Elections 2010 Kyela elections!

Status
Not open for further replies.

Mkuu Sikonge,
Rafiki yako Mwakalinga WanaKyela wamemuingiza mjini ama wamemkaribisha nkayani. Kabla hata hajakuwa Mbunge, kuamua kujenga ghorofa, kuanzisha kituo cha radio na kugawa jezi zilizoandikwa Kyela FM aliona ndio maendeleo, hiyo si rushwa outright?! Angelifanya hayo bila ya kuwa na agenda yoyote behind tungelimwita ni mpenda maendeleo ya Kyela lakini kujenga na kugawa vitu halafu kutaka Ubunge in return ni rushwa tu.

Mwakyembe ni moto wa kuotea mbali! Hata kama angelikuwa anapigiwa kura za maoni na Watanzania wote angepeta tu bila ya kutoa jasho kujinadi. Kama walikuwepo wapambe wa Mwakyembe ni katika kulinda haki za chaguo lao asidhulumiwe wala kuhujumiwa kwa sababu tunaambiwa tayari 'Mmasai" mmoja alishasema kama Mwakyembe akirudi kwenye ubunge basi yeye si Mmasai! Tunasubiri wamuengue Dr. Mwakyembe waone kitakachotokea. Nawapa tano ndugu zangu wa Kyela kwa kuonyesha ushujaa dhidi ya Mwakipesile na genge lake. Tunataka Mkoa wa Mbeya na Tanzania isiyo na majungu wala visasi.

Mbona mwanzishaji habari hii hajaeleza jinsi ambavyo katika kampeni mahasimu wa Mwakyembe walijaribu kutumia ujanja wa kutaka Dr. Mwakyembe aanze kuzungumza ili watakapozungumza akina wagombea 'wao' wampiku. Matokeo yake, baada ya kuzungumza Dr. Mwakyembe watu walikuwa wakitawanyika wakidai tayari shughuli imekwisha na wagombea wengine kuachwa wakihutubia mashabiki wao tu! Ilipodhihirika hivyo, Dr. Mwakyembe akawa anawekwa kuzungumza mwisho ili watu wasiondoke. Haikufua dafu, baada ya kuzungumza wananchi walisema waziwazi kwamba tumeishakupitisha MBUNGE WETU Mwakyembe! Pia, sehemu zingine Dr. Mwakyembe alikuwa anazuiwa na wazee kuzunguza wakidai kwamba hana haja ya kuzungumza kwa sababu tayari keshapita!

Mkuu Sikonge,
Kama tunaitakia nchi hii mema kwa dhati tuwashabikie watu wa aina ya Dr. Mwakyembe warudi bungeni kuleta changamoto waliyokwisha kuionyesha kwa kung'oa visiki kwa maslahi ya Taifa. Naamini kabisa kama Dr. Slaa atafanikiwa kuupata urais, watu wenye msimamo kama Dr. Mwakyembe watampa support kubwa katika masuala yanayohusu maslahi ya taifa. Kwa maana nyingine msimamo utakuwa TAIFA MBELE, vyama nyuma!
 
Mkuu nilikuwa sijagundua kumbe ukijumlisha George na Elias Mwakalinga, Mwanjala na dada Mwamunyange jumla yao ni 4501 bado wanashindwa na Dr Harrison M, labda kama wangechukua na zile kadi 10,000 hahahahahahahahaahhhh
.

Masanilo.
Karibu tena nyumbani jf.Ulipotelea wapi?.Nilifikiri umekuja Mwanza kutafuta ubunge.Badala yake sikukusikia wala sikukuona .
Karibu sana hapa Nyakato-mwanza
 
Mwa Njelwa, sasa mbona unakuwa mbaguzi?Kyela si iko TZ?wengine wame oa/kuolewa na wachaga,wapare,wahaya,etc lakini in any case hii ni wilaya iko TZ kama inabidi kusaidiwa(kimawazo na kiuchumi) sio lazima ifanywe na wana Kyela kwa sababu hata kama ingekuwa ina dhabhabu isingeliwa na wana Kyela tu.
Nadhani una habari kuwa mchele 1st class TZ nzima unatoka katika maeneo mengi lakini Kyela iko No. 1 au 2?na wa TZ wote wanaula na kuishi.
Kwa hiyo jukumu la kuizungumzia sio lao tu.
Shukuru mungu wilaya yako haina baya ndio maana haizungumziwi kama inalo ilete hapa-si ndio penye jamii?:tape:

 
Hizi kura 15,336 mhhhh!!!! Ngoja wazihakiki akina Mwakalinga maana naanza kuogopa kuwa Kyela nzima ilipiga kura na kuwa jimbo lenye wana CCM waaminifu sana. Sitashangaa wakiibua majina hadi ya akina Marehemu Mwaka............

