti yake bila ya yeye binafsi kukerwa na uporaji huo wa wazi wa mali za umma.

9) AMA Vyeo ambavyo Zitto Kabwe amekuwa akivisaka kwa udi na uvumba ni Uraisi na uenyekiti wa CDM na migogoro aliyonayo na wenzie ndani ya CDM ni pale anapobaini wamekuwa kikwazo cha yeye binafsi kufanikisha azma zake za kukamata dola…………..


10) AMA Zitto Kabwe aliahidi kuwa mbunge kwa vipindi viwili ambavyo vinafikia ukomo mwaka 2015 lakini kampeni za tamaa za mzee fisi za kuendelea kuwa mbunge kama uraisi utashindikana nazo anazichochea……………bila kuweka wazi mabadiliko ya ahadi zake yanachochewa na nini..........

KWA HULKA NA SILIKA kama hizi hivi mahasimu wake wa kisiasa ndani na nje ya CDM wanakosea kumwona ana uchu wa madaraka ya kukamata dola tu?
 
Kitendo cha Mwenyekitebe cha PAC kuwaita makatibu wakuu wa vyama vya siasa vinavyopokea ruzuku kutoka serikalini, CAG na msajili wa vyama vya siasa ili kuujua ukweli wa suala hili unaonyesha ya kuwa Zitto kabwe alikurupuka kumwaga mtama kwenye kuku wengi wakati mapishi kumbe bado hayajakamilika...........Kwa lugha nyingine ni kuwa aliwatuhumu hata kabla hajawapa nafasi ya kujitetea.....sasa anawapa nafasi ya kujitetea huku alikwisha wahukumu. Hicho kikao ni mahakama ya mtaani tu!
 
He is one of the 'best Political double agent ' we have noted in this Multiparty politics era, striving to take a control of whatever power to quench his intense and selfish desire for power by whatever means.

He might be pursuing what "our man" said soon after 'seizing' power, "what I was 'looking for', I have got it"
 
Kuna kuwa na uchu wa madaraka na kuwa na utayari wa kuongoza.

Zitto ana utayari wa kuongoza, hana uchu wa madaraka.

Zitto angekuwa na uchu wa madaraka asingetumia resources zake kuwawezesha wanasiasa vijana chipukizi kama Kafulila na wengine.
 
Kitendo cha Mwenyekitebe cha PAC kuwaita makatibu wakuu wa vyama vya siasa vinavyopokea ruzuku kutoka serikalini, CAG na msajili wa vyama vya siasa ili kuujua ukweli wa suala hili unaonyesha ya kuwa Zitto kabwe alikurupuka kumwaga mtama kwenye kuku wengi wakati mapishi kumbe bado hayajakamilika...........Kwa lugha nyingine ni kuwa aliwatuhumu hata kabla hajawapa nafasi ya kujitetea.....sasa anawapa nafasi ya kujitetea huku alikwisha wahukumu. Hicho kikao ni mahakama ya mtaani tu!
Kuna mtu Fb alimtwanga hii kitu akatokomea

''Naisoma Public Audit act na kuirudia tena na tena sioni mahusiano ya CAG na Vyama vya siasa!!Ila naona indirect relationship kati yake na vyama vya siasa kupitia kwa msajili wa vyama hivyo!!Labda ni uelewa wangu tu!!Swali la msingi internal audit wa msajili wa vyama je anakagua matumizi ya vyama hivi!!Katika accountability and Governance system ya nchi hii vyama vya siasa haviko accountable kwa PAC!!TUWEKE SIASA pembeni the only person accountable to PAC ni Msajili wa vyama vya SIASA!''
 
