Kylian Mbappe dhidi ya Gadiel Michael, tubadilike Watanzania

ibanezafrica

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2014
Posts
7,261
Reaction score
6,553
Leo hii dunia nzima inamuongelea Kylian Mbappe(23) kwa yale aliyoyafanya makubwa juu ya taifa lake katika fainali za kombe la dunia na kufanikiwa kuifikisha nafasi ya pili timu ya ufaransa.

Leo hii Gadiel Michael(26) anatumikia adhabu ya mechi kadhaa pamoja na faini ya laki 5 kwa kosa la kulazimisha kuingia uwanjani saa 4 asubuhi na kwenda kumwaga ushirikina uwanjani.

Unajiuliza soka letu linaelekea wapi? Ni lini Gadiel michael atafikia level za akina Mbappe?

Viongozi wa timu yake hadi leo hawajakanusha tuhuma zile na huenda ni wao ndio watailipa faini hiyo.

Je tuamini alitumwa na klabu kufanya yale?

Unajiuliza nini vision za vilabu vyetu?isije kuwa tunaigiza tu soka.

Shime kama nchi tubadilike tuwekeze kwenye vipaji viongozi wapunguze ulaji tujiwekee malengo..maana bila malengo hakuna cha maana tutakachofanya tutabaki kupiga domo tu na kubakia kusindikiza tu miaka nenda rudi.

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
 
Bado unalo hilo,? Kwani mzee Mpili alikua anawafanyia kazi gani Yanga?
Simba na Yanga wote washirikina...
Mzee mpili mzaramo maneno mengi na mikwara tu hana uchawi wowote

Simba imehusika ktk matendo mengi ya kishirikina toka enzi za akina hamis tambwe hadi miaka hii.

Yanga umesikia lini anashikwa uchawi zaidi ya usajiri bora?

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu ushirikina kwenye soka la Bongo ni kawaida....kuna ile mechi ya fainali ya FA iliyochezwa kigoma Simba na Yanga.

Simba walifanya yao uwanjani kisha wakaweka ulinzi Yanga wasiingie,Yanga walienda uwanjani mida ya usiku kama saa2 hivi kufika getini wanakuta ulinzi wa vijana wa Simba, zilitokea vurugu kubwa sana.

Simba amesharoga na Yanga anataka kuingia kuroga....warogaji wa Simba walikuwa vijana wa Kigoma,Yanga wao walikuwa jamaa kutoka Dar maana walikuwa wanachonga sana hadi kutishiana eti vijana wa Simba wasikanyage Dar,watakiona cha moto....nilicheka sana aise!

Simba walifanikiwa kulinda geti mpaka asubuhi maana walikuwa na vijana wa KAZI,Yanga walipeleka vibonge wala chips wanaume wa Dar wakafeli kuroga.

Ukiacha ya Mbape na Gadiel maiko....waulize Tifua Tifua wale vijana waliocheza fainali ya Copa coca cola kule Brazil na kina Neymar mbona hatukuwaona hata ligi ya madafu walipotelea wapi?
 
Badala ya kuwa professional mnatumainia ndumba..msitarajie kufika mbali.
Hakuna mechi inachezwa bila mganga kucheza mechi hapa katika ardhi ya kitanganyika.

Hata wachezaji wana amini katika kuroga ushinde mechi kuna mechi moja Mayele kakosa sana Magoli,akaenda kuishika nyavu ya goli akiamini kuna uchawi.
 
Bado unalo hilo,? Kwani mzee Mpili alikua anawafanyia kazi gani Yanga?
Simba na Yanga wote washirikina...
Bora angeandika mbape dhidi ya kabwili maana hilo ni kubwa kuliko gadiel Maiko na mume wake mukoko alisema wapo wengine 6
 
Sports academy zinahitaji back up yakutosha,bidii,uzalendo na kujituma cha ajabu kinachofanyikaga tu UMISETA ni full rushwa na kubebana na mambo ya ajabu sana kwa mwendo huo kutoboa ni ngumu sana.
 
Usiongelee kwenye soka tu. Panua mawanda ya hoja yako. Ni sekta au fani gani ambako tunafanya vizuri na kwa viwango vinavyotakiwa? Si mifumo yetu yote imeoza na kila kitu kinakwenda ndivyo sivyo? Nini kinakufanya uamini kuwa kwenye soka kutakuwa na unafuu wakati mambo yetu ni shaghalabaghala tu?
 
Mbappe.....daaa matumbo ya wanawake si ya kuyadharau aisee...yanabeba vitu vya maana sana❤
 
Hujacheza mpira ndio tatizo,soka letu bila ndumba haliendi
 
Na jezi za mazindiko
 
Bado unalo hilo,? Kwani mzee Mpili alikua anawafanyia kazi gani Yanga?
Simba na Yanga wote washirikina...
Elewa point, tunaquestion mtazamo wa mchezaji kuhusu mpira, Mpili si mchezaji.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…