Laana ya Wenger yamtafuna Alexis Sanchez

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Huyu mchezaji alipokuwa Arsenal alijishebedua sana akikataa kusaini mkataba mpya ili aongezewe mpunga , Mzee Wenger hatimaye akasalimu amri na kuamua kumsalimisha kwa Bwana matamaa aitwaye Morinho , ambaye kwa vile hakuwa na uchungu na hela za watu akaamua kumlipa Sanchez mihela ya kufa mtu .

Kwa bahati mbaya kinyongo na laana ya Wenger vikamfuata Alexis kila alipogusa mpira , akaanza kustukiwa na kupigwa benchi , na baada ya Morinho kuondoka hali imekuwa mbaya zaidi , na sasa anatafuta namba kwenye Ndondo cup .

Wenger ana nini lakini , mbona kila mchezaji anayeondoka kwa nyodo anaishia kubaya ?
 
Aliyelaaniwa ni yule aliyekiuka kiapo cha kanisa na baadaye kuamua kushirikiana na wauwaji

Mwacheni Mzee wa watu. Alikosa upadri kwa sababu zisizozuilika (Wakatoliki nao; mtu ananyimwa upadri kwa kuwa tu hajalelewa kwenye familia yenye baba na mama!!??!!). Mwacheni aepuke kula mihogo.
 

Ndivyo itakavyokuwa kwa Beno Kakolanya na Gadiel Michael...hawatacheza au kung'aa huko Simba..., mark mmy words...hakuna mchezaji wa Yanga aliyeleta nyodo na kuamua kwenda akafanikiwa huko...watacheza mwezi mmoja au miwili, na ndio utakuwa mwisho wao...
 
labda Gadiel , lakini Beno alidhulumiwa na Yanga
 
Wivu tu Kwasu Kwasu mnataka kuwakopa wachezaji kila siku signing fees za mikataba iliyopita hadi leo hamjamaliza ,wote wameondoka wainaidai Kwasu ,na Yondani angekuwa umri wa miaka 26 lazima tungemchukua mchezaji mzuri hawezi kufa ,njaa kwasababu yenu.vilaana visivyo na sababu haviwezi kumpata mtu majembe yatakamua kiroho safi
 
labda Gadiel , lakini Beno alidhulumiwa na Yanga

Yeye alikuwa msaliti...alishawishiwa aombe malipo yake kwa nia ya kuikomoa Yanga...watu wa Simba ndio waliomwendea baada ya kuwa nyota kwenye mchezo wa Yanga na Simba wa 0-0 kwa hiyo wakaona kuwa njia ya kuikomoa Yanga isiwe bingwa ni kutumia Beno kwani haina uwezo wa kumlipa...Mtu wa Simba akaenda kwenye kambi ya Yanga usiku wa manane na kumchukua Beno...Kama Beno angebaki ubingwa ungekuwa wa Yanga...kwa hiyo Beno ni msaliti...hatacheza mpira Simba...
 

Hakuna cha wivu hapo...utakuja kuniambia comrade...utaniambia...Mwache huyo Gadiel aende Simba hatacheza hapo...Beno naye hatacheza...Atakayecheza kidogo ni Ajibu kwani hajawahi kuisaliti Yanga kivile na yeye mwenyewe ni Simba...Beno pia ni Simba na kabla hajaja Yanga ilikuwa asajiliwe Simba lakini wapo baadhi ndani ya Simmba ambao hawakumtaka kipindi kile...ila kosa la Beno ni kutumika ili kuihujumu Yanga...Gadiel yeye hajitambui, pamoja na kuomba radhi lakini bado laana itamfuata tu tena kwa saana..ubishoo wake utamtokea puani...Malipo (ya usaliti) ni hapa hapa duniani.
 
Boss Iyo ni kazi lakini wanaangalia maslai
 
Boss Iyo ni kazi lakini wanaangalia maslai

Maslahi yawe ya haki na siyo kuhujumu timu nyingine...Kwa wale wasioyafahamu mazingira ya soka ya Tanzania wanaweza wakaona Gadiel na Beno hawakuwa na tatizo..Lakini kiukweli Gadiel na Beno walitumika kuihujumu Yanga..Gadiel alitumika kinamna..sina haja ya kufafanua hapa...Hii inadhihirishwa kwa namna alivyowazimia Yanga simu siku za mwisho kabla ya kwenda Simba...amekwenda huko kulipa fadhila...kama hakuwa na nia mbaya na Yanga asingeweza kuzima simu...Lakini huko hatacheza mpira..Pamoja na kwamba msimu uliopita Yanga haikuwa vizuri kitimu lakini ingeweza kuchukua ubingwa kamasiyo hujuma...hujuma nyingine ilikuwa ni ile ya viporo kwa timu fulani...Timu inakuwa na viporo mpaka mechi 10 wapi na wapi...
 
Nimesikia huku vijiweni kuwa Sanchez anahitajika na Inter Milan. Nilichogundua Inter wanafanya kazi kubwa sana kuinoa Man United na kuifanya iwe imara zaidi kuliko hata Ed Woodward.
 
Yondani alitoka Simba kwa sababu hizi hizi, nakukumbusha tu.
 
Yondani alitoka Simba kwa sababu hizi hizi, nakukumbusha tu.
Sikatai wachezaji wanapaswa kuangalia maslahi ata Mimi kama naidai club signing fee ya msimu uliopita na wakati huu wananipa nusu ,kiufupi ni kurundika deni lisilolipika wakati wanafanya hivyo wanasajiri wachezaji wengine kwa Pesa ndefu Mimi wa zamani nakopwa ,sio fair
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…