Kweli kiswahili kitatufikisha nchi ya ahadi?

Kweli kiswahili kitatufikisha nchi ya ahadi?

Pangaea

JF-Expert Member
Joined
Jun 14, 2012
Posts
202
Reaction score
41
WanaJF.
Nipo kando ya TV ninafuatilia majadiliano bungeni. Ninaona waheshimiwa kadhaa wananadai nchi hii itaendelea iwapo Kiswahili kitaenziwa. Ninatambua umuhimu wa lugha kama chombo cha mawasiliano na nionavyo hapa Tanzania hatuna tatizo la uelewa wa Kiswahili. Pia sheria, vitabu vya kufundishia nk vinaweza kuandikwa kwa Kiswahili ili wasiofahamu Kiingereza waweze kufahamu. Lakini siamini kama kuuondoa Kiingereza na kubaki na Kiswahili peke yake si sababu ya kuondoa umaskini, kuboresha elimu, kuleta haki na usawa katika nchi, kukuza uzalendo. Jambo la msingi ni kuboresha elimu ya Tanzania- maslahi ya waalimu, mazingira ya shule, vyuo vinavyofundisha walimu (hasa vyuo vikuu) na sifa za kuwa mwalimu zitizamwe (mtu ambaye hajapata mafunzo ya ualimu asirusiwe kufundisha kama ilivyo sasa), mitaala iboreshwe nk. Siamini kama nchi za wenzetu hazifundishi lugha za kigeni. Suala ni ubora wa elimu. Ninaomba kuwasilisha.
 
WanaJF.
Nipo kando ya TV ninafuatilia majadiliano bungeni. Ninaona waheshimiwa kadhaa wananadai nchi hii itaendelea iwapo Kiswahili kitaenziwa. Ninatambua umuhimu wa lugha kama chombo cha mawasiliano na nionavyo hapa Tanzania hatuna tatizo la uelewa wa Kiswahili. Pia sheria, vitabu vya kufundishia nk vinaweza kuandikwa kwa Kiswahili ili wasiofahamu Kiingereza waweze kufahamu. Lakini siamini kama kuuondoa Kiingereza na kubaki na Kiswahili peke yake si sababu ya kuondoa umaskini, kuboresha elimu, kuleta haki na usawa katika nchi, kukuza uzalendo. Jambo la msingi ni kuboresha elimu ya Tanzania- maslahi ya waalimu, mazingira ya shule, vyuo vinavyofundisha walimu (hasa vyuo vikuu) na sifa za kuwa mwalimu zitizamwe (mtu ambaye hajapata mafunzo ya ualimu asirusiwe kufundisha kama ilivyo sasa), mitaala iboreshwe nk. Siamini kama nchi za wenzetu hazifundishi lugha za kigeni. Suala ni ubora wa elimu. Ninaomba kuwasilisha.

Kwangu mimi uko sahihi. Nchi za kiarabu zinatumia kiarabu katika kila kitu, mbona maendeleo yao ni mafuta tu na wala hawana la zaidi! Yakiondoka mafuta/kila nchi ikiwa na mafuta wanakuwa kama sisi. Sweden huwezi kupata cheti bila kufaulu kiingereza! Fuatilia utaona ukweli! Sawa tuwe na lugha yetu lakini maendeleo hayatakuja kwa kusema kiswahili fasaha.
 
Kwangu mimi uko sahihi. Nchi za kiarabu zinatumia kiarabu katika kila kitu, mbona maendeleo yao ni mafuta tu na wala hawana la zaidi! Yakiondoka mafuta/kila nchi ikiwa na mafuta wanakuwa kama sisi. Sweden huwezi kupata cheti bila kufaulu kiingereza! Fuatilia utaona ukweli! Sawa tuwe na lugha yetu lakini maendeleo hayatakuja kwa kusema kiswahili fasaha.
Ni kweli mkuu, suala hapa lazima UBORA wa elimu uangaliwe. Watu waache visingizio. Fuatilia matokeo ya mtihani wa Kiswahili wa kidato cha nne uone wanafunzi wanavyofeli. Tungetarajia kuona "A" za kutosha katika somo la kiswahili. Wapo wanaosoma "English medium schools" na wanaongea Kiswahili kizuri sana.
 
