Uchaguzi 2020 Kwenu ndugu zangu watanzania zingatia haya

Uchaguzi 2020 Kwenu ndugu zangu watanzania zingatia haya

4 7mbatizaji

JF-Expert Member
Joined
Dec 8, 2019
Posts
8,406
Reaction score
9,619
Ndugu zangu nawasalim wote wakubwa kwa wadogo kupitia yule atupae pumzi.

Kichwa cha habari hapo juu chahusika na tukiwa tumebaki na siku mbili kuwapigia viongozi wetu tuwatakao, hivyo zingatia yafuatayo

1. Tafadhali sana kapige Kura, na chagua kiongozi umpendaye bila shurti ya mtu yeyote

2. Tuna wagombea wengi ila kwa kweli CHADEMA na CCM ndo habari ya mjini na Moto unawaka kwa vyama hivi viwili, mtoto hatumwi sokoni na hivyo kwenye karatasi ya wagombea urais CCM chini ya mgombea wao yupo namba moja na CHADEMA chini ya mgombea wao a.k.a Simba wa Yuda, kimbunga Lissu 2020, au wengine husema mbeba maono, ni wa mwisho, namanisha ndo amefunga karatasi ya wapiga Kura.

3. Upigapo Kura punguza hasira au furaha moyoni mwako ili usiharibu Kura ya mgombea unaemtaka. Weka vema kwenye kisanduku cha mgombea umpendae isitoke nje ya kibox na usifanye cha ziada mfano Kama kutoboa macho ya mgombea utakuwa umeharibu Kura.

4. Kura ni Mali yako maana we ndo mwajiri wa viongozi wako kuanzia diwani, mbunge, mpaka rais hivyo una haki kulinda Kura yako au kutoilinda Kama Kuna mtu unaemwamini atakulindia kura yako kwa niaba yako

Mwisho ndugu zangu: Mungu awasimamie katika kutimiza wajibu huu muhimu ili kuwaajiri viongozi wema. Barikiwa Sana kwa ujumbe huu
 
Wakati wa maamuzi huwa sipangiwi
Maana hata mkuu wetu anasema hapangiwi
Tuache sisi na vitutuli vyetu
 
Ni kweli kura ni haki yako ila ili kura yako iwe na thamani pigia CCM.
 
Ni kweli kura ni haki yako ila ili kura yako iwe na thamani pigia Ccm


Pigia Chadema. Shida, kero, karaha, udikteta, manyanyaso, umungu-mtu, ubabe, kiburi, majivuno, visasi, mateso, kukosekana uhuru na haki nk, shida zote hizo za miaka mitano iliyopita zinatosha, Tunataka amani na uhuru ndani ya nchi yetu.

Dec/ 1961 ilikuwa ni siku ya kupata uhuru kutoka kwa mkoloni mweupe na 28/Oct/2020, ni siku ya kupata Uhuru kutoka kwa mkoloni mweusi.

✌🏻✌🏻✌🏻✌🏻✌🏻✌🏻 Uhuru waja.
 
Umeandika vyema sana mleta hoja lakini ili hiyo kura iwe na maana zaidi ni vyema wakamchagua Rais Magufuli, wabunge na madiwani wa CCM ili MAENDELEO yaje kwa speed ya 5G.

October 28th tujitokeze kwa wingi tukamchague JPM.

JPM ANATOSHA
CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
 
Ndugu zangu nawasalim wote wakubwa kwa wadogo kupitia yule atupae pumzi.

Kichwa Cha habari hapo juu chahusika na tukiwa tumebaki na siku mbili kuwapigia viongonzi wetu tuwatakao ,hivyo zingatia yafuatayo...
Kura kwa Tundu Lissu kwa ukombozi wa nchi yetu kutoka makucha ya fisi mkatili.
 
Back
Top Bottom