Kwenu LATRA na Serikali ya Mkoa

Kwenu LATRA na Serikali ya Mkoa

ikerege

Member
Joined
Jun 21, 2022
Posts
22
Reaction score
13
Juzi nikua mkoani Mbeya na Tunduma katika safari zangu ila kwa nilichoshuhudia ni mateso sana, sijui tatizo nini. Sikuweza kupata usafiri wa saa 12 alfajiri kwahiyo nikaja Uyole kuvizia usafiri wowote. Jamani, tulipandishwa bus aina ya fuso ambalo lilituacha Makambako!

Mpaka tunafika Dar tulikuwa tumepanda bus 4, kisa hizo gari 'za hakuna' kulala haziruhusiwi, na abiria ni wengi kupita maelezo. Hizi gari zilikuwa zinasaidia sana pale Uyole maana wasafiri kutoka Malawi, Zambia wanaochelewa asubuhi tunapanda nao, kuzikataza imekua ni kero kubwa sana, sijui mbadala wake ni upi.

Mama anafungua nchi, RC anasema K/Koo iwe 24/7 wageni waje na kufanya biashara, sasa wanakwama hapo Uyole, usafiri ni shida. Ruhusuni bus kubwa muwape ratiba ya mchana au hizo coaster muwape vibali wafanye biashara, hali ni mbaya sana, nadhani wakazi wa Mbeya mtakua mnaelewa.
 
Tatizo speed kali na unajua kabisa hali ya barabara za Tanzania ni mbovu sasa fikiria safari ya usiku, pia kutaka gari iende irudi ndani ya siku mbili.
 
Tatizo ulikubali pokewa na mawinga wa pale Uyole...

Iko hivi, gari zako pale ila zaondoka

Kuna Noah zinazoleta magazeti zinalala ndani

Zaondoka giza, saa 12 uko Dsm

Au unapanda tanker za Transit hazilali
 
Sijapata comment ya maana kumbe na nyinyi waluwalu tu, nataka LATRA watujibu kwanini wasitoe vibali bus kubwa kama NEWFORCE zianze ratiba ya mchana ?mbona ilikuepo tunduma saa 5 asubuhi,?
 
Mama anafungua nchi, RC anasema K/Koo iwe 24/7 wageni waje na kufanya biashara, sasa wanakwama hapo Uyole, usafiri ni shida. Ruhusuni bus kubwa muwape ratiba ya mchana au hizo coaster muwape vibali wafanye biashara, hali ni mbaya sana, nadhani wakazi wa Mbeya mtakua mnaelewa.
Waboreshe TAZARA pia
 
Back
Top Bottom