MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 14,588
- 32,361
Wakuu najua sisi wote tunapitia changamoto mbalimbali ila tunapofanya maombi na sala zetu naomba tusisahau kuyaombea makundi yafuatayo;
1. Wanawake wote waliobakiza krismasi chache za kusherehekea kabla ya kutimiza umri wa miaka 40 huku wakiwa hawaoni mwelekeo wowote wa kupata mume ambaye watapata nae mtoto.
2. Watu wote walio kwenye madeni yanayowataabisha na kujionasua imekuwa ngumu. Hakika watu hawa wana stress za hatari.
3. Wanaume na wanawake wote wenye wapenzi/wachumba wasio waaminifu ila inaonekana kama kuna nguvu zisizo za kawaida zinazowafanya waendelee kuvumilia upuuzi badala ya kujiondoa kwenye uhusiano.
4. Wanandoa wanaonyanyaswa na wenza wao.
5. Wanafunzi wanye jitihada lakini ikija mitihani huishia kupata alama za chini yaani wanaokesha lakini hawapandishi.
6. Waajiriwa wote ambao kiuhalisia mishahara yao ni ya kuwasaidia kuzuia tu misiba yao ila haiwezi kufanya maendeleo yoyote.
7. Wajasiriamali wanaopambana ila hupata mabalaa kila mara na kuanguka. Yaani hawajawahi anzisha kitu kikaenda vizuri hata miaka miwili.
8. Wazazi wote ambao wametelekezwa na watoto wao. Watoto wanalala five star apartments ila wazazi wanalala kwenye nyumba za mbavu za mbwa. Pia tuwaombee hao watoto wajitambue.
9. Wafuasi wote wa chama cha Mbowe kwa kupotezewa muda wao huku Sultani Mbowe akifakamia asali.
10. Watu wote kama Mdude ambao wanapigania kitu kinachoenda kunufaisha watu wengine na sio wao.
1. Wanawake wote waliobakiza krismasi chache za kusherehekea kabla ya kutimiza umri wa miaka 40 huku wakiwa hawaoni mwelekeo wowote wa kupata mume ambaye watapata nae mtoto.
2. Watu wote walio kwenye madeni yanayowataabisha na kujionasua imekuwa ngumu. Hakika watu hawa wana stress za hatari.
3. Wanaume na wanawake wote wenye wapenzi/wachumba wasio waaminifu ila inaonekana kama kuna nguvu zisizo za kawaida zinazowafanya waendelee kuvumilia upuuzi badala ya kujiondoa kwenye uhusiano.
4. Wanandoa wanaonyanyaswa na wenza wao.
5. Wanafunzi wanye jitihada lakini ikija mitihani huishia kupata alama za chini yaani wanaokesha lakini hawapandishi.
6. Waajiriwa wote ambao kiuhalisia mishahara yao ni ya kuwasaidia kuzuia tu misiba yao ila haiwezi kufanya maendeleo yoyote.
7. Wajasiriamali wanaopambana ila hupata mabalaa kila mara na kuanguka. Yaani hawajawahi anzisha kitu kikaenda vizuri hata miaka miwili.
8. Wazazi wote ambao wametelekezwa na watoto wao. Watoto wanalala five star apartments ila wazazi wanalala kwenye nyumba za mbavu za mbwa. Pia tuwaombee hao watoto wajitambue.
9. Wafuasi wote wa chama cha Mbowe kwa kupotezewa muda wao huku Sultani Mbowe akifakamia asali.
10. Watu wote kama Mdude ambao wanapigania kitu kinachoenda kunufaisha watu wengine na sio wao.