Ziko sababu nyingi za wazi na zinazotatulika zinazosababisha umaskini ama kukosa maendeleo kwa Tanzania. Kusema kiswahili ndicho kitaondoa matatizo haya ni uvivu wa kufikiri ama kukosa maono na elimu sahihi ya maendeleo, kukosa uchungu and nia ya dhati ya kuondoa umaskini, ama kukata tamaa.

Kukuza na kuuza kiswahili siyo kosa lakini si mtaji mkubwa na wa pekee wa maendeleo ya Tanzania. Kiswahili kama lugha nyingine yoyote kitauzika kimataifa ikiwa kitaambatana na vivutio ama umuhimu. Badala ya kuanza kusema tubadili mitaala tusomeshe watoto hadi University Kiswahili, ni vizuzri tukaanza kujichimbia katika ubunifu na uvumbuzi wa kisayansi na technologia sahihi ambayo itavutia wanunuzi wengi ambapo ili waweze kuinunua na kuitumia ipasavyo kwa manufaa muafaka, lazima wajue kiswahili. Kuwaza tutafika mbalil kwa longo longo tu ya uswahili wetu hapa ni matumizi mabaya ya muda wa uzalishaji na raslimali za taifa. Na kama tukianza eti kiswahli bila technolojia tutakuwa kama bush men. Mimi napita.
 
Kuna umuhimu wowote wa kutunza utamaduni wa nchi?
Labda ukijibu hili naweza kukuelewa labda.
 
Utamaduni wa nchi ni lazima utunzwe. Bila utamaduni tutakuwa ni taifa lisilo na msingi. Naomba tuende mbele zaidi tuangalie, utamaduni wa nchi yetu ni upi? Unakwenda katika upana gani? Tanzania inaundwa na jamii mbali mbali zenye tamaduni tofauti na ambazo kwa ujumla wake zinaumba utamaduni wa Mtanzania. Tunazo sera na kanuni rasmi ambazo zinazimamia utunzaji na hata mirathi ya utamaduni wetu kwa vizazi vijavyo? Kiswahili ni moja ya utamaduni wetu na tunatakiwa kuheshimu na kuenzi kwa maana sahihi ya manufaa ya maendeleo. Katika kuenzi utamaduni lazima kuwe na sayansi na sanaa sahihi inayotoa mwongozo unaopelekea kuhakikisha kwamba tamaduni zetu zipo kwa ajili ya maendeleo chanya na si vinginevyo. Naomba ieleweke kwamba tafsiri na matumizi mabaya ya dhana za kutunza tamaduni vinaweza kutupeleka katika msala wa kutisha. Tupo pamoja.
 
Kuna umuhimu wowote wa kutunza utamaduni wa nchi?
Labda ukijibu hili naweza kukuelewa labda.
Utamaduni upi unaotaka kutunza? Hebu iangalie jamii yako na jiangalie wewe. Wakenya wanaosifika kwa kujua Kiingereza wameshawapita Watanzania kwa kukitumia Kiswahili, UMEWAHI KUJIULIZA NI KWA NINI!!! umewahi kuwasikia wakiziacha lugha zao za asili? Ama hata hicho Kiingereza?
 
Mie mfurukutwa wa Kiswahili na mfurukutwa wa fizikia.

Nimepewa mchongo wa kutafsiri kitabu cha fizikia kwenda Kiswahili.

Nitafsirie neno "quantum" liende katika Kiswahili kwanza, ukiweza tunaweza kuongea kuhusu Kiswahili kutuwezesha.
 