Asiyekubali kushindwa si mshindani. Get a life dude!
 
Kitu gani wakati mmemshinda? Binadamu tuna tabia mbaya sana. Rafiki yako akishindwa au kufeli maisha, mtihani, uchaguzi basi unamkimbia. Mimi hilo sifanyi hata kidogo. . Kupanga ni kuchagua. Uamuzi wa Wanakyela uheshimiwe.

Nimekuelewa Mkuu!!!

Najua huu ni wakati ambao Mwakalinga anakuhitaji zaidi, hakika u rafiki wa kweli.
 
.

Mbona unaongelea yaleyale yaliyosemwa na wenzio?.Hakukuwa na lingine uko kyela?
 
.

Masanilo.
Karibu tena nyumbani jf.Ulipotelea wapi?.Nilifikiri umekuja Mwanza kutafuta ubunge.Badala yake sikukusikia wala sikukuona .
Karibu sana hapa Nyakato-mwanza

Teh teh teh nilikuwa kwenye kura za Maoni mkubwa! Nilienda mkoa mmoja wapo wa pembezoni nilikofanyia kazi nimeambulia aibu tu

Ila mkuu naogopa sana memba wapya usije kuwa ni yule mwenye IDs mingi kama Mkulima, Muheza ama Buc.... ukachafua hali ya hewa Lol

jilala
Join Date Mon Aug 2010
Posts 6
Thanks : 0
Thanked 1 Time in 1 Post
 
ujumbe wangu kwa Mwakalinga ni kua, aende Kyela akiwa na agenda za wazi wazi, ajitahidi kuwaambia watu wazi na ukweli agenda yake juu ya matatizo ya kitaifa Ufisadi na Umasikini ukiwa mmoja wapo, aache kuwa karibu na kina Lowassa na mafisadi papa wengine.
atuambie kua kwanini wanakyela wasiamini kua yale yote aliyoyapeleka kule ilikua danganya toto akitaka kuchaguliwa kwa jina la kuleta maendeleo ?
Mwakalinga umeshindwa kwa jina la haki na Demokrasia, nenda ukafie mbele(Kisiasa) , umeshindwa kutuaminisha kwanini wewe ni bora kuliko Mwakyembe kwa maana ya Mbunge na Majukumu ya Mbunge kama sheria na taratibu za nchi zinavyosema.
Mwakyembe Hongera sana.
 
i) Mbunge aliyopo alikuwa na mkakati wa muda mrefu kushinda pamoja na kuhasisi mashina ya wakeleketwa jambo ambalo wagombea wengine walilisahau na kusubiri fair play dakika za majeruhi. Imekula kwao.

Kushinda ni mpango mkakati pamoja na upeo wa timu ya wanakampeni unayounda. Dr. Mwakyembe timu anayo na walijua ushindi wa mezani hauko upande wao wakaenda chaka they manage to produce the result.

ili mzazi uliliacha.
 
.

Katabazi.
Kwa utafiti wako wa harakaharaka, hivi populations ya kyela ni ngapi?.
Kinachonishangaza hapa ni hiyo idadi ya wana ccm waliojitokeza kupiga kura ni 20,000 na je ambao hawakupiga?
 
.
No.Mimi ninaitwa magoli kwa jina lingine.Lakini bahati mbaya mods walinifuta kutokana na sababu zilizonje ya uwezo wao.Kwa hiyo nimerudi na ID nyingine na nimeamua kuwajulisha hili jambo.Wakinifuta tena,basi nita seti mambo mengine kwenye internet.Duh,Pole sana.umetumia demokrasia yako na usikate tamaa.Jaribu tena 2015 or jaribu chama kingine.
 
.
No.Mimi ninaitwa magoli kwa jina lingine.Lakini bahati mbaya mods walifuta kutokana na sababu zilizonje ya uwezo wao.Kwa hiyo nimerudi na ID nyingine na nimeamua kuwajulisha hili jambo.Wakinifuta tena,basi nita seti mambo mengine kwenye internet.