Hi Ruta,

Nilikua napita tu nikisoma kwa haraka nikaona hii thread yako... Naona nitakua siitendei haki nisipo changia pia... Ngoja twende nukta baada ya nukta maana pamoja na kua mimi sio mwanachama wa chadema Zitto ni mmoja ya wanachadema ninao wakubali. Wapo wengine ila either they don't communicate much or they don't make the news headlines. but nawakubali sana tu.
Umepanga thread yako as if una fact but in reality ni hisia zaku tu na hata hizo hisia hukufika kwa kutumia any analysis, ni just pure assumptions. Hasa hizo nukta za mwanzo unapo zungumzia about mining and how he was tipped to shut the process down.
Sijui wewe ulitaka iweje, maana yeye na civil society, na Chadema waliona ni sawa kamati iundwe na itoe maone, then sheria ibadilishwe kufatana na maoni hayo. sheria haijaklamilika na mabadiliko yanaendelea (las in date was just earlier this year). Kupinga ni haki ya kila mtu ina uwezo wa kutoa mawazo mbadala hakupewa kila mtu.
Unapo mtabiria kua ana nia ya kugombea wenyekiti wa chama napend kujua hizo taarifa umezitoa wapi maana hatujaziskia. alisema anatamani kugombea uraisi na akaongeza kua hatozungumzia ntena hadi katiba mpya itakapo patikana (so he can first see if he qualifies or not). Sasa kusema kua anacho kifanya sasa ni sababu anavizia hivyo vyeo, wakati hata hatujui kama anaweza kuvigombea, ni dhana yako tu na sio fact.
Zitto alisema atawahoji makatibu wa vyama kwa sababu kuna tofauti ya kauli kati ya vyama, CAG na Registrar. Angekua kawahukumu wala asingewaita. Hivi kwanini Tanzania watu wanaogopa kuhojiwa? kuhojiwa ni kupewa nafasi ya kutoa version yako ili pande zote za shilingi zionekane kabla maamuzi hayakjachukuliwa. Angekua kawahukumu angewaita wa nini?
Halafu nimalize kwa kusema kua yote anayo yafanya mi nayaona in line na sheria za nchi, au in line na spirit ya katiba. Haamui yeye kama yeye sababu ukimtoa madaraka Zitto ni mwananchi wa kawaida kabisa. Anatoa matamko, maamuzi na anatenda kwa kutumia madaraka aliop[ewa na wananchi (Ubunge) au alio pewa na Bunge (Mwenyekiti wa PAC) au alio pewqa na chama (naibu katibu mkuu wa chama). Ikiwa anacho kifanya ni tofauti na taasisi hizo basi hapo ndio awe condemned.
Kwa kifupi umesoma alicho fanya Zitto, ukaamua kua alitumwa na tamaa ya madaraka (au njaa), na ukatoa conclusion kutokana na mawazo yako hayo ambayo yanasimamia hisia zako, na sio facts.
Ni hayo tu kwa sasa.
 
Kuna mtu Fb alimtwanga hii kitu akatokomea

''Naisoma Public Audit act na kuirudia tena na tena sioni mahusiano ya CAG na Vyama vya siasa!!Ila naona indirect relationship kati yake na vyama vya siasa kupitia kwa msajili wa vyama hivyo!!Labda ni uelewa wangu tu!!Swali la msingi internal audit wa msajili wa vyama je anakagua matumizi ya vyama hivi!!Katika accountability and Governance system ya nchi hii vyama vya siasa haviko accountable kwa PAC!!TUWEKE SIASA pembeni the only person accountable to PAC ni Msajili wa vyama vya SIASA!''

True.very true na wao PAC wamkamate koromeo badala ya kukimbilia kwenye vyombo vya khabari kujitafutia umaarufu wa bei poa...............
 