WanaJF.
Nipo kando ya TV ninafuatilia majadiliano bungeni. Ninaona waheshimiwa kadhaa wananadai nchi hii itaendelea iwapo Kiswahili kitaenziwa. Ninatambua umuhimu wa lugha kama chombo cha mawasiliano na nionavyo hapa Tanzania hatuna tatizo la uelewa wa Kiswahili. Pia sheria, vitabu vya kufundishia nk vinaweza kuandikwa kwa Kiswahili ili wasiofahamu Kiingereza waweze kufahamu. Lakini siamini kama kuuondoa Kiingereza na kubaki na Kiswahili peke yake si sababu ya kuondoa umaskini, kuboresha elimu, kuleta haki na usawa katika nchi, kukuza uzalendo. Jambo la msingi ni kuboresha elimu ya Tanzania- maslahi ya waalimu, mazingira ya shule, vyuo vinavyofundisha walimu (hasa vyuo vikuu) na sifa za kuwa mwalimu zitizamwe (mtu ambaye hajapata mafunzo ya ualimu asirusiwe kufundisha kama ilivyo sasa), mitaala iboreshwe nk. Siamini kama nchi za wenzetu hazifundishi lugha za kigeni. Suala ni ubora wa elimu. Ninaomba kuwasilisha.

Mkuu nakubaliana na wewe kuhusu hili ila inabidi uwe makini sana. For the time being kama unataka ufanikiwe kielimu ama kiajira then ni lazima ujue kuongea na kuandika English vizuri.
Wewe ingia ktk mkumbo wa kukikandia kiingereza then ukienda job interviews utakwaa kisiki. Wanasiasa wenu kila kukicha wanaimba wimbo wa kiswahili sijui iwe lugha ya taifa na tukienzi, lakini jiulize watoto wao wanasoma wapi?
Ukijilinganisha na nchi kama sijui Sweden ama China utakuwa unapotea. Hao wachina wenyewe wanajitahidi sana kujifunza English. Tanzania ni nchi maskini, hivyo hatuna ubavu wa kusema oooh tung'ang'anie kiswahili na tuachane na English. Hapo utakuwa unajidanganya.
Halafu wakenya na waganda wakija bongo kuchukua kazi zenu kwaajili ya umaimuna wenu mnaanza kuwachukia.
Be very careful na huu mkumbo wa kukienzi kiswahili
 
Ni kweli mkuu, suala hapa lazima UBORA wa elimu uangaliwe. Watu waache visingizio. Fuatilia matokeo ya mtihani wa Kiswahili wa kidato cha nne uone wanafunzi wanavyofeli. Tungetarajia kuona "A" za kutosha katika somo la kiswahili. Wapo wanaosoma "English medium schools" na wanaongea Kiswahili kizuri sana.

Actually "A" nyingi zinatoka english medium!!!Sawa kabisa
 
Utamaduni upi unaotaka kutunza? Hebu iangalie jamii yako na jiangalie wewe. Wakenya wanaosifika kwa kujua Kiingereza wameshawapita Watanzania kwa kukitumia Kiswahili, UMEWAHI KUJIULIZA NI KWA NINI!!! umewahi kuwasikia wakiziacha lugha zao za asili? Ama hata hicho Kiingereza?

Umegusa sehemu nyeti sana kuhusu Wakenya na Kiswahili.

Ili uweze kumfundisha mgeni, mfano Wamarekani weusi wameanza kukihusudu Kiswahili, inabidi uwe competent na kiingereza. Hapo ndo wanapotupiga bao Wakenya. Sasa leo ukitaka kuondoa Kiingereza kabisa maana yake the Kenyans will have the upper hand
 
Ukweli mimi huwa nasikitika watu wanapo-undermine umuhimu wa lugha ya Kiingereza. Kwa dunia ya leo yenye ushindani mkubwa kingereza ni muhimu sana, na kutojua kwetu kungereza kunatugharimu sana mpaka dakika hii, nenda kwenye mahoteli yetu ya kitalii wamejaa wakenya, nenda Arusha tour-guide wengi ni wakenya, bila kiingereza tunapunguza sana uwezo wetu wa kushindana kimataifa.

