Kylian Mbappe dhidi ya Gadiel Michael, tubadilike Watanzania

Bora angeandika mbape dhidi ya kabwili maana hilo ni kubwa kuliko gadiel Maiko na mume wake mukoko alisema wapo wengine 6
Mkuu bila shaka unashiriki haya matendo maana comments zako huwezi acha kutamka hizo tabia maana kinacho mtoka mtu ndio kilicho moyoni mwake
 
Nilitarajia Gadiel Michael angekuwa ni mmoja wa walinzi bora kabisa wa upande wa kushoto.
Alifanya maamuzi sahihi kabisa pale alipolazimisha kuhama kutoka Azam, kwenda Yanga! Maana alipokuwa Yanga, aliaminiwa! Na hivyo alicheza kwa kiwango kikubwa, kiasi cha kujihakikishia namba kwenye timu ya Taifa.

Kuhamia kwake simba, kwa upande wangu lilikuwa ni kosa kubwa sana ambalo aliwahi kulifanya katika maisha yake ya mpira. Kwa sababu tayari simba ilikuwa ina mlinzi wake tegemeo (Mohamed Hussein Zimbwe Jr.).


Kilichotokea baada ya uhamisho wake, ndiyo hiki sasa cha kubadilishiwa majukumu ya kutoka kuwa mchezaji wa kutumainiwa, na kuwa mganga wa timu. I wish angevumilia tu zile changamoto za wakati ule pale Yanga. Hata mwenzake Ibrahim Ajib naye hali si hali pale Azam fc.
 
Hakuna mechi inachezwa bila mganga kucheza mechi hapa katika ardhi ya kitanganyika.

Hata wachezaji wana amini katika kuroga ushinde mechi kuna mechi moja Mayele kakosa sana Magoli,akaenda kuishika nyavu ya goli akiamini kuna uchawi.
Nigeria.ghana.algeria.guinea nk
Wanafikaje world cup?
Fukijisahau na hizi ndumba aisee
 
Masuala ya uchawi ni ya kiimani tu ni kawaida ya binadamu yoyote kutafuta kitu cha kuwekea imani pale ambapo uwezo wake unafika mwisho au anapokua na hisia hicho kitu kinampa bahati au kumwezesha kushinda kwa namna fulani., tunaona kaka anaingia uwanjani ndani kavaa rozali inaonekana sawa cha kushangaza akiingia mchezaji kavaa hirizi atasakamwa wakati kimsingi wote wamefanya kitu kile kile tu ila kwa imani tofauti anaeenda kanisani kuomnewa kabla ya mechi ana tofauti gani na anaeenda kwa mganga? zote ni imani tu hazina impact yoyote katika uhalisia juzi argentina wachezaji walivaa rebons nyekundu miguuni na kipa alivaa mkononi wakiamini itawapa bahati iyo ina tofauti gani na mchezaji anaeingia uwanjani akiwa amevaa hirizi akiamini itampa bahati? Majuzi tu pogba alikua na skendo ya kutumia ushirikina na ni mchezaji mkubwa tu hapa duniani. As long as mtu hajasababisha maafa yoyote binafsi sioni umuhimu wowote wa kukomalia suala la imani za watu kila mtu ana uhuru wa kuamini anachokitaka cha muhimu tu ni kuweka sawa mifumo yetu ya soka kuanzia ngazi ya watoto, vijana mpaka wakubwa baada ya hapo anaeamini katika ukristo, uislamu, uchawi n.k as long as avunji kanuni yoyote basi imani yake iheshimiwe hao mbappe na gadiel michael wamekuzwa kisoka katika msingi tofauti kabisa uwezi ukatumia kigezo cha ushirikina pekee kusema ndo sababu ya mmoja kuwa na mafanikio kushinda mwenzake hata kama mbappe angeonesha vitendo vinavyoashiria ushirikina bado kimafanikio angekua juu ya gadiel michael kwa sababu msingi waliokuzwa kisoka ni mbingu na ardhi.. by the way nimeshtuka kujua kwamba gadiel michael ana miaka 26
 
Una afiki mchezaji kwenda kunyunyuza unga uwamjani?
 
Una afiki mchezaji kwenda kunyunyuza unga uwamjani?
Kwenye mikutano ya dini watu wanakanyaga mafuta wengine wanazamishwa kwenye maji kwamba ndo wanabatizwa na wanakufa mbona mikutano ya dini haikemewi wala kupigwa marufuku alfu wewe unasema kumwaga unga tu ambao hauna madhara yoyote.. kama huo unga hauna madhara yoyote basi inaweza ikatumika kama mbinu ya kucheza na saikolojia ya wapinzani tu., kwenye game na caf confederation msimu jana simba aliwasha moto uwanjani je alishinda? Wachezaji wengi tunaona wakiingia uwanjani wanapiga ishara ya msalaba au wananyanyua viganja vya mikono juu kama kushukuru au kupokea kitu baraka kutoka kwa Mungu wao ni matukio na ishara zinazofungamana na na imani tu ila hazina impact yoyote kiuhalisia maana sometimes bado timu zao zinafungwa point yangu inakuja inabaki pale pale as long as kitendo husika hakina madhara yoyote na hakuna sheria iliyovunjwa basi imani ya mtu iheshimiwe, tusuke mifumo yetu ya soka kuanzia ngazi ya watoto mpaka wakubwa kwanza baada ya hapo mchezaji akiamini katika ukristo, uislamu, uchawi, uganga n.k iyo ni juu yake muhimu tu iyo imani yake isivunje kanuni au kuleta madhara kwa wengine
 
Kuongoza kundi ni mafanikio? [emoji23][emoji23]Tuna safari ndefu
Kumbe siyo mafanikio? Unavukaje hatua inayofuata kama haujafuzu makundi? Mlianza na kusema hakuna kombe la robo fainali ya Club bingwa lakini hamjawahi kutuonesha kombe la unbeaten....
 
Upo sahihi,niligusia hili moja tu la soka baada ya hamasa ya WC

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
 
Usifananishe Rozari na Hirizi

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
 
Nadhani ingekuwa vyema kujadili Yanga iliyofanya usajili wa pesa nyingi halafu bado wachezaji wake hawana performance ya wachezaji wa Simba yenye first 11 iliyojaa wenyeji zaidi.
Performance ipi unayoongelea mkuu? Maana so far yanga anaongoza ligi kuu kwa tofauti ya point 4 dhidi ya uyo unayesema kamzidi performance
 
Inayo performance ya magoli ya offside, penalt za kupewa na bahasha nono
Leo tumewafunga coast 3-0
Ni offside?
Bahasha?
Penati?

Mara zote hizi tumewafunga nyie simba kuanzia Ngao
Ni offside?
Ni bahasha?
Penati?

Club africaine ya tunisia tuliifunga kwao

Ni offside?
Ni bahasha?,
Ni penati?

Jamani fanyeni sajili za kutulia hapo ndio mnapokoseaga na hata sasa mmejiingiza kwa saidor mmeshapotea,kwani hamna scouting ya nguvu⁸
Yaani nyie mnaokotezaga tu wachezaji baadala ya kukaa na kupanga na kutoka nje ya nchi..masubiria tu mara Akpan,mara Kibu,mara Deejan na sasa Saidor...mchezaji ambaye bado ana mapenzi na wananchi kwa kauli yake mara ya mwisho,mna hakika atajitoa 100% siku tukikutana? Mnafeli sana nyie kwenye sajili

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…