Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe leo anafanya mkutano wa hadhara katika Jimbo la Kisesa mkutano unaotajwa kusubiriwa na hamu kubwa hasa baada ya kutangaza kuwanyima huduma za pembejeo za kilimo kama wananchi hao wataendelea kuungana na mbunge wao Luhaga Mpina kuwa kulaumu wakulima kuuziwa dawa feki za kupulizia wadudu wa pamba na kuendelea kulalamikia makato wanayokatwa wakulima na kulalamikia bei ndogo ya pamba.
Jambo la kusisimua kubwa mkutano huo Bashe alipanga kuzungumza na wananchi wa Kisesa lakini Bashe akafanya ubunifu wa kuwagharamia posho, chakula na usafiri wananchi wa majimbo mengine ya Mkoa wa Simiyu na mikoa jirani kwenda Jimbo la Kisesa ili kuufanya mkutano huo uonekane umejaa watu wanaompinga Mpina.
Bashe amewagharamia wananchi kutoka ngazi ya vijiji wengi wao wakiwa viongozi wa CCM ngazi ya matawi ambapo kila kijiji kinatoa majumbe 20 ili wafurike kwenye mkutano huo huku waratibu wa mkutano huo wakidaiwa kuwaahidi wananchi hao posho ya shilingi 1aki moja kila mmoja, lakini pia wakigharamiwa usafiri wa mabasi na kupewa chakula.
Baadhi ya viongozi wa CCM wamempongeza Bashe kwa ubunifu huo wa kualika wananchi wa majimbo na wilaya nyingine kwenda Kisesa kwa na kubainisha kuwa ndiye Waziri wa kwanza kuja na ubunifu huo.
Tumeshatembelewa na mawaziri wengi hapa Meatu, lakini hatujawahi kuona waziri anaandaa utaratibu mzuri kama huu wa kusafirisha wajumbe wa ccm na kuwandaalia posho ya laki 1, lakini pamoja na ubunifu huo tunaomba bashe asimamie kikamilifu ahakikishe hizo fedha alizopanga kutulipa hiyo laki 1 tulipwe hiyo hiyo isije ikapigwa na viongozi wetu wa chama ngazi ya wilaya maana nao hawaamiiniki sana" alisikika mjumbe kutoka JImbo la Meatu anayekwenda Kisesa kwenye mkutano.
Mkutano huo wa Bashe unadaiwa kualika watu kutoka Itilima, Maswa, Meatu, Bariadi, Busega, Kishapu, Igunga na wengine kutoka maeneo ya Mwanza na Dodoma.
Jambo la kusisimua kubwa mkutano huo Bashe alipanga kuzungumza na wananchi wa Kisesa lakini Bashe akafanya ubunifu wa kuwagharamia posho, chakula na usafiri wananchi wa majimbo mengine ya Mkoa wa Simiyu na mikoa jirani kwenda Jimbo la Kisesa ili kuufanya mkutano huo uonekane umejaa watu wanaompinga Mpina.
Bashe amewagharamia wananchi kutoka ngazi ya vijiji wengi wao wakiwa viongozi wa CCM ngazi ya matawi ambapo kila kijiji kinatoa majumbe 20 ili wafurike kwenye mkutano huo huku waratibu wa mkutano huo wakidaiwa kuwaahidi wananchi hao posho ya shilingi 1aki moja kila mmoja, lakini pia wakigharamiwa usafiri wa mabasi na kupewa chakula.
Baadhi ya viongozi wa CCM wamempongeza Bashe kwa ubunifu huo wa kualika wananchi wa majimbo na wilaya nyingine kwenda Kisesa kwa na kubainisha kuwa ndiye Waziri wa kwanza kuja na ubunifu huo.
Tumeshatembelewa na mawaziri wengi hapa Meatu, lakini hatujawahi kuona waziri anaandaa utaratibu mzuri kama huu wa kusafirisha wajumbe wa ccm na kuwandaalia posho ya laki 1, lakini pamoja na ubunifu huo tunaomba bashe asimamie kikamilifu ahakikishe hizo fedha alizopanga kutulipa hiyo laki 1 tulipwe hiyo hiyo isije ikapigwa na viongozi wetu wa chama ngazi ya wilaya maana nao hawaamiiniki sana" alisikika mjumbe kutoka JImbo la Meatu anayekwenda Kisesa kwenye mkutano.
Mkutano huo wa Bashe unadaiwa kualika watu kutoka Itilima, Maswa, Meatu, Bariadi, Busega, Kishapu, Igunga na wengine kutoka maeneo ya Mwanza na Dodoma.