Sipingi kuenzi Kiswahili, lakini nasisitiza kwamba tunaweza kuenzi Kiswahili na bado tukaweka msisitizo katika kujua Kiingereza. Hivi mnajua kwamba pamoja na kujigamba katika umahili wa Kiswahili bado wengi waofundisha Kiswahili Marekani na nchi nyingine ni Wakenya?

Tuache unafiki, unakuta mtu anapinga matumizi ya Kiingereza mashuleni wakati mtoto wake anasoma English mediaum school.
 
Ukweli mimi huwa nasikitika watu wanapo-undermine umuhimu wa lugha ya Kiingereza. Kwa dunia ya leo yenye ushindani mkubwa kingereza ni muhimu sana, na kutojua kwetu kungereza kunatugharimu sana mpaka dakika hii, nenda kwenye mahoteli yetu ya kitalii wamejaa wakenya, nenda Arusha tour-guide wengi ni wakenya, bila kiingereza tunapunguza sana uwezo wetu wa kushindana kimataifa.

Sipingi kuenzi Kiswahili, lakini nasisitiza kwamba tunaweza kuenzi Kiswahili na bado tukaweka msisitizo katika kujua Kiingereza. Hivi mnajua kwamba pamoja na kujigamba katika umahili wa Kiswahili bado wengi waofundisha Kiswahili Marekani na nchi nyingine ni Wakenya?

Tuache unafiki, unakuta mtu anapinga matumizi ya Kiingereza mashuleni wakati mtoto wake anasoma English mediaum school.
Halafu wakenya na waganda wakija bongo kuchukua kazi zenu kwaajili ya umaimuna wenu mnaanza kuwachukia.
Be very careful na huu mkumbo wa kukienzi kiswahili
 
Hivi mnajua kwamba pamoja na kujigamba katika umahili wa Kiswahili bado wengi waofundisha Kiswahili Marekani na nchi nyingine ni Wakenya?

Mkuu, Uganda kwenye redio yao ya Taifa wana kipindi cha Kiswahili. Siku nikapiga simu kuomba niwe mgeni wao na nikapewa appointment

Siku ya siku tukawa live on air. Pamoja na host palikuwa na mgeni mwingine kijana tu mwenye asili ya Congo. Hao jamaa wapo fit mimi cha mtoto. Ila kwasababu Kiswahili kwa mimi ni kama Chelsea kuchezea Stamford Bridge bado niliweza kuchangia penye utata.

Baada ya hapo yule host kumbe ni Mwalimu katika shule ya msingi Nakasero pale Kampala akanialika kwenye vipindi vyake. Jamaa ni Mganda lakini anaongea Kiswahili cha Tanzania fasaha kabisa. Anafundishia kwa kutumia vitabu vya Wakenya ila he is so pragmatic he's got many excerpts from Nipashe newpapers for highlighting different topics
 
Kiswahili ni moja ya utamaduni wetu. Kiswahili kinaongewa karibia katika nchi Sita za africa, Zaire, Uganda, Kenya, Burundi, Rwanda, Tanzania na kidogo southern Sudan. Lakini utakuta nchi hizo mbali ya kuongea kiswahili , zina Lugha moja ya kimataifa wanaongea kwa ufasaha sana . Kiingereza au Kifaransa ni moja ya Lugha muhimu sana kuzijua .

Hapa marekani , kila niendapo hospitalini nina kuta madaktari bingwa ni wakenya, waghana na wanigeria tuu lakini watanzania hamna hatupo.. Kwa hiyo Lugha za nje zinasaidia sana wataalamu wetu kupata kazi nje ya nchi.

