MTENDAHAKI
JF-Expert Member
- Mar 3, 2011
- 4,013
- 1,447
Watu wanajiuliza sababu za elimu kushuka kiasi cha watoto kumaliza miaka saba ya shule ya msingi pasipo kujua kusoma na kuandika. Hivi kwa wazazi wa leo, tunaokagua madaftari ya watoto wetu (hata wanaosoma English medium) mmeona idadi ya masomo anayosoma mtoto wa darasa la kwanza na la pili.
Naomba niwakumbusha watu tuliosoma miaka ya themanini na mwanzoni mwa tisini. Na leo nagusia madarasa hayo tu kwa watoto wanaosoma English medium.
Kwa mwaka mzima wa darasa la kwanza tulikuwa na masomo 2 yaani Somo la Mwandiko na Hisabati, la ziada lilikuwa ni Kusoma ambalo lilikuwa linatokana na masomo hayo mawili.
Darasa la pili vivyo hivyo tulikuwa na masomo 2 na moja la kusoma. Hakika tulikuwa tunajifunza na tulijua kusoma na kuandika
Hivi sasa mwanangu wa chekechea (Ambako wengine hatukuwahi kubeba daftari kwenda nalo shule wala kurudi nalo) yeye ana madaftari na vitabu 3, kila siku anapewa homework 2
Kila siku kuna meseji anapewa mzazi amsaidie kufanya homework, hivi kama mimi mzazi sijasoma namsaidia vipi,nyie waalimu mna kazi gani
Wa darasa la pili ana daftari saba yaani masomo saba, wa la tatu ana madftari kumi, hivi kweli mtoto mdogo huyu tunategemea asome masomo yote hayo na aelewe?? matokeo ya hakuna kitu mtoto anaambulia,hivyo mzazi kulazimika kutafuta mafunzo ya ziada kwa mwanao.
Nasema tumevuruga elimu yetu sana, ni bora tukarudi kurekebisha tulipoanguka.
Naomba niwakumbusha watu tuliosoma miaka ya themanini na mwanzoni mwa tisini. Na leo nagusia madarasa hayo tu kwa watoto wanaosoma English medium.
Kwa mwaka mzima wa darasa la kwanza tulikuwa na masomo 2 yaani Somo la Mwandiko na Hisabati, la ziada lilikuwa ni Kusoma ambalo lilikuwa linatokana na masomo hayo mawili.
Darasa la pili vivyo hivyo tulikuwa na masomo 2 na moja la kusoma. Hakika tulikuwa tunajifunza na tulijua kusoma na kuandika
Hivi sasa mwanangu wa chekechea (Ambako wengine hatukuwahi kubeba daftari kwenda nalo shule wala kurudi nalo) yeye ana madaftari na vitabu 3, kila siku anapewa homework 2
Kila siku kuna meseji anapewa mzazi amsaidie kufanya homework, hivi kama mimi mzazi sijasoma namsaidia vipi,nyie waalimu mna kazi gani
Wa darasa la pili ana daftari saba yaani masomo saba, wa la tatu ana madftari kumi, hivi kweli mtoto mdogo huyu tunategemea asome masomo yote hayo na aelewe?? matokeo ya hakuna kitu mtoto anaambulia,hivyo mzazi kulazimika kutafuta mafunzo ya ziada kwa mwanao.
Nasema tumevuruga elimu yetu sana, ni bora tukarudi kurekebisha tulipoanguka.