Kyerwa, Kagera: Waziri Mkuu Kassim Majaliwa agoma kufungua ofisi ya TANESCO kutokana na gharama kutoendana na ujenzi uliofanyika

Majengo ya Tanesco yanatumia gharama kubwa Sana bila sababu za msingi ..

Ni ajabu Serikali imeshindwa kuwa na standards za gharama za majengo kwa taasisi zake ..
 
Kwa ujinga wako huo huo
Inaonyesha unajenga na material ya cheap na low quality ... Lkn kama unaelewa gharama za vifaa kwa sasa nafikri utaelewa
 
Bati 8 unless unajenga banda la kuku
 
Bibi kashawaambia yeye hakusomea construction engineerin na kwamba hawezi kushuka chini kutizama matumizi ya kodi za walala hoi wake, sasa mnataka nini tena? Acha wapige tena natamani wapige zaidi. So far, mbona huku juu ndo wapigaji wamerudishwa ofisini na hakuna makelele? Acheni watu wawe matajiri make sera yetu sahivi ni CHUKUA CHAKO MAPEMA
 
Majengo ya Tanesco yanatumia gharama kubwa Sana bila sababu za msingi ..

Ni ajabu Serikali imeshindwa kuwa na standards za gharama za majengo kwa taasisi zake ..
Hii hoja ya msingi sana majengo ya umma wanapaswa kuwa na design inayofanana kutegemea na wizara, mahitaji ya ofisi na geography ya eneo majengo hayo yanajengwa.

Anyway mimi siyo mtaalamu wa majengo lakini mianya ya upigaji ni mingi sana nchi kiasi cha nchi kugeuka shamba la wahuni.
 
Haiingii akilini kila Halmashauri inajenga majengo kwa design yao mwisho wa siku hakuna gharama inayojulikana Sasa hapa Serikali inazingua.

Kama ulivyosema taasisi chini ya Wizara fulani ziwe na majengo yanayofanana ..

Sasa unakuta BoT za Kanda kila moja ina design yake,majengo ya wakuu wa Wilaya,mikoa nk hii haina maana kabisa..
 
Tatizo ni hao wanasiasa uchwara, wanajenga kwa kutumia kitu wanaita force account wadala yakitumia wakandarasi eti ni wezi! Majaliwa ni disgrace kwa taifa hili.
 
Binafsi naweza nikasema ni sawa kwa kile kibanda cha M7 kwa sababu
Gharama za ujenzi sass ivi zipo juu mnoo
Kama una experience ya ujenzi wa sasa utaelewa tub
Acha basi mkuu m7 unaijua Bwashee?
 
Nawapongeza sana hao waliohusika hapo!

Kama kina Ruge wamefisadi mabilioni lakini wanachiwa na watu tunashangilia kwamba walionewa, kwanini wengine wasifisadi?

Mtu yeyote mwenye nafasi kula sepa.
Na hii Ndio sahihi...maana ukinyoosha mambo ili masikini unaowaonea huruma waone uafadhali,,watakutukana ukifa,,na Wenye naZo uliowaharibia watakuwinda ufe...

Kila mtu katika nafasi yake na apige..apige kweli kweli
 
Binafsi naweza nikasema ni sawa kwa kile kibanda cha M7 kwa sababu
Gharama za ujenzi sass ivi zipo juu mnoo
Kama una experience ya ujenzi wa sasa utaelewa tub
Msingi laki 4
Madirisha na mlango laki 8
Bati laki 1 na 80
Gypsum na rangi laki 3
Tofali na cement na mchanga 1m
Fundi laki 4
Mbao laki 2

Tujumlishe.

Ni kama Tsh 3, 280,000/=
 
Kuna majengo mengine ni ya umma lakini yanajengwa kama lodge.

Inapaswa kila wizara iweke standard za majengo ya wizara ikiwemo na gharama za jengo husika na gharama zipangwe kufuata ofisi inayojengwa mkoani iwe juu kidogo kuliko za wilayani.

Siyo kila mtu anajifanyia anavyotaka matokeo yake ni watu kuendelea kujenga vibanda vya walinzi kwa milion 7.

Nchi hii inakatisha tamaa sana.
 
Ukiona jengo la Geita TC utadhani ni Hotel,,hii haikubaliki
 
Ukiona jengo la Geita TC utadhani ni Hotel,,hii haikubaliki
Mambo mengi yanaenda bila taratibu kuna njia nyingi za kudhibiti huu wizi mdogo mdogo kwenye miradi kama huu wa Kyerwa.

Serikali yetu iko very disorganized kwenye mambo mengi kila mmoja anajifanyia anavyotaka.

Mathalani hata magari ya viongozi wangeweka standards huko LGAs ma V8 yasitumike zitumike gari zingine tu.

Hivyo hivyo kwenye majengo pia
 
Huyo maza mwenye mask kama Subzero amevaa koti jeusi anaonekana mpigaji kwa kumcheki tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…