Asante mkubwa! Nimejifunza kitu JF hizi Ghost name tuna ziabuse sana! Sijibu PM wala mtu akitaka nijua zaidi ya Masa Kugema.....maana baadaye jamaa huja na ID mpya akamwaga upupu na wewe ulimwamini na kumwambia mimi kwa Jina ni John Shibuda na ninatokea Buchosa. hahahaha

Tuache hayo! bila shak umefurahia Mwakyembe kushinda mchakato maana huyu atamsaidia raisi wetu Dr Slaa kujenga heshima na mendeleo maana wote wanapinga Ufisadi
 

Mkuu,

Tatizo lako unamentality ya Wanyamwezi ya kuwa nyoronyoro/upole usio na tija ambao umefanya RA ameweza kuwarubuni kwa pesa hadi wakamuangusha mpambanaji Selelii badala ya Wanyamwezi hao kuona fahari ya kuwa na Mnyamwezi kama huyo shujaa aliyetetea maslahi ya Taifa wakati wa sakata la Richmonduli! Wanyakyusa hawako hivyo, wakishakudharau basi hata uje na majisenti huambulii kitu midhali wao wameishaamua wanachokitaka. Hili liwe fundisho kwa hata wanasiasa wanaowania urais.

Pia hata kama Mwakalinga atahamia CHADEMA haitamsaidia Dr. Slaa kwa sababu Mwakalinga atakosa. Wanyakyusa walishaamua Mwakyembe wao apite atapita tu.
 

Sikonge,
Kwa hilo nakubaliana nawe, kwamba wewe ni mtani wetu sisi wanyakyusa hili ni zuri kwani tunadumisha mila. Naomba nikupe mambo mawili tu ambayo Dr kayasimamia akiwa MP. La kwanza ni la usambazaji wa umeme vijijini tangu mwaka 2005 mpaka sasa umekuwa wa kasi nzuri. Pili kiwanda cha stamico wafanyakazi walikuwa hawajalipwa kwa miaka mingi, mbunge wao Dr. Mwakyembe aliwatetea mpaka wakalipwa. ( Ukitaka kuota manundu nenda pale kawaambie wale wafanyakazi kwamba Mwakyembe hafai)

Nina mpango wa kuja Sikonge kugombea jimbo, kwani njie watani zetu (wasukuma) naona RA anawakimbiza.
 

Ningemshauri ndugu yangu Mwakalinga asiende CHADEMA maana koti la Rostam na Lowassa atakuwa bado analo, litakuwa kosa kubwa kama CHADEMA watampokea. Chama kinachomfaa ni CUF maana wanaendana sera!
 
Wewew lazima unatoka Ileje.....
Kyela sasa ni halmashauri ya mji....hupewi hadhi hiyo bila kufikia vigezo kadhaa......
Kwa maana nyingine, Kyela inafanana na Njombe , Rungwe nk
Ongea kwa point siyo kukurupuka.

Nani aliyekwambia kuwa ukiwa na halmashauri maana yake mmeendelea? Inawezekana Mwakalinga akawa anachangia mapato ya halmashauri kiasi kikubwa sana kuiwezesha ku-qualify kuwa halmashauri huku wengine mkiwa choka mbaya kama hali halisi ilivyo! Ukinisoma vema, nina maana ni muda muafaka kwa wana Kyela sasa kuanza kufikiria maendeleo yenu kama wananchi na si kukimbilia kujenga Mbeya na Dar na mikoa mingine.

Chagueni mada za kuendeleza Kyela na si ubishi wa Mwakalinga, Mwakyembe na wengine....

Mwingine anaongelea mchele,,, du! Hiyo nayo kali zaidi.
 
.

Katabazi.
Kwa utafiti wako wa harakaharaka, hivi populations ya kyela ni ngapi?.
Kinachonishangaza hapa ni hiyo idadi ya wana ccm waliojitokeza kupiga kura ni 20,000 na je ambao hawakupiga?

Wengine tulitoka Mbeya mjini,Dar es Salaam nk....kule ni kwetu bana...hata Mengi alihama kisutu kurudi moshi lakini makazi yake Dar..usipotee kulinganisha census figures na hii mambo....mgombea mmoja katoaka London even!!!!!
 

lakini Mwakalinga anachangia bila kutegemea kurudisha ? nothing for free, sasa anataka kurudisha tumichango twake, anataka wampe Ubunge.
 
Ningemshauri ndugu yangu Mwakalinga asiende CHADEMA maana koti la Rostam na Lowassa atakuwa bado analo, litakuwa kosa kubwa kama CHADEMA watampokea. Chama kinachomfaa ni CUF maana wanaendana sera!

CHADEMA hatafit, mi ningemshauri aende kule TLP, huenda atafit.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…