La Bandari ya Bagamoyo kama ni kweli basi ni ukombozi

La Bandari ya Bagamoyo kama ni kweli basi ni ukombozi

Mbagamoyo

Member
Joined
Dec 14, 2020
Posts
18
Reaction score
49
1610113353084.png

Asalam ndungu zangu!

Nimepitia mitandao naona suala la Bandari ya Bagamoyo limeibuka upya. Limeibuka kwamba limepata ufunmbuzi na litatimia. Faida na hasara zake.

A) Faida
1. Uhamishaji wa teknolojia kwa haraka.

Tuliambiwa Kuna viwanda takribani 700 kwenye ukanda wa Bandari na maeneo jirani. Hi ni fursa tuikimbilie.

2. Ajira
Tuliambiwa uzalishaji mkubwa wa ajira. Ajira rasmi na zisizo rasmi. Zisizo rasmi Zina nguvu kubwa sana. Tuzipe nafasi.

3. Utandawazi kimataifa

Bidhaa za Tanzania zitauzwa nje kwa wingi zaidi. Bandari ya Bagamoyo ni kama wazo pana la zile economic zones etc.

Hasara.

1. Hofu
Haina sababu.

2. Wivu
Sifa itaenda kwa nani. Ni no progressive approach.

3. Kufa kwa Bandari kongwe za Dar, Tanga, Mtwara.

Ni ukosefu wa Taarifa. Bandari Bubu Tanzania huenda zinafanya kazi zaidi ya Bandari rasmi.

Tutafiti. Tuamue, Tusonge mbele

Zaidi soma:
 
Jiwe ndiye aliyeikataa hadharani. Sasa kapigwa shule imemuingia kichwani?
 
Ndoto nzuuuri isiyo na tija. Dead like dead.
 
Jiwe ndiye aliyeikataa hadharani. Sasa kapigwa shule imemuingia kichwani?
Nani kampa hilo darasa?Jiwe anajifahamu mwenyewe, akiona sifa/manufaa yake binafsi hayapo hawezi idhinisha jambo lolote hata mpige mayowe vipi.
 
hakuwahi kukataa muwe mnasoma mambo kwa utulivu.

alisema lisitishwe lipitiwe upya kwa maslahi ya pande mbili,sio moja tu.
Ushawahi kusikia 10%?! Malizia mwenyewe....stukaaaa
 
Hawa wachina ni wabaya sana serikali izidi kuwakumbatia tu.

Kipindi kile magu amekula kiapo kitu cha kwanza kustopishani hiyo bandari.

Wa walitoka hadi tpa wakaeleze hasara na masharri wachina walioweka kuwa kwa sisi tz tukikubali tuu tumepigwa dole. Naona wachina washaanza kumkolombeza mtu huko leo hii atakubali.

Sasa kule mwanzo alikataa nini au ilikuwa danganya toto.
 
Bandari ya Bagamoyo ni muhimu sana kwa 'HUGE+" Economy of tanzania LAKINI ni baada ya mikataba kubadilishwa baadhi ya vifungu kwani baadhi ya vifungu vilikuwa vya hovyo kweli
 
Nadhani Mama Yetu atalifanyia kazi hili

The white elephant bagamoyo port
 
Back
Top Bottom