Waisrael walipowaokoa ndugu zao pale Entebe mwaka 1976 siraha kubwa walioitumia kumtenga mtu gaidi na raia wao ni lugha ya kiebrania. walisema lala chini wote kwa kiebrania, na waisraeli wote walilala chini , ila wale waliosimama hawakujua kimesemwa nini, ndipo askari wa israeli waliwafyatulia risasi na kuwapeleka ahera mipalestina na mijerumani miuaji,mara moja.

Hivyo kiswahili ni kizuri kukitumia, lakini Lugha ya kiingereza nayo ina umuhimu wake.
 
WanaJF.
Nipo kando ya TV ninafuatilia majadiliano bungeni. Ninaona waheshimiwa kadhaa wananadai nchi hii itaendelea iwapo Kiswahili kitaenziwa. Ninatambua umuhimu wa lugha kama chombo cha mawasiliano na nionavyo hapa Tanzania hatuna tatizo la uelewa wa Kiswahili. Pia sheria, vitabu vya kufundishia nk vinaweza kuandikwa kwa Kiswahili ili wasiofahamu Kiingereza waweze kufahamu. Lakini siamini kama kuuondoa Kiingereza na kubaki na Kiswahili peke yake si sababu ya kuondoa umaskini, kuboresha elimu, kuleta haki na usawa katika nchi, kukuza uzalendo. Jambo la msingi ni kuboresha elimu ya Tanzania- maslahi ya waalimu, mazingira ya shule, vyuo vinavyofundisha walimu (hasa vyuo vikuu) na sifa za kuwa mwalimu zitizamwe (mtu ambaye hajapata mafunzo ya ualimu asirusiwe kufundisha kama ilivyo sasa), mitaala iboreshwe nk. Siamini kama nchi za wenzetu hazifundishi lugha za kigeni. Suala ni ubora wa elimu. Ninaomba kuwasilisha.

Kichagga ndio kitakufikisha unapopataka.
 
Wakenya wanakijua Kiingereza na lugha zao za kikabila, sasa hivi kiswahili ndiyo lugha rasmi ya taifa lao. Kenya ndiyo inatambulikana kama chimbuko la lugha kiwahili duniani, ndiyo maana google na microsoft walichukuwa wakenya wengi kutafsiri kiingereza kwenda kiswahili. Tanzania tunakumbuka shuka asubuhi, tulishapigwa bao. Asili ya kiswahili ni KENYA.
 
Wakenya wanakijua Kiingereza na lugha zao za kikabila, sasa hivi kiswahili ndiyo lugha rasmi ya taifa lao. Kenya ndiyo inatambulikana kama chimbuko la lugha kiwahili duniani, ndiyo maana google na microsoft walichukuwa wakenya wengi kutafsiri kiingereza kwenda kiswahili. Tanzania tunakumbuka shuka asubuhi, tulishapigwa bao. Asili ya kiswahili ni KENYA.

Hapana mkuu, mimi nadhani ni kwasababu unlike Tanzanians the Kenyans consider Kiswahili and English equally important thus they're competent in both
 
kuacha kusisitiza kiswahili ndio kumetufikisha hapa. umoja wetu umekuwa dhaifu. kuna wanaohisi kuwa kwa kujiunga na wazungumzaji wa kiingereza wamejikomboa tayari. kumbe wamejitoa kwao wanaelea kwn limbo. msemo wa chako ni chako. cha kuazima..... ni wa kweli.
mpaka tutakapoweza kujitambua sisi ni nani ndio tutaweza kupiga hatua kama nchi.
 
