Laana ya mzee Membe itaendelea kumtafuna Zitto Kabwe hadi ACT wazalendo itakapokufa

Laana ya mzee Membe itaendelea kumtafuna Zitto Kabwe hadi ACT wazalendo itakapokufa

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Kitendo cha KC wa ACT wazalendo Zitto Kabwe kumtelekeza mgombea wa chama chake mzee Membe na kumuunga mkono Tundu Lisu wa Chadema wakati wa uchaguzi mkuu hakikuwa cha kiungwana kabisa.

Kwa sasa Zitto Kabwe anafanana na Augustino Lyatonga Mrema kwa kila kitu katika medani za siasa.

Laana ya mzee Membe itamuandama Zitto Kabwe na Saccos yake ya ACT wazalendo hadi saccos hiyo itakapokufa.

Juzi kaipongeza CCM kwa ushindi mnono wa Buhigwe na akasema uchaguzi ulikuwa wa haki Leo anasema atakata rufaa mahakamani uchaguzi haukuwa huru, ndio dalili za kuanza kuokota makopo hizi.

Heri Chadema wanasubiri Tume huru ya uchaguzi.

Jumamosi: Simba 5 Kaizer Chiefs 0
 
Bwashee usiwe kama umelewa mbege!

Membe hakuwa na hela kama Lowasa ndio maana akazinguliwa.
 
Back
Top Bottom