Hi Ruta,

Nilikua napita tu nikisoma kwa haraka nikaona hii thread yako... Naona nitakua siitendei haki nisipo changia pia... Ngoja twende nukta baada ya nukta maana pamoja na kua mimi sio mwanachama wa chadema Zitto ni mmoja ya wanachadema ninao wakubali. Wapo wengine ila either they don't communicate much or they don't make the news headlines. but nawakubali sana tu.
Umepanga thread yako as if una fact but in reality ni hisia zaku tu na hata hizo hisia hukufika kwa kutumia any analysis, ni just pure assumptions. Hasa hizo nukta za mwanzo unapo zungumzia about mining and how he was tipped to shut the process down.
Sijui wewe ulitaka iweje, maana yeye na civil society, na Chadema waliona ni sawa kamati iundwe na itoe maone, then sheria ibadilishwe kufatana na maoni hayo. sheria haijaklamilika na mabadiliko yanaendelea (las in date was just earlier this year). Kupinga ni haki ya kila mtu ina uwezo wa kutoa mawazo mbadala hakupewa kila mtu.
Unapo mtabiria kua ana nia ya kugombea wenyekiti wa chama napend kujua hizo taarifa umezitoa wapi maana hatujaziskia. alisema anatamani kugombea uraisi na akaongeza kua hatozungumzia ntena hadi katiba mpya itakapo patikana (so he can first see if he qualifies or not). Sasa kusema kua anacho kifanya sasa ni sababu anavizia hivyo vyeo, wakati hata hatujui kama anaweza kuvigombea, ni dhana yako tu na sio fact.
Zitto alisema atawahoji makatibu wa vyama kwa sababu kuna tofauti ya kauli kati ya vyama, CAG na Registrar. Angekua kawahukumu wala asingewaita. Hivi kwanini Tanzania watu wanaogopa kuhojiwa? kuhojiwa ni kupewa nafasi ya kutoa version yako ili pande zote za shilingi zionekane kabla maamuzi hayakjachukuliwa. Angekua kawahukumu angewaita wa nini?
Halafu nimalize kwa kusema kua yote anayo yafanya mi nayaona in line na sheria za nchi, au in line na spirit ya katiba. Haamui yeye kama yeye sababu ukimtoa madaraka Zitto ni mwananchi wa kawaida kabisa. Anatoa matamko, maamuzi na anatenda kwa kutumia madaraka aliop[ewa na wananchi (Ubunge) au alio pewa na Bunge (Mwenyekiti wa PAC) au alio pewqa na chama (naibu katibu mkuu wa chama). Ikiwa anacho kifanya ni tofauti na taasisi hizo basi hapo ndio awe condemned.
Kwa kifupi umesoma alicho fanya Zitto, ukaamua kua alitumwa na tamaa ya madaraka (au njaa), na ukatoa conclusion kutokana na mawazo yako hayo ambayo yanasimamia hisia zako, na sio facts.
Ni hayo tu kwa sasa.

Kwanza nikushukuru sana for declaring interest that you have soft spot for the guy...........as such you are not objective on the subject but very subjective to pleasing him!....................lakini on serious note ni kuwa afanye kazi kwa vikao na apeleke ushauri Bungeni waliomtuma.........................yeye siyo bunge, period!
 
Kwanza nikushukuru sana for declaring interest that you have soft spot for the guy...........as such you are not objective on the subject but very subjective to pleasing him!....................lakini on serious note ni kuwa afanye kazi kwa vikao na apeleke ushauri Bungeni waliomtuma.........................yeye siyo bunge, period!

Having a soft spot is a personal issue. Kumkubali kwa kazi anazo zifanya is something objective. Don't distort what I said.
Halafu yeye hajawahi sema (au kuonesha) kua yeye ndio bunge. Kama kuna mtu anapenda ku-stick to the procedures ni yeye. He never tries to excites the mass using hate or passion but he uses texts, rules, regulations and best practices.
Wapo ambao wanajiona wenyewe na taasisi wanazo simamia ni kitu kimoja, kiasi cha kuchanganya personal opinion, personal belonging na hata personal relations na taasisi wanazo simamia. Ila kwa leo tunamjadili Zitto, so I wont dwell on this.
Back to Zitto, unaweza kutoa ushahidi wa kua alipokea chochote toka Barick?
 
Watanzania wenzangu kwa uelewa wangu miye nitasema ukweli daima ya kwamba hakuna kiongozi yeyote alobakia na mtetezi wa haki tena anakupa za uso kama Zitto. Zitto ni mkweli, mtu anayemkoma nyani giledi bila kumwonea aibu na hilo linawachukiza wengi japo ana makosa yake kama binadamu. Lakini kama kiongozi Zitto namkubali na sidhani kama tuna mtu individual anayefaa kuwa rais wa Tanzania zaidi yake kwa sasa hivi.

Na imefika mahala naanza kumwelewa zaidi kwa sababu hakuna kiongoz mwenye mfano bora na mwenye uchungu, mwenye uzalendo wa kweli zaidi ya propaganda za kisiasa ambazo wakisha ingia madarakani wanachota na kujisifia kuwa wao hawawezi kuishi kimaskini kwa sababu majirani walowapa kura kuwaongoza ni maskini. Zitto anachukiwa kwa sababu sio kama wao, sio MNAFIKI maana Mnafiki ni yule anayeahidi vitu hatimizi, anayeaminiwa lakini haaminiki, na mwongo!.. Ishara hizi wanazo viongozi wengi sana wa Tanzania kuliko Zitto.
 
Back
Top Bottom