WanaJF.
Nipo kando ya TV ninafuatilia majadiliano bungeni. Ninaona waheshimiwa kadhaa wananadai nchi hii itaendelea iwapo Kiswahili kitaenziwa. Ninatambua umuhimu wa lugha kama chombo cha mawasiliano na nionavyo hapa Tanzania hatuna tatizo la uelewa wa Kiswahili. Pia sheria, vitabu vya kufundishia nk vinaweza kuandikwa kwa Kiswahili ili wasiofahamu Kiingereza waweze kufahamu. Lakini siamini kama kuuondoa Kiingereza na kubaki na Kiswahili peke yake si sababu ya kuondoa umaskini, kuboresha elimu, kuleta haki na usawa katika nchi, kukuza uzalendo. Jambo la msingi ni kuboresha elimu ya Tanzania- maslahi ya waalimu, mazingira ya shule, vyuo vinavyofundisha walimu (hasa vyuo vikuu) na sifa za kuwa mwalimu zitizamwe (mtu ambaye hajapata mafunzo ya ualimu asirusiwe kufundisha kama ilivyo sasa), mitaala iboreshwe nk. Siamini kama nchi za wenzetu hazifundishi lugha za kigeni. Suala ni ubora wa elimu. Ninaomba kuwasilisha.

mm nakubaliana na hoja kuwa endapo kiswahili kitatumika nchi yetu inaweza kupata maendeleo. sababu ziko nyingi la msingi kabisa lazima sote tukubaliane lugha ni njia ya mawasiliano na maelewano. sasa wewe angalia viko vitu vya msingi kama vingeandikwa kwa kiswahili kuhusu masuala ya afya na kilimo hata mwananchi wa kawaida angejua na kuchukua tahadhari

mm nimejaliwa kutembea nchi za ASia kadhaa, ndugu yangu asilimia karibu 97% hawajui Kiingereza, wanajifunza katika lugha zao, na zimewarahisishia kuwasiliana na kuelewana kirahisi, na ndio umekuwa mwanzo wa kufanya vizuri katika maendeleo. kwanini? hata vitabu vinaandikwa ktk lugha yao, vinasomwa na kueleweka hata na wananchi wa kawaida na kisha inakuwa rahisi kutekelezwa. lkn kwetu unakuta hata sera/mikakati/miongozo/sheria zinaandikwa kwa kiingereza wakati mwananchi wa kawaida hajui kiingereza na ni sehemu ya utekelezaji wa maamuzi yaliyoandikwa, unatarajia nini? ataweza kusoma na kuelewa

nashauri tubadilike, tujifunze kwa kiswahili

upungufu mwingine kuhusu walimu wasio na sifa hilo linatekelezeka ikiwa siasa haitaingilia suala la elimu na maslahi ya wahusika. ww fikiria kwasbabu ya upungufu wa ualimu miaka ya 2004-2008 hivi walichukuliwa vijana wengi waliomaliza F4-F6 na kuajiriwa baada ya kufundishwa kwa muda wa miezi mitatu, je unatarajia nn, huu ulikuwa mwanzo wa kuvuruga msingi mzuri wa elimu. vilevile watu waliofeli ndio wanachukuliwa kuwa walimu unatarajia nn? mbona vyuo vikuu havichukui watu wasiopata GPA chini ya upper second na first class. hl litizamwe vizuri na kwa makini

kuhusu wanafunzi kufeli kiswahili mm siwezi kushangaa kwani kile kiswahili kinavyofundishwa kinakuwa kimeacha utaratibu wa kawaida wa kumfanya mtu kuelewa na kisha kumpima uelewa. kimekuwwa too complicated, mm nimesoma kiswahili hadi A-Level, ninajua tatizo kwann watu kiswahili kina washinda kufaulu. mfumo na namna ya ufundishaji wake ni tatizo

suala lingine ni mfumo wa elimu, hauzingatii vipaji vya wananchi, mtu unasoma masomo kibao wakati mwingine bila sababu. vipaji vitambuliwe na viendelezwe, ndipo tutapata walimu bora, wanasayansi bora, wasaikolojia bora, watawala bora, wanasheria bora n.k.
 
Back
Top Bottom